Huyu Dada Simuelewi.Nisaidieni JF...

Mhubiri

Senior Member
Feb 12, 2008
180
21
Kuna mdada mmoja,siyo mzuri sana lakini ni mrefu,mrembo na msomi na ni type yangu na binafsi namuona ni wife material.Nimempenda huyu dada.Yuko single.Ni muda mrefu namtongoza lakini kila mara huwa ananikatisha tamaa,kuwa pamoja na kuwa im a nice guy lakini hatatoka na mimi na ana enjoy company yangu kama rafiki/kaka.Huwa nikimuomba kutoka nae,Hakatai hata kidogo,na huwa anajiandaa sana kwa maana ya kujipodoa na kuvalia vizuri sana as if anakwenda kukutana na mpenzi wake na si rafiki/kaka kama anavyodai kunichukulia.Na huwa ana flirt sana tu,tunapokutana au kuongea kwenye simu au sms.

Kinachonishangaza zaidi(pamoja na maneno yake kuwa hawezi kuwa mpenzi wangu)akiniona au akisikia kuwa nina mpenzi huwa ananinunia na hataki kukutana na mimi tena.Alinifanyia hivi nilipokuwa natoka na msichana mwingine.Tulikuwa hatuwasiliani wala hatukutani.Alipopata habari kuwa nimeachana na huyu msichana (mwanzoni mwa mwezi uliopita)aliniandikia message ya kunijulia hali baada ya muda mrefu.Nilipopata message yake nilifurahi sana.Nikaamua kumfukuzia tena safari hii nikiwa na imani kubwa labda kitaeleweka.Nikamuomba,akakubali kama kawaida tukatoka.Tuliongea sana usiku ule,lakini nilipomkumbushia issue yangu ya kumtaka,alinichomolea katakata,na kama kawaida yake akidai kuwa ana enjoy tu company yangu kwavile ananichukulia kama rafiki/kaka.Sikukata tamaa japo deep down nilikasirika.Nikawa naendelea kukutana nae na kuwasiliana nae mara kwa mara.

Sasa wakuu ni juzi tu jumamosi,nikaamua kutoka na demu mwingine club moja hivi.Kama zali pale club na yeye alikuwepo na nikagongana naye macho kwa macho,akiniona na huyu demu mwingine.Akanikatia jicho kunionyesha kuwa amechukia.Jumapili niliamua kumpigia,lakini hakupokea.Jana jumatatu nikamuandikia message lakini mpaka sasa hakunijibu.

Wakuu kifupi nampenda huyu demu na kama angeingia kwenye line,nilitaka nioe kabisa.Tatizo simuelewi kama ni mgumu wa kuelewa somo,hanipendi,ni sitaki nataka,ananitega au vipi??
Sasa wakuu nisaidieni mawazo,nimfanyeje huyu manzi?
Nitaheshimu mawazo yenu wakuu,isipokuwa matusi na dhihaka zisizokuwa na maana.
 
Inaonekana kweli unampenda,ila sasa na wewe unazidi kuharibu anapokuona na vidosho mara kwa mara anadhani wewe ni player

Hebu Muombe Mungu
Pili keep distance kidogo,msipoonana kwa muda hiyo hali inaweza kubadilika
pia,je umemchunguza na kuwa na uhakika hana mtu?
 
Mmh let me think~that gal is a lesbian, run for your life broda!.:wink2:
 
Kwa mtu kama huyo, usitake kumonja kwanza, naona kama unampango wa kumfanya demu wa "hit and run" jaribu kujadili naye kuhusu maisha siyo kwenda room to kugongana
 
hawa viumbe ni wa ajabu hata ukiishi nao miaka mia hutawaelewa, wachukulie kama walivyo.....
 
chapa kazi mpaka kieleweke mkuu.. pengine yalishamkuta bado ana makovu
 
No offense, but Could it be maybe you are her Plan B :wink2:???

She is holding out, hoping to meet and/or get with Mr plan A, lakini mean while is hanging onto you just in case Plan A doesnt materialize!?
 
Inaonekana kweli unampenda,ila sasa na wewe unazidi kuharibu anapokuona na vidosho mara kwa mara anadhani wewe ni player

Hebu Muombe Mungu
Pili keep distance kidogo,msipoonana kwa muda hiyo hali inaweza kubadilika
pia,je umemchunguza na kuwa na uhakika hana mtu?

