Huyu ndiye Prof. Abdulrahman Mohamed Babu!

pamoja na kiu ya Babu kuitawala Zanzibar kwa njia yeyote lakini kitu ninachoamini na kinachoaminika na wengi ni kuwa kama angetawala, Zanzibar ingekuwa mbali mno kutokana uwezo wake Prof. Babu.
 
Katika kitabu cha Prof.Babu kiitwacho African Socialism or Socialist Africa? ndicho pengine kinaonyesha Babu alikuwa na mrengo gani.Kifupi ni kwamba ni kweli Prof.Babu alikuwa mjamaa.Tofauti na Mwalimu Nyerere ilikuwa ni namna ya kutekeleza sera za ujamaa.Prof.Babu alikuwa anataka Scientific Socialism,ujamaa unaotokana na mazingira ya nchi za kiafrika,kuliko kuiga kila kitu kutoka mataifa ya ujamaa kama vile Uchina.Maana inasemekana Mwalimu Nyerere alichukua sera za ujamaa kutoka China (hasa sera ya vijiji) ambayo baadae wote tunajua nini kilichotokea.
...Prof. Babu alikuwa mjamaa ambaye aliweza kuuona ukweli wa kile kilichokuwa kinaendelea duniani kiuchumi na kisiasa. Hii inaonekana dhahiri miaka ya mwishoni mwa uhai wake, katika machapisho aliyoyafanya, kama, lile linaloongelea "the second liberation of africa".

...Nimevutiwa na jinsi alivyoweza kuyachambua maendeleo ya nchi mbalimbali -angalau kwa ufupi sana- na kuonyesha jinsi gani tunavyodanganywa na IMF & Co. na kutekeleza sera zinazoonyesha tunaendelea -kwenye takwimu- huku tukishusha ubora wa maisha ya wananchi walio wengi, kwa kuongeza lindi la umaskini.

...Pengine, mchango wake wa muhimu kwenye hilo chapisho ni kuonyesha wazi kuwa, bila maendeleo ya viwanda, tena vilivyowekwa kwenye sekta na maeneo fulani kimkakati, hatutaweza kuwa na maendeleo ya kweli, na hivyo kujikomboa.

...He is a jewel in many stones.
 

Ni vigumu sana kueleza kwa ufasaha kwanini Babu aliondolewa kwenye Baraza la Mawaziri tena akiwa nje ya nchi.Lakini watu wengi sana wanaamini kwamba Prof.Babu aliondolewa kwenye uwaziri kutokana na shinikizo kutoka kwa Karume ambaye alikuwa anaona hatari ya kupinduliwa huko Zanzibar.Na wanachama wa Umma Party wakiongozwa na Babu walikuwa wanaogopwa sana na Karume.Hivyo walitakuwa kurudishwa Zanzibar ambako wangekabiliana na mkono wa Karume.Pamoja na hilo,Mwalimu Nyerere hakupenda sana jinsi Karume alivyokuwa anawashughulikia wapinzani wake,lakini alilazimika kwani alikuwa tayari kwa lolote ili mradi Muungano uweze kudumu.
 
...kwamba Prof.Babu aliondolewa kwenye uwaziri kutokana na shinikizo kutoka kwa Karume ambaye alikuwa anaona hatari ya kupinduliwa huko Zanzibar....
Kama ndio hivyo basi alipokuwa fired angerudishwa Zanzibar au angekamatwa. Sasa mtu mnaeogopa atapindua nchi ukimtoa kwenye uwaziri ukamwacha mtaani ndio anakuwa sio hatari?

Ni vigumu sana kueleza kwa ufasaha kwanini Babu aliondolewa kwenye Baraza la Mawaziri tena akiwa nje ya nchi.
Ndio maana ninadharau sana media na wanahistoria wa Tanzania, Nyerere amekufa na siri hizo, Karume amekufa na siri hizo, Babu amekufa na siri hizo, Kawawa ambae labda angejua jua, amekufa na siri hizo, hakuna aliyekuwa na kende au udadisi wa kumuuliza Nyerere mambo haya, na nikasema wakati wa msiba wa David Wakati, kwamba Tanzania haikuwahi kuwa na media wakati ule na mpaka leo haina wana historia. Mambo mengi bado hayajulikani badala yake tunadanganywa tu.
 
