Hukumu ya kunyongwa kwa Tundu Lissu itakuwa ni doa kubwa kwa vyombo vya usalama

Hukumu ya kunyongwa kwa Tundu Lissu itakuwa ni doa kubwa kwa vyombo vya usalama

DaudiAiko

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2012
Posts
409
Reaction score
343
Wanabodi,

Naamini kwamba msimamo wa mahakama kuhusu kesi ya Tundu Lissu ndio utakao tufahamisha kama kweli hana hatia.Ushahidi wa kutosha kutoka upande wa serikali ndio unaoweza kumshawishi hakimu kutoa adhabu ya kifo kwenye kesi hii ya uhaini.

Mwanasheria yeyote mwenye nafasi ya kumtetea mteja wake mara nyingi hufahamu uwezekano wa kushindwa au kushinda kesi na uwezekano wa kupunguza adhabu inayoweza kutolewa na mahakama kwa mteja wake. Tofauti na kesi zingine ambazo zingechukua muda mrefu kwa mahakama kusikiliza ushahidi na kutoa tathmini kutokana na ushahidi, ushahidi dhidi ya Tundu Lissu uko wazi.

Soma Pia: Tundu Lissu ashtakiwa kwa Uhaini, arudishwa rumande, kesi yake kusikilizwa Aprili 24, 2025

Kuna video za Lissu na hotuba kadhaa zilizo kwenye mitandao ya jamii zinazo mnukuu Tundu Lissu akiahidi kuzuia uchaguzi kwa kuhamasisha fujo. Kama video hizi zitaweza kutumiwa kama ushahidi, basi utetezi utahitaji hoja nzito sana kupinga mashtaka haya. Wafuasi wa CHADEMA waseme kwamba adhabu ya kunyongwa haiendani na kosa la “Kupanga uhaini” na sio kwamba kesi ni ya kubambikiwa

Polisi na wanasheria wa serikali walikamilisha hatua ya kumfikisha Tundu Lissu mahakamani. Hatua zitakazofuata zinaweza kuwatia hofu na kuwafanya kufikiria kama adhabu atayopata mtuhumiwa inaendana na kosa lake. Kama wana mpango wa kumuachia Lissu, basi nyakati za kufuta mashtaka ni sasa kabla kesi haijasikilizwa sana. Kama kweli Tundu Lissu atanyongwa kwasababu ya alicho kisema kwenye hotuba, hata kama alichochea uhaini, basi itakuwa kitendo ambacho milele kitakuwa doa kwenye vyombo vyetu vya usalama. Vilevile matukio kama haya yanatakiwa yatafsiriwe na vyombo vya usalama kama hitilafu kwenye kanuni ya uendeshaji wa nchi.

Mabadiliko kwenye sheria zetu baada ya utafiti wa kina kufanywa yanaweza kutoa tafsiri ya kutosha kuhusu uchochezi, uanaharakati, uhaini, na kadhalika.
 
Wanabodi,

Naamini kwamba msimamo wa mahakama kuhusu kesi ya Tundu Lissu ndio utakao tufahamisha kama kweli hana hatia.Ushahidi wa kutosha kutoka upande wa serikali ndio unaoweza kumshawishi hakimu kutoa adhabu ya kifo kwenye kesi hii ya uhaini.

Mwanasheria yeyote mwenye nafasi ya kumtetea mteja wake mara nyingi hufahamu uwezekano wa kushindwa au kushinda kesi na uwezekano wa kupunguza adhabu inayoweza kutolewa na mahakama kwa mteja wake. Tofauti na kesi zingine ambazo zingechukua muda mrefu kwa mahakama kusikiliza ushahidi na kutoa tathmini kutokana na ushahidi, ushahidi dhidi ya Tundu Lissu uko wazi.

Soma Pia: Tundu Lissu ashtakiwa kwa Uhaini, arudishwa rumande, kesi yake kusikilizwa Aprili 24, 2025

Kuna video za Lissu na hotuba kadhaa zilizo kwenye mitandao ya jamii zinazo mnukuu Tundu Lissu akiahidi kuzuia uchaguzi kwa kuhamasisha fujo. Kama video hizi zitaweza kutumiwa kama ushahidi, basi utetezi utahitaji hoja nzito sana kupinga mashtaka haya. Wafuasi wa CHADEMA waseme kwamba adhabu ya kunyongwa haiendani na kosa la “Kupanga uhaini” na sio kwamba kesi ni ya kubambikiwa

Polisi na wanasheria wa serikali walikamilisha hatua ya kumfikisha Tundu Lissu mahakamani. Hatua zitakazofuata zinaweza kuwatia hofu na kuwafanya kufikiria kama adhabu atayopata mtuhumiwa inaendana na kosa lake. Kama wana mpango wa kumuachia Lissu, basi nyakati za kufuta mashtaka ni sasa kabla kesi haijasikilizwa sana. Kama kweli Tundu Lissu atanyongwa kwasababu ya alicho kisema kwenye hotuba, hata kama alichochea uhaini, basi itakuwa kitendo ambacho milele kitakuwa doa kwenye vyombo vyetu vya usalama. Vilevile matukio kama haya yanatakiwa yatafsiriwe na vyombo vya usalama kama hitilafu kwenye kanuni ya uendeshaji wa nchi.

