Huyu mwanamke simuelewi

Huyu mwanamke simuelewi

Mr Eggo

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2012
Posts
2,028
Reaction score
1,051
Wasalaam wana jukwaa.

Ni matumaini yangu mko poa mnaendelea na mishe za maisha

Embu kwa pamoja tushirikiane kwenye kamkasa aka,,,katika pita pita zangu jijini apa nikabahatika kukutana na binti mmoja mzaliwa wa mkoa huu,,,kama kawaida tukaanza taratibu na hatimae tukakubaliana kuwa wapenzi, ( to be honest,,i miss gf and br life maana i have almost 7 month not into it,) nilifurahi angalau nimempata wa kusaidia majukum ya apa na pale ukizingatia naishi mwenyewe.

Uyu binti ni mrembo, rangi zangu zile, mambo ya rock city ndo usiseme (kitonga) ila tatizo likawa moja kuonana, kila nikifanya arrangement tuonane anaonekana kupata dharura, nimepanga zaidi ya mara tatu anapangua, last time ikabidi nimfate mimi ndo nikapata walau wasaha wa kuongea nae.

Kinachonifanya niwashirikishe mkasa ni tabia yake ambapo kwa usiku tunaweza kuongea hata usiku kucha mpaka nakwazika ila mchana ukimpigia simu kupokea ni bahati yako siku iyo, ikifika saa 4 usiku na kuendelea mnajiachia, ukimuuliza kwanini anasema anakuwa bize na shughuli za nyumbani (amemaliza chuo hajapata kazi bado), kuna wakati nahisi ana mahusiano mengine labda lakini nikifatilia trend ya matukio nashindwa kuelewa.

Anasisitiza kila siku kua ananipenda na anawish niwe mme wake and she even cry when i threatened her kuwa nitamuacha (sasa cjui analia ya kwenye simu ile tehe tehe).

Mchango na uzoefu wenu unahitajika
 
ha ha ha mkuu unaliwa unachapiwa yupo bussy anahudumia mwenzio.... ila shida ndiyo zinamfanya awe hivyo
 
bado upo hapo hapo tu mpaka leo? nsubiria ukija kwa mara ya pil ukija na season two yake
 
Huyo mchana anamuhudumia mwenzio kupika na kupakua anarudi home jioni jioni ndo anapata chance ya kuongea na wewe,be careful man!!By the way endelea kumchunguza utagundua ukweli.
 
Mi wangu huh mwaka wa pili nimeonana nae mara 9 tu....we kumbe miezi dah
 
Si tutajuaje pengine mpenzi wako ni popo mchana anavaa za njano usiku nyeupe
 
aisee...
fanya kama ulivyofanya kumpata....
 
na wewe mchana kuwa busy na mambo yako, usimsumbue mwenzio

Ukimchunguza sana bata humlii...
 
ha ha ha mkuu unaliwa unachapiwa yupo bussy anahudumia mwenzio.... ila shida ndiyo zinamfanya awe hivyo

Huyo mchana anamuhudumia mwenzio kupika na kupakua anarudi home jioni jioni ndo anapata chance ya kuongea na wewe,be careful man!!

Hivi nikiwauliza mmelijuaje hili mwaweza nipatia jibu linaloridhisha??
 
Maisha haya basi tu,
mwanamke akikwambia yupo busy na majukumu muelewe vyema kama ni uongo utajua tu,au ulitaka akudanganye nini?
 
Chunguza kwa umakini kabla ya kufanya maamuzi magumu.
 
Mwanaume wake ni mlinzi analinda usiku tu!Sasa sababu ya kutopokea sim zako mchana ni kwamba jamaa anakuwepo home so anashindwa kuongea, usiku akienda lindoni ndo anajiachiiiia na wewe. Hahahaaa, poleee!Chungu lakini DAWAA
 
Fanya surprise siku moja Uende mchana ujue kinacho mkeep busy!!
 
Back
Top Bottom