Hivi Abdularahman Mohamed Babu aliwahi kuwa Profesa? Sikumbuki. Nikumbusheni.

Nilisikia alikuwa Sharifu na kule kwetu masharifu wanaheshimiwa kama sio kuogopwa. U prof usije ukawa kama ule wa usharifu
 
Upinzani wa Babu dhidi ya Nyerere ulikuwa ni wa kisomo!!..................................pichani MALCOLM X alipokuja Tanzania akiwa na Abdul-Rahman BABU...........................................
Abdulrahman Mohamed Babu was born in 1924 in Zanzibar, East Africa - then a British protectorate. He described his childhood in a brief autobiographical sketch which was intended to form the basis of memoirs which he had been commissioned to write (African Socialism or Socialist Africa?[SUP][citation needed][/SUP]), but which were always postponed by more immediate work relating to contemporary struggles.
Babu was among the Afro-Shirazi Party ‘intellectuals' from Zanzibar who had fallen out with Abeid Karume, the leader of the Zanzibar Revolutionary Council. Following the merger between Tanganyika and Zanzibar in April 1964, he was among the progressive, leftist members of the Zanzibari government sent to take up cabinet positions in Dar es Salaam[SUP][1][/SUP].
As a Secretary of the Zanzibar Nationalist Party prior to the Union, Babu had built close relations with the Chinese leadership and was probably the first liberation fighter from East and Central Africa to visit China in 1959. As a result, the British called him ‘the best known Sinophile' in Tanzania. His ideological affinity and work with the New China News Agency made him a good channel of communication with Beijing.[SUP][1][/SUP]
Babu had a key role to play in the establishment of TAZARA Railway with the help of Chinese aid. According to his memoirs, Julius Nyerere wanted to build on Zanzibar's close ties with China and create benefits for the whole country. Babu was named head of the trade delegation that preceded Nyerere's presidential delegation to China in 1964. The outcome of his trip was a trade agreement (separate from the £11 million aid agreement) for £5 million a year for five years. Under this agreement the Tanzanians were to buy whatever they could afford from the Chinese but the Chinese were to buy £5 million worth a year from Tanzania. The Chinese would pay cash for the balance not taken up by purchases from Tanzania. Due to his personal experience with the Chinese and his ideological affinity for their progressive model of development, Babu seized the initiative and mentioned the difficulties his government faced in trying to secure financing for the TAZARA Railway. On 1 July 1965 the Chinese Government made a firm offer of tied aid to the Governments of Tanzania and Zambia, worth £75 million and £150 million to enable them to build the railway line.[SUP][1][/SUP]
A few years later Babu was sentenced to death along with 34 other people, 23 others were acquitted for their alleged role in the 1972 assassination of the then Zanzibar President, Sheikh Abeid Amani Karume. Babu and 12 other prisoners who were held on the Mainland were freed by the then President Julius Nyerere in an amnesty to mark the 14th anniversary of the Union of Tanganyika and Zanzibar in April 1978.
The veteran politician, Abdulrahman Mohamed Babu,72, died on August 5, 1996 at the London Chest Hospital after a short illness. Babu, who had been staying in London for years as a scholar. He returned to Tanzania one year before his death from exile in London since 1978 when he was freed in an amnesty after being sentenced to death in 1973 for Treason................................................

[h=2]Positions held[/h] Chair - Africa Centre (London) (1985–1989)
Foreign Minister (Jan 1964 - Apr 1964)
Founder - Umma Party (Zanzibar) (1963)
Secretary General - Zanzibar Nationalist Party (1957–1963)
Minister of Planning
He was picked NCCR-Mageuzi presidential running-mate. However, the charges against and consequent conviction of the late Prof Babu led to the Electoral Commission to reject his bid to run for the Vice-Presidency.
[h=2]Publications[/h]
 

Attachments

  • clip_image002.jpg
    clip_image002.jpg
    18.1 KB · Views: 94
Joseph Mihangwa Toleo la 355 28
<< Makala iliyotangulia
Abdulrahman Babu
Joseph Mihangwa
jmihangwa@yahoo.com
More information about text fo

