Huyu MC wa Mei Mosi ni timamu?

Huyu MC wa Mei Mosi ni timamu?

obwato

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2012
Posts
1,188
Reaction score
365
Nipo hapa naangalia sherehe za Mei mosi lakini nashindwa kuelewa huyu mshereheshaji ana matatizo ya kufikiri au ndio kujipendekeza kwa mkuu mpaka anaongea kauli zisizopendeza? Kwanza nilimsikia anawakemea watu kuwa "Tulieni kama mnafanyiwa tohara" nikadhani amepitiwa tu lakini amerudia tena kwa kumwambia mgeni rasmi kuwa "usiwe na wasiwasi hii mvua haitonyesha nina uwezo wa kuizuia" hapa amenishangaza sana, ina maana yeye ni Mungu au ni bingwa wa ushirikina? Sifa nyingine sio nzuri kuzitafuta kwenye halaiki kama hii.
 
Kavaa nguo za rangi gani huyo jamaa Msema Chochote!Atakua ni mbunge tarajali!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Haya ni maneno aliyoanza nayo rais Kikwete kabla ya hotuba yake ya Mei Mosi. Sijayapenda kwasababu Tanzania tunasifika ndani na nje ya nchi yetu kwa uchawi. Hapa rais kwa mtizamo wangu, alianza kusujudu uchawi kama sio wachawi.
 
Kikwete akamuumbua alipoanza kuhutubia. Mvua imekushinda
 
Mkulu kasemaje maaana hata hela ya zuku imenishinda,haja wadangaja wafanyakazi?
 
Nipo hapa naangalia sherehe za Mei mosi lakini nashindwa kuelewa huyu mshereheshaji ana matatizo ya kufikiri au ndio kujipendekeza kwa mkuu mpaka anaongea kauli zisizopendeza? Kwanza nilimsikia anawakemea watu kuwa "Tulieni kama mnafanyiwa tohara" nikadhani amepitiwa tu lakini amequdia tena kwa kumwambia mpeni rasmi kuwa "usiwe na wasiwasi hii mvua haitonyesha nina uwezo wa kuizuia" hapa amenishangaza sana, ina maana yeye ni Mungu au ni bingwa wa ushirikina? Sifa nyingine sio nzuri kuzitafuta kwenye halaiki kama hii.

Kama umemsikiliza rais amesema nini kuhusiana na hili ndo ungeelewa huyo MC alikuwa anamaanisha nini. Taifa hili kuna watu ni inseparable na uchawi pamoja na MC na hiyo imethibitishwa na maneno ya rais kabla hajaanza hotuba yake ya Mei Mosi.
 
Mkulu kasemaje maaana hata hela ya zuku imenishinda,haja wadangaja wafanyakazi?

Anasema uwanja wa ndege Songwe inaweza kutua ndege ya Obama 747 bila shida, pia anawashauri wachangamkie kilimo cha maua tuwashinde Kenya. Kima cha chini cha mishahara ameahidi kitaongezwa kwa kiasi kikubwa kidogo ila hakuta wahusika wataona ongezeko mwezi Julai.
 
Kama umemsikiliza rais amesema nini kuhusiana na hili ndo ungeelewa huyo MC alikuwa anamaanisha nini. Taifa hili kuna watu ni inseparable na uchawi pamoja na MC na hiyo imethibitishwa na maneno ya rais kabla hajaanza hotuba yake ya Mei Mosi.

Nimemuelewa kaka ndio maana nikahoji utimamu wa akili zake maana mwenye busara hawezi kujisifu kwa ushirikina hadharani.
 
Nipo hapa naangalia sherehe za Mei mosi lakini nashindwa kuelewa huyu mshereheshaji ana matatizo ya kufikiri au ndio kujipendekeza kwa mkuu mpaka anaongea kauli zisizopendeza? Kwanza nilimsikia anawakemea watu kuwa "Tulieni kama mnafanyiwa tohara" nikadhani amepitiwa tu lakini amequdia tena kwa kumwambia mpeni rasmi kuwa "usiwe na wasiwasi hii mvua haitonyesha nina uwezo wa kuizuia" hapa amenishangaza sana, ina maana yeye ni Mungu au ni bingwa wa ushirikina? Sifa nyingine sio nzuri kuzitafuta kwenye halaiki kama hii.

....Mkuu msamehe ...heri malaria ipande kichwani kuliko njaa ...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom