Huyu mtoto 'anauzwa' sokoni hadi umri gani?

Ncha Kali

JF-Expert Member
Sep 19, 2019
14,510
27,003
Hakuna cha salamu!

Kumekuwa na hii kasumba ya kujibu maswali ya watoto wetu wanapodadisi kuhusu upatikanaji wa 'wadogo' zao, mtoto akihoji anataka mdogo wake ataambiwa “nitaenda kununua” nikuletee!

Naye basi anafurahia ahadi na hata mdogo wake atapopatikana basi hutamba kuwa mama yake amemnunulia, kwanza ni nini msingi wa uongo wa namna hii?

Basi turudi kwenye hoja.

Ni sahihi kuwaongopea watoto mambo ya kikubwa kwa kisingizio cha umri wao?

Kama uliwahi kuwa mtoto, huenda uliwahi kudanganywa hivi pia. Kama una kumbukumbu nzuri, uligundua ukweli [kwa njia gani] ukiwa na umri gani?

Wazazi wengi kwa sababu mbalimbali wamekuwa hawawezi kuzungumza na watoto wao kuhusu elimu ya uzazi, watoto wanakua tu na kujikuta kila mmoja anaelewa kwa namna yake.

Je, kama kuna haja ya kuzungumzia hili... upi ni umri sahihi kwa mtoto kupewa elimu hii?

Wasalaam.

Ncha Kali.
 
Africa kuna changamoto nyingi si hiyo tu kuna nyingine ikitokea baba au mama ana mototo wa nje ambaye ni ndugu yako ni umri gani unapaswa wazazi wakueleze .. Maana kibongo bongo ni wewe na akili zako ujiongeze
 
Kwani kwenye shule za msingi si kuna syllabus inafundisha yote haya?Ya nini mzazi kuumiza kichwa juu ya mambo haya kama huko shuleni kuna syllabus inafundisha haya mambo?



Kwahiyo watoto watulie hadi darasa la tano!
 
Ndiyo,ile syllabus imekuwa designed kwa usahihi kulingana na umri wa watoto.Wataalam walifanya tafiti wakagundua kuwa umri sahihi wa mtoto kuelezwa hayo mambo ni darasa la tano.

Utakuta washaanza kuliwa bila hata kujua, mara paap mimba hii hapa!
 
Mie nilikua naangalia wazungu sana kwenye TV toka mdogo kabisa, kwahiyo nilikua najua kabisa watoto huzaliwa na hutoka tumboni kwa mama.

Ila Alipozaliwa mdogo angu nilitangaza mtaa mzima mama Yangu kazaa Mzungu.
 
Kwani wewe ulifundishwa kuto.mba,? Kuna kiumbe chochote duniani kilifundishwa hilo? Ni mambo ya asili (nature). Kila kiumbe kitajua muda ukifika. Mada hii haina mashiko. Huhitaji kuwaambia watoto wametoka wapi. Muda wao utafika na watajua wenyewe. Ni suala la busara na maadili tu.
 
Mbona Mimi nisikia mdogo wangu alimwambia MWANAE Huyu mdogo wako nimemtoa Tumboni.
 
Back
Top Bottom