JUKUMU la kuteka Kituo cha Polisi cha Malindi na
Magereza alipewa Amour Mohamed Dugheish;
wakati jukumu la kuteka “Cable and Wireless ”,
Kituo cha Redio na Uwanja wa ndege, alipewa
Hashil Seif Hashil na wengine kupewa maeneo
mengineyo muhimu.
Na huu ndio uhalisia wa mambo yalivyokuwa
kiasi kwamba duru za Kibalozi Visiwani wakati
huo zilinukuliwa zikisema, “Afro-Shiraz ndio
wanaotoa askari, lakini UMMA Party ndio
wanaoratibu na kudhibiti mipango yote ya
Mapinduzi” hadi ushindi (Smith, William, 1971).
Ni kwa sababu hii haishangazi kuona kwamba,
baada ya Mapinduzi hayo, wapiganaji wa UMMA
Party ndio pekee waliounda Jeshi la kwanza la
ukombozi la Watu wa Zanzibar – “Zanzibar
Peoples’ Liberation Army” (ZPLA), likiongozwa na
Komandoo, Kanali Ali Mahfoudh.
Kwa kifupi, Mapinduzi haya yalianza kama
“maasi” tu ya walalahoi wa mjini waliokata
tamaa ya maisha kwa lengo la kuchoma moto na
kuteketeza mji wa Zanzibar.
Ni pale tu yalipoingiliwa na Wanamapinduzi
wenye taaluma hiyo, makada wa UMMA Party
waliofunzwa kisiasa na kijeshi, kwamba maasi
hayo ya walalahoi yaligeuka kuwa “maasi” ya
kimapinduzi. Na kama alivyosema Babu baadaye
kwamba, “……..Mabadiliko hayo ambayo
hayakutarajiwa siku hiyo, yalifungua mengi:
kutoka malalamiko mlipuko kuwa maasi yenye
kuongozwa na itikadi ya chama (UMMA); kutoka
matarajio finyu ya utaifa kuwa mapinduzi ya
kijamii; na kutoka giza nene lisilo na matumaini
hadi kufunguka kwa taswira ya matumaini,
muhimu katika kujenga mfumo mpya wa kijamii.
Yote haya yalichochea ghadhabu ya mataifa ya
kibeberu…..”.
Nyerere, Uingereza wagoma kuyatambua
Mapinduzi
Nchi za Kisoshalisti hazikupoteza muda wala
nafasi katika kuyatambua Mapinduzi; Urusi,
China, Czechoslovakia, Vietnam na Ujerumani
zote mbili (Mashariki na Magharibi) ziliyatambua
Januari 13, na kuleta hima misaada mingi
mikubwa, ya kijeshi na ya kiuchumi. Zanzibar
ikakaribisha pia wataalamu kutoka China,
Ujerumani Mashariki na Urusi.
Urusi pekee ilileta meli iliyojaa magari, mizinga na
bunduki kubwa za kutungua ndege na vifaru
pamoja na silaha mzo mzo. Na mwishoni mwa
Februari 1964, Babu akatangaza kupokelewa kwa
msaada wa Shilingi za Kizanzibari 3,700,000/=
kutoka China akisema, “Huo ni mwanzo tu wa
makubwa yajayo”.
Majina ya kikoloni yalibadilishwa haraka, badala
yake yakawekwa majina ya Kikomunisti. Kwa
mfano, Uwanja wa Taifa ukaitwa “Mao Tse-
Tung”; shule moja ikapewa jina la
Mwanamapinduzi wa Cuba, “Fidel Castro”;
Hospitali ya Taifa ikaitwa “V. I. Lenin” na
Madaktari wa Kichina wakafurika; Vyuo viwili
vikaitwa “Patrice Lumumba” na kingine “Kwame
Nkrumah”, na mengineyo.
Kwa nchi za Afrika Mashariki, Kenya iliyatambua
Mapinduzi Januari 13, na Uganda Januari 14;
wakati Rais wa Tanganyika, Mwalimu Nyerere,
alikataa kuyatambua Mapinduzi hayo akidai
hakuwa na uhakika kama kweli Karume alikuwa
ameshika madaraka; bila shaka kwa maana
kwamba hakupendelea Zanzibar kuwa mikononi
mwa Wakomunisti.
Katika kipindi hicho, wakati Serikali mseto ya
Mapinduzi ya UMMA Party na ASP ikijaribu
kusimama kwa miguu yake, Uingereza na
Marekani, kwa hasira, ghadhabu na hofu ya
Zanzibar kughubikwa na Ukomunisti, ilipanga
mikakati mbalimbali kukomesha hali hiyo,
ukiwamo mkakati wa kuivamia Zanzibar kijeshi;
kumuua Babu au kuunda Shirikisho la Nchi za
Afrika Mashariki (EAF) ili Zanzibar imezwe ndani
ya tumbo kubwa la EAF isifurukute. Na kama
yote hayo yakishindwa, basi, liundwe Shirikisho la
Tanganyika – Zanzibar kwa madhumuni hayo
hayo ya kuidhibiti Zanzibar
Marekani na Uingereza zapata hofu
