Huyu mwanamke simuelewi

Huyu mwanamke simuelewi

Wakuu naombeni ushauri kuna mpenzi wangu tuna muda wa miezi mitatu sasa katika mahusiano yetu, ila simuelewi nikimpigia simu anachelewa kupokea au asipokee kabisa ni kimuuliza tatizo nini anatoa sababu zisizo za msingi, mara nyingi mi ndo mpigaji sana wa simu na nikikaa kimya kuto kumpigia hanitafuti, kuna siku nilimuuliza bado ananipenda akanijibu yuko njia panda na hajielewi na muda mwingi simu yake inakuwa busy sana nikimpigia wakati wa usiku, wakuu naomba mnisaidie nifanyeje? bado namhitaji
heee...mweee! hapo penye red patamu! ukipiga simu anapochelewa kupokea au hapokei kabisa basi fahamu kuwa wakati huo huwa yuko na jamaa 6X6 na wako kazini so don't disturb...men at work! umeelewa? :bowl:
 
Wakuu huyu mwanamke nimekuwa nikimpenda sana kiasi kwamba niliamini kwamba anaweza kuwa mke wangu wa baadaye wala sikutaka kumchezeya ,nimekuwa nikimsaidie mambo mengi kiuchumi na kumpa zawadi ndogondogo na nilimwambia kabisa dhumuni la kuwa na yeye ni kuwa mke na mme wa baadaye lakini bado aeleweki kweli imeniuma sana nimeshindwa mambo gani nimfanyie anielewe.
 
nilikupenda kimapenzi solemba oh dada.umeachwa solemba kaka.jiweke pembeni.kwani unachimba dhahabu hapo.
 
Wakuu naombeni ushauri kuna mpenzi wangu tuna muda wa miezi mitatu sasa katika mahusiano yetu, ila simuelewi nikimpigia simu anachelewa kupokea au asipokee kabisa ni kimuuliza tatizo nini anatoa sababu zisizo za msingi, mara nyingi mi ndo mpigaji sana wa simu na nikikaa kimya kuto kumpigia hanitafuti, kuna siku nilimuuliza bado ananipenda akanijibu yuko njia panda na hajielewi na muda mwingi simu yake inakuwa busy sana nikimpigia wakati wa usiku, wakuu naomba mnisaidie nifanyeje? bado namhitaji

chukua chako mapema bro, dem haeleweki huyo anakuaje njia panda wakati we ndo mtima wako ulipo? kaa pembeni mapema usije kufa na mawazo bure maisha mazuri sana ukiwa na "peace of mind". Mpotezee wako wa ukweli yupo muombe Mungu akuonyeshe njia
 
Mimi naamini si kila mahusiano yanapaswa kuwa ndoa, hivyo, tafakari, chukua hatua
 
refa akipiga filimbi,ujue mpira umeisha.huyo dada either ana mtu mwengine,ila hajui achagui yupi.au anaona mahusiano yenu ni ya kuzinguana tu,hakuna jipya,kwa hiyo hajui afanye nini
 
umeshafanya diagnosis unashindajwe treatment?
 
Fikiria kabla ya kutenda.
Huenda bado anakupenda ila tatizo ni wewe au huenda kuna kitu kinamsibu ndo maana ameambua kukujibu hivyo, hebu jaribu kumuachia muda kidogo wakufikiri ili uangalie nini kinachomsumbua akili.
 
Kama haujui kusoma hata picha pia nazo huoni???

Hapo huna mpenzi!



Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom