LAAM RASHIDI
Member
- Sep 12, 2016
- 44
- 66
1-Najiuliza sana ni watanzania wangapi kati ya milioni 50 tuliopo tunaweza kulipa nauli ya ndege kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine au kutoka nchini kwenda nje ya nchi? Ukweli ni wachache sana!
2-Najiuliza sana ni watanzania wangapi kati ya milioni 50 tuliopo tunaweza kununua vocha ya sh.500 kila siku na kuziweka katika simu zetu? Ukweli ni wengi sana tunaweza kumudu kuweka vocha kila siku!
3-Mheshimiwa Rais wangu kulikuwa na haja kubwa sana kuanza kuifufua kwanza kampuni yetu ya kizawa ya simu (TTCL) kabla hata ya kuifufua ATCL,ni ukweli uliowazi biashara ya mitandao ya simu inakua kila uchwao leo duniani kote,kampuni za nje zimewekeza hapa nchini na zinajiendesha kwa faida siku zote,watanzania tunatamani sana kutumia mtandao wetu kuliko kuendelea kuitumia hii ya kigeni,Mheshimiwa kulikuwa na haja kubwa sana kuiboresha TTCL kabla hata ya ATCL,mapato yangepatikana maradufu kwa kuwa wananchi wengi wangeitumia huduma ya kampuni lakini pia tungetengeneza ajira kwa vijana wengi sana watakaojishughulisha na uuzaji was bidhaa za TTCL mf.vocha za simu nk.
TTCL inahitaji kuendeshwa na vijana waliopo katika biashara hii kwa muda mrefu sana,vijana wenye mtazamo wa kibiashara na vijana wazalendo waliopo nchini.
Mf.KELVIN TWISA,EPHRAIM MAFURU ni aina ya vijana tuliowaona wakifanya makubwa kule waliko.
Mheshimiwa Rais TTCL ni kampuni tukiisimamisha vyema kabisa itatuingizia mapato mengi sana kupitia kwetu wananchi kuliko hata ATCL.
2-Najiuliza sana ni watanzania wangapi kati ya milioni 50 tuliopo tunaweza kununua vocha ya sh.500 kila siku na kuziweka katika simu zetu? Ukweli ni wengi sana tunaweza kumudu kuweka vocha kila siku!
3-Mheshimiwa Rais wangu kulikuwa na haja kubwa sana kuanza kuifufua kwanza kampuni yetu ya kizawa ya simu (TTCL) kabla hata ya kuifufua ATCL,ni ukweli uliowazi biashara ya mitandao ya simu inakua kila uchwao leo duniani kote,kampuni za nje zimewekeza hapa nchini na zinajiendesha kwa faida siku zote,watanzania tunatamani sana kutumia mtandao wetu kuliko kuendelea kuitumia hii ya kigeni,Mheshimiwa kulikuwa na haja kubwa sana kuiboresha TTCL kabla hata ya ATCL,mapato yangepatikana maradufu kwa kuwa wananchi wengi wangeitumia huduma ya kampuni lakini pia tungetengeneza ajira kwa vijana wengi sana watakaojishughulisha na uuzaji was bidhaa za TTCL mf.vocha za simu nk.
TTCL inahitaji kuendeshwa na vijana waliopo katika biashara hii kwa muda mrefu sana,vijana wenye mtazamo wa kibiashara na vijana wazalendo waliopo nchini.
Mf.KELVIN TWISA,EPHRAIM MAFURU ni aina ya vijana tuliowaona wakifanya makubwa kule waliko.
Mheshimiwa Rais TTCL ni kampuni tukiisimamisha vyema kabisa itatuingizia mapato mengi sana kupitia kwetu wananchi kuliko hata ATCL.