Tangu mwanzo, Serikali za Uingereza na Marekani
hazikufurahishwa na harakati za Kikomunisti
Visiwani Zanzibar, harakati ambazo hatimaye
zilizaa Mapinduzi, Januari 12, 1964.
Hofu ya mataifa hayo ya Magharibi ilikuwa ni juu
ya Zanzibar kugeuka kitovu cha kueneza
Ukomunisti ukanda wa Afrika Mashariki enzi hizo
za vita baridi kati ya nchi za kibepari za
Magharibi, zikiongozwa na Marekani na
Uingereza; na nchi za Kisoshalisti za Mashariki,
zikiongozwa na Urusi na China.
Hofu hiyo ilizidishwa na Mapinduzi hayo ya
Kikomunisti, na jinsi Zanzibar ilivyofungua
milango haraka haraka kwa China na Urusi na
namna zilivyomwaga misaada ya kijeshi na ya
kiuchumi, huku Abdulrahman Babu, wakati huo
Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara,
akiitangazia dunia kuwa “huo (ulikuwa) ni
mwanzo tu”.
Alhamis, Januari 16, 1964, siku ya tano ya
Mapinduzi, Rais Karume, Hanga na Babu
walikwenda Dar Es Salaam kwa ndege
kumbembeleza Nyerere aitambue Serikali yao, pia
awape askari kwenda kurudisha amani na
utulivu.
Huku nyuma, Kiongozi wa Serikali, “Field Marshal”
John Okello, bila kujua juu ya safari ya Karume na
wenzake, akadai kwamba Karume hakushiriki hata
kidogo katika mapambano hivi kwamba
hakustahili kuwa Rais, japo Rais asiye na
madaraka.
Kwa hiyo jioni hiyo, Okello akafuta uteuzi huo na
yeye akajipa cheo cha Rais na Waziri wa Ulinzi;
na akamteua Karume kuwa Makamu wa Rais,
uteuzi ambao hakuutekeleza baada ya kupata
wazo la pili.
Haijafahamika bado walichozungumza Karume,
Hanga, Babu na Nyerere, lakini siku mbili
baadaye, askari polisi 300 kutoka Tanganyika
waliwasili Zanzibar kwa kazi iliyokusudiwa.
Itakumbukwa miaka mitatu kabla ya Mapinduzi
na miezi kadhaa kabla ya uhuru wa Tanganyika
Desemba 9, 1961, Rais Nyerere aliwahi kutamka
hofu yake kwa Zanzibar kuwa karibu na
Tanganyika, akisema, kama angekuwa na “uwezo
wa kukitokomeza kisiwa kile hadi katikati ya
bahari ya Hindi”, angefanya hivyo, kwa kuhofia
“usumbufu” na kutuumiza kichwa siku za
baadaye.
Hofu ya Mwalimu ambayo baadaye ilikuja
kujulikana kama “The Zanzibar headache”
(ugonjwa wa kuumiza kichwa kuhusu Zanzibar)
ilitokana, kwanza na harakati za uhuru za
Kikomunisti Visiwani zilizoongozwa na Babu enzi
hizo za vita baridi, kwamba huenda zingemtia
majaribuni juu ya msimamo wake kuhusu sera
zake za kutofungamana na upande wowote
Kimataifa iwapo suala la Zanzibar lingezua mzozo
kati ya mataifa makubwa, ikizingatiwa kwamba
yeye alikuwa mpenzi na kipenzi cha nchi za
Magharibi, hasa Uingereza.
Itakumbukwa pia kwamba mwaka 1957, wakati
harakati za Wakomunisti ndani ya ZNP zikichanja
mbuga kuelekea uhuru, Waingereza waliingilia kati
kwa kusaidia kuanzishwa kwa ASP ili kupunguza
kasi ya ZNP, pia Nyerere akiwa mmoja wa
waliosaidia. Kwa hiyo, hofu ya Mwalimu juu ya
harakati za Kikomunisti ilikuwepo tangu harakati
za uhuru hadi Muungano mwaka 1964.
Pili, Mwalimu aliogopa Zanzibar yenye migogoro
chini ya Sultani kama Mkuu wa nchi, kwamba
nchi hiyo ingeweza kutumika kama kituo cha
maadui kuishambulia Tanganyika. Hofu ya
Mwalimu juu ya Zanzibar kwa mambo hayo
mawili iliungana na ile ya Uingereza na Marekani
juu ya Zanzibar kuwa kitovu cha kueneza
Ukomunisti ukanda wa Afrika Mashariki, na kwa
sababu hiyo, Mwalimu akafunga nira na Mataifa
hayo.
Mazingira tangulizi
Kabla hatujatizama kuona namna mataifa ya
Magharibi yalivyojiingiza kudhibiti Ukomunisti
Zanzibar hadi shinikizo la Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar, ni vyema tuangalie
kwanza mazingira yaliyowezesha mchezo
