Duh! Unatakiwa kujikomboa kutoa utumwa wa fikra. Nimefanya Bsc IT kama wewe, sijawahi kuajiriwa. Kwanza nilianza kufanya kazi zinazoendana na profession yangu kwa kutumia laptop yangu nlokuwa natumia chuoni (TECRA A8 na specs za chini balaa, nakumbuka enzi hizo nlinunua 1.6M kwa pesa iliyotokana na hustle za likizo), baadaye mambo yalininyookea kiasi nikaregister kampuni nikawa naofisi ambayo ni duka pia nafanya retail ya vifaa vihusianavo na IT. Baada ya mafanikio mafupi kuna jambo liliingia kati nikapotea mpaka nikatelekeza "kampuni".....wanaoamini katika mambo ya giza wakaanza kusema nimerogwa na bwana mmoja niliwahi kufanya nae kazi moja kwa muda fulani japo yeye ni mtu prominent sana na ana mafanikio makubwa sana, walinong'ona kwamba wengi waliopishana kauli na huyo jamaa walipotea na hawakurudi tena kwenye ulimwengu wa biashara. Mimi nilifaham vizuri tatizo na sehem niliyokosea hvo niliwaacha waongee huku mimi nikipanga naanzaje, maana nilipoteana hasa kwa takribani mwaka mzima. Baadaye bwana mmoja alikuwa rafiki yangu sana akawa ananifuata nyumbani kila baada ya siku kadhaa, ananisalimia na kuniachia pesa kidogo, laki, elfu hamsini na kunishawishi nirudi mjini, lakini kutokana na hali nilokuwa nayo na hadhi yangu uchwara haikuniwia rahisi kurudi na kuanza moja. Baadaye nilikubaliana naye baada ya yeye kunishawishi, aliniambia kauli moja tu ambayo ilinipa nguvu ya ajabu..."Rene, wewe ni zaidi ya rafiki yangu, nakufaham vizuri sana, nafaham uwezo ulionao kichwani. Mimi mwenzako bado nimesimama nasonga, sina cha kukupa, lakini naamini tukiunganisha nguvu....kichwa ulichonacho na rasilimali kiasi nilizonazo tutatengeneza kitu kikubwa". Siku hiyo aliniacha nikiwaza sana, kumbe mimi huyu nayejiona ni total failure kuna watu wanaoniona vingine. Nilisema "huyu si mimi, I'm not a coward lazy retard", kesho yake saa moja na nusu nilifikka ofisini kwake nikiwa na na laptop yangu begani, jamaa alinitazama mara moja tu akatabasamu na kunambia "welcome aboard soldier", miaka kadhaa sasa tuna kampuni tatu za pamoja, anayo moja ya kwake na nina mbili za kwangu tunapasua anga, watu wanalia mwaka mgumu lakini huwezi amini kwetu sisi toka Magu aingie madarakani neema inatudondokea tu, kila kazi tunayoomba tunapata! Kuna siku tunagombana nusu ya kupipgana, lakini baada ya muda kidogo tumeshayasahau! Amini nakwambia, kazi ya kuajiriwa itakudumaza akili!