Mabadiliko kwenye sheria zetu baada ya utafiti wa kina kufanywa yanaweza kutoa tafsiri ya kutosha kuhusu uchochezi, uanaharakati, uhaini, na kadhalika.
LISSU ANATAKIWA KUGOMA KUJITETEA ..WAACHE MAHAKAMA KUHUKUMU KWA KUANGALIA UPANDE MMOJA
 
Wanabodi,

Naamini kwamba msimamo wa mahakama kuhusu kesi ya Tundu Lissu ndio utakao tufahamisha kama kweli hana hatia.Ushahidi wa kutosha kutoka upande wa serikali ndio unaoweza kumshawishi hakimu kutoa adhabu ya kifo kwenye kesi hii ya uhaini.

Mwanasheria yeyote mwenye nafasi ya kumtetea mteja wake mara nyingi hufahamu uwezekano wa kushindwa au kushinda kesi na uwezekano wa kupunguza adhabu inayoweza kutolewa na mahakama kwa mteja wake. Tofauti na kesi zingine ambazo zingechukua muda mrefu kwa mahakama kusikiliza ushahidi na kutoa tathmini kutokana na ushahidi, ushahidi dhidi ya Tundu Lissu uko wazi.

Soma Pia: Tundu Lissu ashtakiwa kwa Uhaini, arudishwa rumande, kesi yake kusikilizwa Aprili 24, 2025

Kuna video za Lissu na hotuba kadhaa zilizo kwenye mitandao ya jamii zinazo mnukuu Tundu Lissu akiahidi kuzuia uchaguzi kwa kuhamasisha fujo. Kama video hizi zitaweza kutumiwa kama ushahidi, basi utetezi utahitaji hoja nzito sana kupinga mashtaka haya. Wafuasi wa CHADEMA waseme kwamba adhabu ya kunyongwa haiendani na kosa la “Kupanga uhaini” na sio kwamba kesi ni ya kubambikiwa

Polisi na wanasheria wa serikali walikamilisha hatua ya kumfikisha Tundu Lissu mahakamani. Hatua zitakazofuata zinaweza kuwatia hofu na kuwafanya kufikiria kama adhabu atayopata mtuhumiwa inaendana na kosa lake. Kama wana mpango wa kumuachia Lissu, basi nyakati za kufuta mashtaka ni sasa kabla kesi haijasikilizwa sana. Kama kweli Tundu Lissu atanyongwa kwasababu ya alicho kisema kwenye hotuba, hata kama alichochea uhaini, basi itakuwa kitendo ambacho milele kitakuwa doa kwenye vyombo vyetu vya usalama. Vilevile matukio kama haya yanatakiwa yatafsiriwe na vyombo vya usalama kama hitilafu kwenye kanuni ya uendeshaji wa nchi.

Mabadiliko kwenye sheria zetu baada ya utafiti wa kina kufanywa yanaweza kutoa tafsiri ya kutosha kuhusu uchochezi, uanaharakati, uhaini, na kadhalika.

..hakuna kesi hata moja ya uhaini hapa Tz ambayo ilihusisha mtuhumiwa mmoja tu.

..pia kesi zote za uhaini hapa Tz zilikuwa na wanajeshi Jwtz walioshirikishwa katika njama za uhaini / kupindua.

..kesi zote za uhaini hapa Tz watuhumiwa walipanga kuiondoa serikali, na walikula njama kumuua Raisi.

..ukifuatilia historia ya kesi za uhaini utaona hiki wanachomtuhumu Lissu hakifanani na uhaini.
 
Lissu anafanyiwa deconstruction tu arudi kwenye mstari na kwenye akili. Hawezi kuishi na kuropoka kama vile nchi hii ni ya babu yake. Kurejesha amani ni kazi ngumu kuliko kuilinda
 
Wanabodi,

Naamini kwamba msimamo wa mahakama kuhusu kesi ya Tundu Lissu ndio utakao tufahamisha kama kweli hana hatia.Ushahidi wa kutosha kutoka upande wa serikali ndio unaoweza kumshawishi hakimu kutoa adhabu ya kifo kwenye kesi hii ya uhaini.

Mwanasheria yeyote mwenye nafasi ya kumtetea mteja wake mara nyingi hufahamu uwezekano wa kushindwa au kushinda kesi na uwezekano wa kupunguza adhabu inayoweza kutolewa na mahakama kwa mteja wake. Tofauti na kesi zingine ambazo zingechukua muda mrefu kwa mahakama kusikiliza ushahidi na kutoa tathmini kutokana na ushahidi, ushahidi dhidi ya Tundu Lissu uko wazi.

