Huyu ndo mke wa Lutu

Huyu ndo mke wa Lutu aliebadilika kuwa jiwe la chumvi [emoji849]

"""Kitu gani kilipelekea mke wa Lutu ageuke nyuma?

View attachment 2246532
MKE WA LUTU ALIGEUKA JIWE LA CHUMVI.

Simulizi la Biblia kuhusu Lutu hupatikana Agano la kale kwenye kitabu cha Mwanzo sura ile ya 19. Katika sura hiyo ya 19 ukisoma mstari wa 1 hadi 11 utaona habari za malaika wawili waliomtembelea mtu wa Mungu ambaye ni Lutu wakimpasha habari kuhusu uharibifu uliokuwa karibu kulipata jiji la Sodoma alikoishi yeye na familia yake., Jiji hilo lingeangamizwa kutokana na dhambi nzito walizokuwa wakifanya wakaaji wake. Lakini pia, utakutana na vitimbi walivyofanyiwa malaika hao wawili kutoka kwa wakazi wa mji huo mwovu.

Mstari wa 12 Lutu anaagizwa na malaika wale kuwapasha habari ndugu zake wote walioishi jijini hapo ili waondoke naye kupisha uharibifu wa jiji hilo uliokuwa karibuni kutimizwa. Mwitikio wa ndugu zake ulimvunja sana moyo. Simulizi husimulia kuwa Lutu alipoongea nao kuhusu onyo hilo, machoni pao alionekana kama mtu anayefanya mzaha tu. Hawakumsikiliza!

Baada ya malaika hao kuona kuwa Lutu alikuwa akipoteza muda kuwaonya watu hao wenye kiburi, waliamua "kumtwaa" yeye, mke wake, pamoja na binti zake wawili na kuwatoa nje ya jiji hilo, kisha wakawaambia hivi: β€˜Kimbieni ili kuokoa uhai wenu! Msitazame nyuma, mkitazama nyuma mtakufa!’ Hata hivyo mke wa Lutu hakutii agizo hilo. Walipotembea umbali fulani kutoka Sodoma, tayari vishindo na ngurumo za kutisha zilikuwa zikisikika nyuma yao kuashiria kizaazaa kilichokuwa kikilipata jiji hilo ovu. Huenda Lutu alitamani "kugeuka nyuma" ili kushuhudia tukio hilo la kutisha, lakini alijizuia kwa sababu alikumbuka maagizo ya malaika wale wawili, 'Mkitazama nyuma mtakufa!' Wakiwa mbioni kuelekea mbali zaidi na uharibifu ule uvumilivu ulimshinda mke wa Lutu, mwanamke huyo alisimama na kutazama nyuma, lakini palepale aligeuka kuwa jiwe la chumvi!

Unaweza kuwazia jinsi Lutu mtumishi wa Mungu alivyojisikia baada ya ghafla mke wake kusimama? Hatujui Lutu alisema nini, lakini huenda alimwita mkewe kwa sauti kubwa huku akiendelea kukimbia akisonga mbele pamoja na binti zake wawili aliokuwa amesalia nao. Lazima mtu huyo alitamani sana kugeuka nyuma ili kufahamu kilichokuwa kimempata mkewe, lakini hangethubutu kufanya hivyo kwa sababu aliheshimu na kumwogopa sana Mungu!

*Tunajifunza nini kutokana na simulizi hili la Biblia? Hizi ni nyakati za mwisho, tunaelekea kwenye ukomo wa mfumo huu uliopotea. Tunapohubiriwa kuacha mabaya tunapaswa kutii. Mungu huokoa wale wanaotii maagizo yake, lakini wale wasiotaka kusikiliza maonyo yake huwaacha waangamie!

Biblia kuna simulizi nyingi sana zenye kufundisha, kutia moyo na kutufariji. Kisa hiki kuhusu Lutu kinapatikana kwenye Biblia, kitabu cha Mwanzo sura ya 19.

C&P
 
Barikiwa kwa uchambuzi mzuri
 
Asante
Asante
 
Ubarikiwe sana
 
πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ ila wabongooo mkuu umefikiria nini kuanzisha uzi huu
 
Ni kweli kabisa.

Miji ya Dodoma Na Gomola ilikuwa Katika nchi ya Islael.
Kwa sasa miji Ile inapatikana Katika Mji wa Jericho YERIKO.

YERIKO NI MJI AMBAO UNA SIFA ZIFUATAZO

1. Kinapatikana kichuguu cha Mke Wa Rutu.

2.Ni Mji ulio chini zaidi Duniani, kutoka usawa wa Bahari.

3. Mji ambao inapatikana Bahari mfu. Yani Dead sea. Hakuna kiumbe chochote ndani ya hayo maji,
Binadamu hazami Wala hawezi kufa ndani ya maji kutokana na chumvi Kali sana.

4. YERIKO imekufa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…