Mkuu siwezi kujizuia kutoka na wengine.Namtongoza huyu demu karibu miaka miwili sasa.Kipindi kirefu hiki kwa mwanaume kubaki mpweke.Sijamchunguza saana kuwa hana mtu.Naamini hana mtu kwavile yuko so available ninapomuhitaji.Ingekuwa ni two timer angekuwa ananipiga kalenda za mara kwa mara.
 
No offense, but Could it be maybe you are her Plan B :wink2:???

She is holding out, hoping to meet and/or get with Mr plan A, lakini mean while is hanging onto you just in case Plan A doesnt materialize!?

Nemo;if that is the reason,why then she becomes so jealousy and full of hate when she sees me with another woman?
 
Huyo tayari ni wa kwako komaa nae mpaka kieleweke.

Nimekuwa mvumilivu sana lakini sasa naelekea kuchoka,nahitaji mbinu mpya!!

Kwa mtu kama huyo, usitake kumonja kwanza, naona kama unampango wa kumfanya demu wa "hit and run" jaribu kujadili naye kuhusu maisha siyo kwenda room to kugongana

Mkuu nimemuonyesha dalili zote kuwa namtaka awe zaidi ya gf na hata tulivyokutana baada ya kimya cha muda mrefu mada kuu ilikuwa ndiyo hiyo,lakini wapi mkuu haeleweki.Na anachonichosha zaidi ni ku 'act' kwake kama mpenzi wangu wakati kiuhalisia hatuko pamoja kama couple.

hawa viumbe ni wa ajabu hata ukiishi nao miaka mia hutawaelewa, wachukulie kama walivyo.....

chapa kazi mpaka kieleweke mkuu.. pengine yalishamkuta bado ana makovu

Umesema kitu ambacho sijawahi kufikiria.Sijawahi kumuulizia kwa undani kuhusu mahusiano yake ya mwanzo,nikidhani kwamba si muhimu na naweza kuharibu na mwenyewe hajawahi kunisimulia kwa undani.Labda nianze?
 
So, nafikiri jambo zuri ukimtafuta ata best yako wa karibu akae naye amweleze unavyojifili au rafiki yake,
 
mh pole sana bro kwa kuandika hii thread ukiwa na hisia kali moyoni mwako,nimesoma huu ujumbe kwa makini sana,huyu manzi umesema una miaka miwili ukiwa naye,labda nikuulize kijiswali,hujawahi kumuomba chezo? na je kama ulimuomba alisemaje?
kwa maoni yangu mimi kama hana mwitikio kwako,hisia,basi wewe una maamuzi yako.hebu mchunguze tena kwa mara ya mwisho kama unaona haelewi somo na wewe umeshampa ukweli basi kula kona hamna haja ya kupoteza muda wako bwana,tafuta mwingine ambaye atakupenda kwa dhati,haya mapenzi ukicheza unaweza kuwehuka bure na ukashindwa kutekeleza majukumau yako ya kila siku bro.
ni hayo tu:rain::rain:
 
No offense, but Could it be maybe you are her Plan B :wink2:???

She is holding out, hoping to meet and/or get with Mr plan A, lakini mean while is hanging onto you just in case Plan A doesnt materialize!?


have the same thinking......inawezekana jamaa anafanywa plan B aisee

lakini pia kwa nini Mhubiri usimhubirie kwamba unataka kumwoa kabisa na sio kumwonja tu?
 
Haiwezekani akuzungushe kihvyo! Huyo atakuwa na tatizo mchunguze ki intelgensia, asijekuwa huko chni kuna kasoro au ana zote 2 (ke na me)
 
Nemo;if that is the reason,why then she becomes so jealousy and full of hate when she sees me with another woman?

She is jelous because, "Who is to say , that wewe and your new squeeze wont end up being forever?" U having someone else means you are definately no longer available. Kaput fall back option gone! So now not only does she lack Plan A, but Plan B is gone as well.

I, personally most of guys I have had in a situation similar to yours......ni wale that I can almost date if only they had this or that, or I could change this or that behaviour
 
how are you nemo.nimekupata:usa2:



She is jelous because, "Who is to say , that wewe and your new squeeze wont end up being forever?" U having someone else means you are definately no longer available. Kaput fall back option gone! So now not only does she lack Plan A, but Plan B is gone as well.

I, personally most of guys I have had in a situation similar to yours......ni wale that I can almost date if only they had this or that, or I could change this or that behaviour
 
Back
Top Bottom