Ibrahim ajibu na dunia ya peke yake!

Its Pancho

JF-Expert Member
Sep 21, 2018
14,184
22,586
Tunaishi kwenye dunia hii moja, wote kwa pamoja, tunaishi kwa pamoja pia mzunguko wetu wa maisha ni mmoja!

Lakini kuna watu ni kinyume chake, wao wana mzunguko wao, maisha yapo kivyao, tabia kivyao!

Ibrahim ajibu, huyu mtu ana dunia ya peke yake!
Ni mmoja kati ya namba kumi bora kwa sasa kwa upande wa wazawa na wageni pia! (baadhi)
Huwa namshangaa sana ajibu anauchukulia mpira kirahisi!
Yaani anaufanya kama mzaha na masikhara kwake, na mpira unamtii bila shuruti!
Mpira unampenda ajibu ila yeye anauona rahisi mno,anaufananisha na kunywa maji! Mtu wa ajabu huyu! Mvivu wa mazoezi, lakini bado mpira unamtii!
Nijikite kwenye Mada zaidi..
Nimeskia ajibu kashaanza mazungumzo na club yake ya zamani simba!
Well sio jambo baya yeye kurudi alipotoka! Na wala sio jambo zuri yeye kurudi alipotoka zaidi ya yeye kuwa vizuri kimaslahi!

Kama ninavyosema ajibu anauchukulia mpira kimasihara sana na ndo maana mpaka sasa yupo yanga jambo baya zaidi hajali kuhusu maslahi yake yeye anauchukulia mpira kama starehe!
Halitokua kuwa jambo la ajabu yeye kuongeza mkataba yanga!
Ingekuwa vipi kama mbwana samatta angeendelea kubaki simba mpaka Leo?
Sio ajabu sasa angekuwa ndanda! Au mwadui!
Kwanini? Sababu mpira ni short career Leo unacheza baada ya miaka kumi tayari mpira unaanza kukukataa!
Wakati mwingine huwa nafikiri sababu ya wachezaji wetu wengi kutokucheza nje ni sababu ya uongozi unaowasimamia
lakini pia hakuna wakala asiyetaka kumsimamia mchezaji mzuri!
Jambo la msingi ni kwenda na wakati, muda haukusubiri!
Kwa sasa soka la ulaya limejaa wachezaji aina ya ajibu.
Wasiotumia nguvu nyingi.
Akili nyingi..
Wenye jicho mbele ya goli!
Na kizuri zaidi ajibu ni kiungo!
Anaweza kutumika nyuma ya striker na akafanya vizuri! Ukizingatia kwa sasa viungo wa aina hiyo wapo wachache!
Ni wakati sasa wa ajibu kufikiria career yake na maisha yake pia nikimaanisha maslahi!
Mpira ni pesa na pesa iko miguuni kwake!
Naunga mkono ajibu kurudi Simba (sipo kishabiki hapo)
Leo hii mchezaji kama samatta
Akifikisha miaka 30 anaweza kuanza kusomea kozi ya ukocha huko kwa wazungu huku anamalizia soka lake!
Baada ya muda pale Genk anaweza kupewa team ya vijana akaanza nayo huku anapiga pesa huku anatengeneza jina kwa kupitia taaluma nyingine ya ukocha!
Yote haya yanakuwa ukiwa ulaya tofauti na huku kwetu Africa!

"Pancho boy "
 
Wac
Tunaishi kwenye dunia hii moja, wote kwa pamoja, tunaishi kwa pamoja pia mzunguko wetu wa maisha ni mmoja!

Lakini kuna watu ni kinyume chake, wao wana mzunguko wao, maisha yapo kivyao, tabia kivyao!

Ibrahim ajibu, huyu mtu ana dunia ya peke yake!
Ni mmoja kati ya namba kumi bora kwa sasa kwa upande wa wazawa na wageni pia! (baadhi)
Huwa namshangaa sana ajibu anauchukulia mpira kirahisi!
Yaani anaufanya kama mzaha na masikhara kwake, na mpira unamtii bila shuruti!
Mpira unampenda ajibu ila yeye anauona rahisi mno,anaufananisha na kunywa maji! Mtu wa ajabu huyu! Mvivu wa mazoezi, lakini bado mpira unamtii!
Nijikite kwenye Mada zaidi..
Nimeskia ajibu kashaanza mazungumzo na club yake ya zamani simba!
Well sio jambo baya yeye kurudi alipotoka! Na wala sio jambo zuri yeye kurudi alipotoka zaidi ya yeye kuwa vizuri kimaslahi!

