Huyu kocha ataishusha hii timu daraja!!

Huyu kocha ataishusha hii timu daraja!!

Freyzem

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2013
Posts
10,180
Reaction score
24,798
Mwanzoni wakati huyu kocha anapewa hii timu alishangiliwa kwa vifijo na nderemo na kuonekana kuwa huyu ndiye kocha aliyestahili kuichukua hii timu!

Alifanya usajili wa nguvu tena taratibu taratibu huku akidai kuwa anatafuta wachezaji makini wanaojua kucheza na namba zao vizuri ili kuhakikisha ubingwa unabebwa!

Mechi za mwanzoni kocha aliona kuna wachezaji wa zamani waliojulikana kama majipu walioonekana kutokucheza vizuri na namba zao, hao waliondolewa kwenye kikosi na namba zao kuchukuliwa na wachezaji wapya, wachezaji wa zamani waliobakia walihamishwa namba zao, golikipa akawa forward, washambuliaji wakawa mabeki yaani timu haieleweki maana huyu kocha hata kozi ya ukocha hakupitia na hata washauri wa timu hakubaliani nao!

Sasa timu imeanza kushiriki ligi, kila mechi kiwango cha timu kile tulichoaminishwa hakionekani!

Mashabiki wameamua kususia kuishabikia timu, wale wafadhili nao wengi hawataki kuifadhili timu.
Ilitokea hivi majuzi timu ilipatwa na mtikisiko wafadhili na mashabiki wakajitolea kuifadhili timu , lakini michango yao kocha akaelekeza isitumike kwa ajili ya walengwa!

...Huyo kocha amekuwa na lugha za kuudhi kwa mashabiki bila kujua wengi wao ndio waliopendekeza aletwe kwenye timu hatimae akapigiwa upatu na kukabidhiwa timu ili ainoe!

Hivi sasa timu inazidi kuporomoka siyo kwa kiwango, mapato, mashabiki na hata wafadhili!
......Hii timu isahau ubingwa, na wakuipandisha daraja itakuwa shughuli kweli kweli!!
 
Ikishuka, itapanda tena daraja, halafu utastaajabu yale waliofanya Leicester City.
Ila mkuu..! hii post ni ya kichochezi
 
Cc.. mzee ruksa
Kichwa cha mwendawazimu..kila kinyozi hunyoa atakavyo..
 
Mfumo anaoutumia hata haueleweli, katikati ya mechi anaweza badili mfumo zaidi ya mara 4...
 
nimekuja mbio mbio nikadhani labda yule kocha wa Timu flani pale EPL ambaye naye alikula 4G

ila saafi naona tunaanza kutumia vizuri KISWAHILI VITU KAMA Takriri,Tasfida,Tanakali sauti vinarudi kwa kasi bado barua ya Maneno kumi tu nahisi nayo muda sio mrefu itarudi
 
Ikishuka, itapanda tena daraja, halafu utastaajabu yale waliofanya Leicester City.
Ila mkuu..! hii post ni ya kichochezi
Mkuu ushachocheka? Mkichocheka huwa mna visirani kama mko bridi mkuu. Pole
 
Tatizo kocha anafanya kazi kama jeshi la mtu mmoja. Pesa za usajili alizopewa kazifungia kabatini hataki kuzitumia kununua wachezaji wa maana kakimbilia kununua usafiri kwa ajili ya wachezaji wakati timu haina matokeo mazuri ya kuiruhusu iwe kufanya safari zake ndani na nje ya nchi. Kikubwa mi naona kocha hataki ushauri toka benchi lake la ufundi ngoja tusubiri mzunguko wa pili tuone kama timu itapona kushuka daraja
 
Mwanzoni wakati huyu kocha anapewa hii timu alishangiliwa kwa vifijo na nderemo na kuonekana kuwa huyu ndiye kocha aliyestahili kuichukua hii timu!

Alifanya usajili wa nguvu tena taratibu taratibu huku akidai kuwa anatafuta wachezaji makini wanaojua kucheza na namba zao vizuri ili kuhakikisha ubingwa unabebwa!

Mechi za mwanzoni kocha aliona kuna wachezaji wa zamani waliojulikana kama majipu walioonekana kutokucheza vizuri na namba zao, hao waliondolewa kwenye kikosi na namba zao kuchukuliwa na wachezaji wapya, wachezaji wa zamani waliobakia walihamishwa namba zao, golikipa akawa forward, washambuliaji wakawa mabeki yaani timu haieleweki maana huyu kocha hata kozi ya ukocha hakupitia na hata washauri wa timu hakubaliani nao!

