Tindo
Platinum Member
- Sep 28, 2011
- 69,593
- 123,090
Mkuu umeongea maneno ya msingi sana na sehemu kubwa nakuunga mkono, hususan paleuliposema kuwa Mambo kibao ya kishenzi, kinyama na kikatili yamefanyika nchi hii lakini hawa wazee wetu hawakusimama kidete kukemea.
Hata hivyo mtu huwa hajachelewa kufanya the right thing, na ni makosa kutofanya kitu sahihi katika muda fulani eti kwa sababu zamani ulikuwa unafanya mabaya.
Lakini pia kila kitu huja huja kwa sababu maalum, huenda hili la wao kuanza kuguswa imekuwa ni awakening call kuwa sasa Chatu waliyemlea ameanza kutafuna wanafamilia adhibitiwe sasa!.
kwa hiyo pamoja na wazee wetu kuzingua hapo mwanzoni, lakini walichokifanya wakati huu ni kitendo sahihi, cha kijasiri na wamesimama kwa niaba ya wanaCCM wote wanaotaka SIASA SAFI na UONGOZI BORA
Tatizo langu nashindwa kuwaunga mkono hawa wazee, ukiacha kwamba wamegusa eneo ambalo sisi wapinzani tumelipigia kelele toka awamu hi ingine madaraka, lakini kiukweli malalamiko yao sio ya kukomeshwa siasa chafu nchini au utawala wa mabavu, bali ni kulinda heshima zao. Sasa mtu anayetetea heshima yake unawezaje kusema ana faida kwa wote?
Kwa taarifa yako hao wazee wanafiki wakihakikishiwa kufichiwa mambo yao, hata wapinzani wachinjwe hapo uwanja wa Taifa hawataongea lolote, sana sana siku hiyo ya mauaji wataenda kutembelea mradi wa SGR. Tuwe makini kutetea mashetani wanapogombana na maibilisi.