kuchezwa na maandalizi ya mchezo wenyewe.
Kama hatua ya kwanza ya kindumbwendumbwe
hicho, Marekani ilimteua na kumhamishia
Zanzibar kutoka Congo (sasa DRC), Balozi na
Jasusi beberu la Shirika la Marekani (CIA), Frank
Carlucci kufanya kazi za kibalozi na kijasusi
Visiwani.
Ndani ya Serikali ya Mapinduzi namo hali
haikuwa shwari kwa wanaharakati wa mrengo wa
kushoto kumtuhumu Karume kushindwa
kusimamia na kuendeleza Mapinduzi. Kwa
sababu hii, wanaharakati wa Chama cha UMMA
ndani ya Serikali – Abdulrahman Babu, Khamis
Abdallah Ameir, Ali Sultani, Ali Mahfoudh, Salim
Rashid, Badawi Qullatein na wengineo,
walioanzisha uhusiano kuunda njama na wenzao
wa ASP wahafidhina wa sera za Kisoshalisti ili
kumpindua Karume.
Wanaharakati wa ASP walikuwa ni pamoja na
Abdallah Kassim Hanga, Abdulaziz Ali Twala,
Hassan Nassoro Moyo na wengineo. Karume na
wenzake wenye siasa mgando, wakaogopa. Na ili
aweze kuendelea kudhibiti madaraka Visiwani
asipinduliwe, aligeuka kumtegemea Mwalimu
Nyerere na Jeshi la Tanganyika Visiwani.
Kwa kipindi chote, Chama cha UMMA kilishinikiza
Hanga ateuliwe kuwa Waziri Mkuu Mtendaji na
Karume abakie kama Rais asiye na madaraka.
Ukweli, mwanzoni Hanga aliteuliwa Waziri Mkuu,
lakini Othman Sharrif akamchochea Karume
abadili uteuzi kwa kumuogofya. Uteuzi ukafutwa
siku hiyo hiyo, Hanga akanywea.
Uingereza, Marekani zaingia kazini
Ili kuhakikisha Ukomunisti hausimiki mizizi Afrika
Mashariki kupitia Zanzibar, Marekani ilibuni
mikakati ifuatayo: ilikuwa, ama kwa Uingereza
kuivamia Zanzibar kijeshi kwa msaada wa
Marekani; au kuunda Shirikisho la nchi tatu za
Afrika Mashariki – Kenya, Uganda, Tanganyika na
Zanzibar ambayo ingemezwa ndani ya Shirikisho
isiweze kufurukuta. Shirikisho la Tanganyika na
Zanzibar kuunda Tanzania lilikuja baadaye kama
ajali tu baada ya mikakati miwili ya kwanza
kushindwa.
Katika sehemu hii ya makala na kuendelea, kwa
kutumia vyanzo mbali mbali, zikiwamo simu za
maandishi ( telegraphs ) za kijasusi za Serikali za
Marekani na Uingereza kwa Mabalozi wao Afrika
Mashariki, na ambazo sasa zimeondolewa katika
orodha ya nyaraka za siri, tutaona namna
mpambano dhidi ya Ukomunisti ulivyoendeshwa
kufikia Muungano wa Tanzania.
Mambo yalianza Januari 13, 1964, siku moja
baada ya Mapinduzi na Okello akiwa tayari
ameunda Serikali yake kwa kumteua Karume Rais
wa Jamhuri ya Zanzibar na Pemba; pale Katibu
wa Jumuiya ya Madola na Waziri wa makoloni
wa Uingereza, Duncan Sandys, alipomwandikia
Rais wa Kenya, Jomo Kenyatta, kumwelezea hali
ya Visiwani akisema “….. Lakini Wajumbe wawili
wa timu ya Sheikh Karume, Bwana (Kassim)
Hanga na Bwana (Abdulrahman) Mohamed
(Babu) wanaaminika kuwa wafuasi wakubwa wa
Ukomunisti. Kama Serikali (ya Zanzibar), hatua
chache tu Pwani ya Afrika Mashariki itakuwa na
mwegemeo wa Kikomunisti, na pengine kuruhusu
vituo vya kijeshi kwa mataifa ya Kikomunisti,
litakuwa jambo hatari sana na la usumbufu
kwetu”.
Barua hiyo ambayo nakala walitumiwa Nyerere na
Obote, ilieleza kuwa, tatizo kubwa lilikuwa ni
Babu na Chama cha UMMA; akamtaka Kenyatta
awasiliane na Nyerere na Obote ili angalau
walizungumze.
Wakati huo Uingereza na Marekani zilikuwa
zimekataa kuyatambua Mapinduzi, kama njia ya
kumshinikiza Karume ajiweke mbali na Babu.
Naye Karume, kwa hasira akawatimua Balozi wa
Uingereza na Kaimu Balozi mdogo wa Marekani
Visiwani, Februari 19, 1964. Mabalozi hao
waliruhusiwa kurejea baada ya nchi zao
kuyatambua Mapinduzi, Februari 23, 1964, huku
nafasi ya Kaimu Balozi wa Marekani ikichukuliwa
na jasusi Frank Carlucci.

