Kitambi toroli
New Member
- Mar 29, 2013
- 2
- 5
Siku za karibu Meya wa Moshi Japhary Michael Chadema ameonekana akipenda zaidi kutumia usafiri wa bodaboda katika majukumu yake ya hapa na pale,hata baada ya kumalizika kwa baadhi ya mikutano ameonekana akipanda pikipiki maarufu kama bodaboda ili kuweza kusalimiana na wananchi wake.
Hofu yangu ni kwamba Meya anatakiwa kuwa makini sana kwani CCM wanaweza kutumia nafasi hiyo ya kutumia bodaboda kummaliza kwani usafiri wa pikipiki ni hatari na rahisi kwa mtu anayepewa jukumu la kummaliza mtu kulitekeleza kwa urahisi hususani ni siasa zetu za tanzania za uadui.
Ila katika hatua nyingine ni fursa ya yeye kujua changamoto mbalimbali kwa wananchi wake kwani anaweza kukutana na hata kushuhudia changamoto mbalimbali zilizopo kwenye Manispaa yake,kuliko kupanda kwenye gari muda wote na kufunga vioo.