Mhubiri
Senior Member
- Feb 12, 2008
- 180
- 21
Kuna mdada mmoja,siyo mzuri sana lakini ni mrefu,mrembo na msomi na ni type yangu na binafsi namuona ni wife material.Nimempenda huyu dada.Yuko single.Ni muda mrefu namtongoza lakini kila mara huwa ananikatisha tamaa,kuwa pamoja na kuwa im a nice guy lakini hatatoka na mimi na ana enjoy company yangu kama rafiki/kaka.Huwa nikimuomba kutoka nae,Hakatai hata kidogo,na huwa anajiandaa sana kwa maana ya kujipodoa na kuvalia vizuri sana as if anakwenda kukutana na mpenzi wake na si rafiki/kaka kama anavyodai kunichukulia.Na huwa ana flirt sana tu,tunapokutana au kuongea kwenye simu au sms.
Kinachonishangaza zaidi(pamoja na maneno yake kuwa hawezi kuwa mpenzi wangu)akiniona au akisikia kuwa nina mpenzi huwa ananinunia na hataki kukutana na mimi tena.Alinifanyia hivi nilipokuwa natoka na msichana mwingine.Tulikuwa hatuwasiliani wala hatukutani.Alipopata habari kuwa nimeachana na huyu msichana (mwanzoni mwa mwezi uliopita)aliniandikia message ya kunijulia hali baada ya muda mrefu.Nilipopata message yake nilifurahi sana.Nikaamua kumfukuzia tena safari hii nikiwa na imani kubwa labda kitaeleweka.Nikamuomba,akakubali kama kawaida tukatoka.Tuliongea sana usiku ule,lakini nilipomkumbushia issue yangu ya kumtaka,alinichomolea katakata,na kama kawaida yake akidai kuwa ana enjoy tu company yangu kwavile ananichukulia kama rafiki/kaka.Sikukata tamaa japo deep down nilikasirika.Nikawa naendelea kukutana nae na kuwasiliana nae mara kwa mara.
Sasa wakuu ni juzi tu jumamosi,nikaamua kutoka na demu mwingine club moja hivi.Kama zali pale club na yeye alikuwepo na nikagongana naye macho kwa macho,akiniona na huyu demu mwingine.Akanikatia jicho kunionyesha kuwa amechukia.Jumapili niliamua kumpigia,lakini hakupokea.Jana jumatatu nikamuandikia message lakini mpaka sasa hakunijibu.
Wakuu kifupi nampenda huyu demu na kama angeingia kwenye line,nilitaka nioe kabisa.Tatizo simuelewi kama ni mgumu wa kuelewa somo,hanipendi,ni sitaki nataka,ananitega au vipi??
Sasa wakuu nisaidieni mawazo,nimfanyeje huyu manzi?
Nitaheshimu mawazo yenu wakuu,isipokuwa matusi na dhihaka zisizokuwa na maana.
Kinachonishangaza zaidi(pamoja na maneno yake kuwa hawezi kuwa mpenzi wangu)akiniona au akisikia kuwa nina mpenzi huwa ananinunia na hataki kukutana na mimi tena.Alinifanyia hivi nilipokuwa natoka na msichana mwingine.Tulikuwa hatuwasiliani wala hatukutani.Alipopata habari kuwa nimeachana na huyu msichana (mwanzoni mwa mwezi uliopita)aliniandikia message ya kunijulia hali baada ya muda mrefu.Nilipopata message yake nilifurahi sana.Nikaamua kumfukuzia tena safari hii nikiwa na imani kubwa labda kitaeleweka.Nikamuomba,akakubali kama kawaida tukatoka.Tuliongea sana usiku ule,lakini nilipomkumbushia issue yangu ya kumtaka,alinichomolea katakata,na kama kawaida yake akidai kuwa ana enjoy tu company yangu kwavile ananichukulia kama rafiki/kaka.Sikukata tamaa japo deep down nilikasirika.Nikawa naendelea kukutana nae na kuwasiliana nae mara kwa mara.
Sasa wakuu ni juzi tu jumamosi,nikaamua kutoka na demu mwingine club moja hivi.Kama zali pale club na yeye alikuwepo na nikagongana naye macho kwa macho,akiniona na huyu demu mwingine.Akanikatia jicho kunionyesha kuwa amechukia.Jumapili niliamua kumpigia,lakini hakupokea.Jana jumatatu nikamuandikia message lakini mpaka sasa hakunijibu.
Wakuu kifupi nampenda huyu demu na kama angeingia kwenye line,nilitaka nioe kabisa.Tatizo simuelewi kama ni mgumu wa kuelewa somo,hanipendi,ni sitaki nataka,ananitega au vipi??
Sasa wakuu nisaidieni mawazo,nimfanyeje huyu manzi?
Nitaheshimu mawazo yenu wakuu,isipokuwa matusi na dhihaka zisizokuwa na maana.