Itaendelea
 
Naomba kujua historia ya prof. Mohamed Babu.
mzee ; Mzee Mohamed Said na Ahmed Rajabu mtujuze
 
Ni katika watu wabaya sana waliowahi kutokea Tanzania.

Moja ya sifa yake kubwa aliyokuwa nayo niuwezo wa kuwashawishi watu, Anaweza akatukusanya akatupa darasa la dakika tano tu na baada yahapo kila mmoja akavaa bomu na kwenda kujiripua. Jamaa hakuwa mtu wakawaida kabisa.
 
Ni katika watu wabaya sana waliowahi kutokea Tanzania.

Moja ya sifa yake kubwa aliyokuwa nayo niuwezo wa kuwashawishi watu, Anaweza akatukusanya akatupa darasa la dakika tano tu na baada yahapo kila mmoja akavaa bomu na kwenda kujiripua. Jamaa hakuwa mtu wakawaida kabisa.


Je, hakuwa na mazuri hata kidogo??
 
Ni katika watu wabaya sana waliowahi kutokea Tanzania.

Moja ya sifa yake kubwa aliyokuwa nayo niuwezo wa kuwashawishi watu, Anaweza akatukusanya akatupa darasa la dakika tano tu na baada yahapo kila mmoja akavaa bomu na kwenda kujiripua. Jamaa hakuwa mtu wakawaida kabisa.
humjui utamfananisha na gaid kasome : AFRICAN SOCIALISM OR SOCIALISM AFRICA?
 
Je, hakuwa na mazuri hata kidogo??

Hakuwa mtu mzuri kabisa. Kuna mzungu mmoja aliwahi muandika kwenye kitabu chake akamzungumza jamaa alivokua kwa mujibu alivomfahamu.

Ila Alikua ni mwanasiasa aliebobea na mwenye uwezo mkubwa kiakili.
 
Back
Top Bottom