Johnny Sins
JF-Expert Member
- Nov 4, 2019
- 2,536
- 3,883
Hii ni picha ya hakimu katika jimbo la Ohio nchini Marekani anayeitwa Michael Scott. Hakimu huyu amevuta hisia za watu kutokana na hukumu anazozitoa dhidi ya wahalifu wanaokwenda kinyume na sheria kwa mujibu wa makosa yao.
Aliwahukumu watu 7 wapande miti 70 baada ya watu hao kukata miti katika eneo la umma na kuiuza kama kuni.
Alimhukumu kijana kuhudumu katika nyumba ya wazee kwa muda wa miezi miwili baada ya kijana huyo kumpiga mzee.
Alimhukumu mlevi mmoja kuwalisha chakula paka katika bustani moja ya wanyama kwa muda wa miezi miwili baada ya mtu huyo kumuweka paka wake katika oven.
Alimhukumu mwizi mmoja kusimama mbele ya duka aliloiba kwa muda wa wiki mbili akiwa amebeba bango lililoandikwa: “Wizi ni mbaya”.
Alimhukumu daktari mmoja kutoa mihadhara (lectures) ya bure katika vyuo mbalimbali kwa muda wa miezi 6 kuhusu madhara ya ulevi baada ya daktari huyo kukamatwa akiendesha gari akiwa amelewa.
