Ryzen
JF-Expert Member
- Dec 6, 2012
- 7,305
- 8,655
- Thread starter
- #61
Asantee saana!Zamani kidogo pale magomeni kulikuwa na Mpemba mmoja anafanya biashara ya kuuza vipande vya pweza mida ya jioni hivi, alipofikisha kiwango flani cha faida akaamua kufunga safari hadi Pemba na kuoa msichana mmoja toka kijijini kwao mrembo balaa. Baada ya upepo wa Dar kumkolea yule dada uzuri wake sasa ulianza kuonekana na kila mtu wenyewe wanaita natural beauty, she was very beautiful, kumbe pale pembezoni kuna kijana mmoja alimiliki taxi kadhaa alimuona na akawa anamtongoza daily, dada akaenda kumshatikia mume kuwa nikija hapa jioni kufata hela za mkate kuna jamaa ananitongoza daily, muuza pweza alimfata jamaa na akamuonya dhidi ya mke wake, jamaa anaemiliki taxi akatoa bomba akamwambia jamaa ukinizingua nakumaliza sasa hivi, muuza pweza kafunga duka kaenda pemba kufata kombora la kichawi, hadi ninavyoandika hapa jamaa mwaka wa 5 huu yupo kitandani na hospitali zote zimeisha. Sikushauri utafute kombora broo TheMason lakini ongea nae huyo kaka kwa wema na huenda akakuelewa.