Kama ninavyosema ajibu anauchukulia mpira kimasihara sana na ndo maana mpaka sasa yupo yanga jambo baya zaidi hajali kuhusu maslahi yake yeye anauchukulia mpira kama starehe!
Halitokua kuwa jambo la ajabu yeye kuongeza mkataba yanga!
Ingekuwa vipi kama mbwana samatta angeendelea kubaki simba mpaka Leo?
Sio ajabu sasa angekuwa ndanda! Au mwadui!
Kwanini? Sababu mpira ni short career Leo unacheza baada ya miaka kumi tayari mpira unaanza kukukataa!
Wakati mwingine huwa nafikiri sababu ya wachezaji wetu wengi kutokucheza nje ni sababu ya uongozi unaowasimamia
lakini pia hakuna wakala asiyetaka kumsimamia mchezaji mzuri!
Jambo la msingi ni kwenda na wakati, muda haukusubiri!
Kwa sasa soka la ulaya limejaa wachezaji aina ya ajibu.
Wasiotumia nguvu nyingi.
Akili nyingi..
Wenye jicho mbele ya goli!
Na kizuri zaidi ajibu ni kiungo!
Anaweza kutumika nyuma ya striker na akafanya vizuri! Ukizingatia kwa sasa viungo wa aina hiyo wapo wachache!
Ni wakati sasa wa ajibu kufikiria career yake na maisha yake pia nikimaanisha maslahi!
Mpira ni pesa na pesa iko miguuni kwake!
Naunga mkono ajibu kurudi Simba (sipo kishabiki hapo)
Leo hii mchezaji kama samatta
Akifikisha miaka 30 anaweza kuanza kusomea kozi ya ukocha huko kwa wazungu huku anamalizia soka lake!
Baada ya muda pale Genk anaweza kupewa team ya vijana akaanza nayo huku anapiga pesa huku anatengeneza jina kwa kupitia taaluma nyingine ya ukocha!
Yote haya yanakuwa ukiwa ulaya tofauti na huku kwetu Africa!

"Pancho boy "
Wachezaji wengi wa Tanzania wana vipaji vikubwa tuu ila wana tatizo moja hawajitambui. Ajibu naye kama wengine hajitambui. Namaanisha wanapofikia timu kubwa wakapewa mi sifa, wakaandikwa kwenye magazeti basi wanaona wameishaiteka Dunia kumbe wanatakiwa waende mbali hasa na wapate maslahi ya maana.

Tunapomzungumzia Samata ni mfano wa wachezaji wanaojitambua na kujiamini. Fikiria alikataa kucheza Simba wakati huo akiwa mdogo anachipukia hadi apewe ahadi ya gari aliyoahidiwa. Huko ndio kujitambua kuwa unathamani na unataka thamani yako ilipe. Kwa hiyo Ajibu namba kumi wa timu yangu anafurahia kusifiwa bongo na kupita mtaani anaitwa staa na kusumbua timu za bongo.
 
Wac

Wachezaji wengi wa Tanzania wana vipaji vikubwa tuu ila wana tatizo moja hawajitambui. Ajibu naye kama wengine hajitambui. Namaanisha wanapofikia timu kubwa wakapewa mi sifa, wakaandikwa kwenye magazeti basi wanaona wameishaiteka Dunia kumbe wanatakiwa waende mbali hasa na wapate maslahi ya maana.

Tunapomzungumzia Samata ni mfano wa wachezaji wanaojitambua na kujiamini. Fikiria alikataa kucheza Simba wakati huo akiwa mdogo anachipukia hadi apewe ahadi ya gari aliyoahidiwa. Huko ndio kujitambua kuwa unathamani na unataka thamani yako ilipe. Kwa hiyo Ajibu namba kumi wa timu yangu anafurahia kusifiwa bongo na kupita mtaani anaitwa staa na kusumbua timu za bongo.
Kabisa... Wanalemaa mapema wkt safari bado
 
wachezaj wanadanganya umri wakina kagere, okwi, wawa wako over 40 na samata ni mmoja wapo yuko over 30
Tumeongelea zaidi maslahi badala ya umri!
Kwanini kina kagere hawataki kwenda nje kula pesa na badala yake wapo hapa??
Jibu ni kuwa wanajua umri unaenda hawawezi kucheza ligi za ushindani tena!
Ndo maana wapo hapa.. na kizuri zaidi wanalipwa vizuri nn shida?? Waende wapi ikiwa kagere analipwa mil 12 na nusu ambayo yeye anaona inamtosha??
 
Back
Top Bottom