Sasa timu imeanza kushiriki ligi, kila mechi kiwango cha timu kile tulichoaminishwa hakionekani!

Mashabiki wameamua kususia kuishabikia timu, wale wafadhili nao wengi hawataki kuifadhili timu.
Ilitokea hivi majuzi timu ilipatwa na mtikisiko wafadhili na mashabiki wakajitolea kuifadhili timu , lakini michango yao kocha akaelekeza isitumike kwa ajili ya walengwa!

...Huyo kocha amekuwa na lugha za kuudhi kwa mashabiki bila kujua wengi wao ndio waliopendekeza aletwe kwenye timu hatimae akapigiwa upatu na kukabidhiwa timu ili ainoe!

Hivi sasa timu inazidi kuporomoka siyo kwa kiwango, mapato, mashabiki na hata wafadhili!
......Hii timu isahau ubingwa, na wakuipandisha daraja itakuwa shughuli kweli kweli!!
2020 mkataba ukiisha, ana renew na hakuna wa kumng'oa. Kaa ukijua hilo
 
Mwanzoni wakati huyu kocha anapewa hii timu alishangiliwa kwa vifijo na nderemo na kuonekana kuwa huyu ndiye kocha aliyestahili kuichukua hii timu!

Alifanya usajili wa nguvu tena taratibu taratibu huku akidai kuwa anatafuta wachezaji makini wanaojua kucheza na namba zao vizuri ili kuhakikisha ubingwa unabebwa!

Mechi za mwanzoni kocha aliona kuna wachezaji wa zamani waliojulikana kama majipu walioonekana kutokucheza vizuri na namba zao, hao waliondolewa kwenye kikosi na namba zao kuchukuliwa na wachezaji wapya, wachezaji wa zamani waliobakia walihamishwa namba zao, golikipa akawa forward, washambuliaji wakawa mabeki yaani timu haieleweki maana huyu kocha hata kozi ya ukocha hakupitia na hata washauri wa timu hakubaliani nao!

Sasa timu imeanza kushiriki ligi, kila mechi kiwango cha timu kile tulichoaminishwa hakionekani!

Mashabiki wameamua kususia kuishabikia timu, wale wafadhili nao wengi hawataki kuifadhili timu.
Ilitokea hivi majuzi timu ilipatwa na mtikisiko wafadhili na mashabiki wakajitolea kuifadhili timu , lakini michango yao kocha akaelekeza isitumike kwa ajili ya walengwa!

...Huyo kocha amekuwa na lugha za kuudhi kwa mashabiki bila kujua wengi wao ndio waliopendekeza aletwe kwenye timu hatimae akapigiwa upatu na kukabidhiwa timu ili ainoe!

Hivi sasa timu inazidi kuporomoka siyo kwa kiwango, mapato, mashabiki na hata wafadhili!
......Hii timu isahau ubingwa, na wakuipandisha daraja itakuwa shughuli kweli kweli!!
Huyu kocha wa ajabu, anafundisha mchezo asioujua hata sheria zake hazijui
 
Mfumo anaoutumia hata haueleweli, katikati ya mechi anaweza badili mfumo zaidi ya mara 4...
Kocha mumemchagua mwenyewe,
Na pengine muda au mkataba wa huyo kocha ukiisha mtachagua tena,
Cha msingi ni kumuomba tu Mungu
 
Kocha anatumia sheria za netball kufundishia mpira wa miguu, humo ndani ni ubishani tuu, kweli ninawasiwasi na hii timu kusonga mbele
 
Sio Siri Guardiola alifikiri EPL ni mchezo , hadi sasa hajielewi maana mambo yanaenda kinyume
 
kocha huyu ana hisa kubwa kwenye timu huwezi mn'goa kirahisi hivyo
 
Huyu kocha ni hasidi na ana roho mbaya kiwango cha shetani,
Kama hata hela iliochangiwa wana maafa kaimaind, kaona waarhirika watapata, si hata hilo kombe atalitafutia plan nyengine ili tusilipate
 
1484593555114.jpg
 
Naona unamzungumzia Guardiola. Alikotoka kote alikua anaongoza ligi,kwenye hii ligi mpya kashindwa kufurukuta. Timu yake ni afadhali ya jana.
 
HUYU KOCHA NIA YAKE FOOTBALL ILA ANAJIKUTA ANATUMIA SHERIA ZA GOFU BADALA YA FOOTBALK.HII TIMU KUSHINDA NGUMU SANA.
 
Back
Top Bottom