Sifi Leo
Platinum Member
- Mar 30, 2012
- 5,937
- 10,815
Ninaomba mwenye cv ya Omar Kishera maana namwona sana mitandaoni hasa Istgaram akiunguruma na vipindi mbalimbali vya elimu kwa UMMA na kwa Taasisi binafsi.
Je, ni miongoni mwa vigogo waliowahi itumikia Tanzania wakiwa na elimu nzuri ila walifubazwa na mifumo ya nchi hii?
Je, akili zake zimerudi baada ya kutoka serikalini?
Sasa amekuja na simulizi dhidi ya Hayati Membe na yeye zinasimua kule Istagram je ni nani mwamba huyu katika diplomasia za Tanzania?
Kwa umahiri anaoonesha akiwa na sigida kwenye paji la uso seems ni waliochezewa na mfumo wetu mwishowe yupo nje ya system akitema madini
Je, ni nani mtu huyu?