Nimetokea kuwa na mahusiano na huyu mwanamke lakini ameonekana akiwa na wivu kupindukia akipiga simu kama ujapokea ni matatizo hata kama ulikuwa umetoka kidogo ukaiacha analamika mpaka anataka kulia , amekuwa ni wa kulalamika tu kwa nini simu yake sipokei, ukimwahidi kitu ukashindwa kukitimiza analalamika kweli sina muda mrefu nae ni kama mwezi sasa,lakini ananitia wasiwasi kuendelea nae. naombeni ushauri je, huyu mwanamke anaweza kuwa mzuri baadae kweli.
Hata sasa huyo mwanamke ni mzuri sana tu. Ninachokiona huyo mwanamke yuko committed ila wewe ndio unazuga, yaani uko mguu ndani mguu nje.
Kinachotakiwa mkae chini muongelee aina ya mahusiano yenu. Inawezekana mwenzako anakuona mchumba, wewe unamuona ni rafiki tu wakupita.
Kama huyo mwanamke yupo humu na anasoma huu uzi, namshauri na yeye aishi kama vile mpita njia (aegeshe), asione kwamba amepata a man of her life.