Soma Pia: Tundu Lissu ashtakiwa kwa Uhaini, arudishwa rumande, kesi yake kusikilizwa Aprili 24, 2025

Kuna video za Lissu na hotuba kadhaa zilizo kwenye mitandao ya jamii zinazo mnukuu Tundu Lissu akiahidi kuzuia uchaguzi kwa kuhamasisha fujo. Kama video hizi zitaweza kutumiwa kama ushahidi, basi utetezi utahitaji hoja nzito sana kupinga mashtaka haya. Wafuasi wa CHADEMA waseme kwamba adhabu ya kunyongwa haiendani na kosa la “Kupanga uhaini” na sio kwamba kesi ni ya kubambikiwa

Polisi na wanasheria wa serikali walikamilisha hatua ya kumfikisha Tundu Lissu mahakamani. Hatua zitakazofuata zinaweza kuwatia hofu na kuwafanya kufikiria kama adhabu atayopata mtuhumiwa inaendana na kosa lake. Kama wana mpango wa kumuachia Lissu, basi nyakati za kufuta mashtaka ni sasa kabla kesi haijasikilizwa sana. Kama kweli Tundu Lissu atanyongwa kwasababu ya alicho kisema kwenye hotuba, hata kama alichochea uhaini, basi itakuwa kitendo ambacho milele kitakuwa doa kwenye vyombo vyetu vya usalama. Vilevile matukio kama haya yanatakiwa yatafsiriwe na vyombo vya usalama kama hitilafu kwenye kanuni ya uendeshaji wa nchi.

Mabadiliko kwenye sheria zetu baada ya utafiti wa kina kufanywa yanaweza kutoa tafsiri ya kutosha kuhusu uchochezi, uanaharakati, uhaini, na kadhalika.
Wakimnyonga Lissu basi jua kinachofata watakuta watu wako Barabarani bila kuambiwa na mtu 😂
 
Ni ngumu kum denconstruct mtu kama Lissu labda mumuue.

..Ni rahisi ku-reform tume ya uchaguzi kuliko kupiga watu na kuwahangaisha na makesi ya kibambikiza.

..Na Lissu yeye " dini " yake ni HAKI sasa kumfunga kwa kudai haki kunam-deconstruct vipi?
 
Vipi kama kuna ushahidi beyond videos?
Vipi kuhusu miamala ya kifedha kutoka ughaibuni?
Tusipende kukurupuka kuna sheria ambazo ni sehemu ya mchakato wa demokrasia
Kupewa pesa toka nje ndiyo utaipindua vipi serikali wewe pekee yako?
Hawa CCM wamechanganyikiwa tu baadanya kuona NRNE watz wana anza ielewa
 
Hukumu ni kunyongwa hadi kufa ,wajiridhishe kwamba ameishafariki na ni maiti.
Kosa lipo au halipo kutokana na clip hata asie wahi kuwa hakimu atatoa adhabu ya kunyongwa hadi kufa.
Lakufanya Chadema mfanye juu chini kama kweli mnampenda Lisu basi mwambieni aombe msamaha ,ila kama mnafurahia ahukumiwe ili mrudi kwenye nafasi zenu ,maana Lisu aliwasakama viongozi wengi wa chadema na kuwashinda kwa hoja ,na kama walimtosa kwa kumshawishi ya kusema ,kwa kweli walikuwa na nia mbaya sana.

Ule mfarakano wa kugombea uenyekiti wa Chadema ulikuwa mtihani wa chama, kama ulivyotokea na unavyotokea kwa CUF ,hapa kuna ukakasi kuwa Chadema badala ya kujitenga waliamua kumtosa mwenzao wakijifanya washauri
 
Hawawezi kumnyonga hawawezi kumfunga asilani utaikumbuka hii post yangu.
Ni sahihi kabisa hakuna Kesi yoyote kwa Lisu kwa alichotamka sababu zipo wazi,yeye ni muhamasishaji tu mageuzi na ni mwenyekiti wa Chama halali cha siasa. Ilipaswa kwanza swala lake lianzie kwa msajili wa vyamabyeye ndiye mwenye jukumu la kudhibiti na kuadhibu viongozi na vyama vya upinzani lakini msajili kasema wazi kauli za CDM ni kauli za kisiasa hazinavmadhara yoyote wao wanatoa wapi kosa hata la uchochezi sembuse la uhaini. Ingekuwa Li,,isu ametoka kusiko julikana kweli lakini vhama chake kipo na kinafanya kazi kama kawaida na hayo anayoshitakiwa nayo Lisu kuusu kuhamasisha maandamano kuzuia uchaguzi bado yanatamkwa wizi wa kura bado yanaongelewa majukwaani sasa watanyonga wangapi.Hii siyo kesi kws sababu kamma ni hivyo Heche naye anapaswa afunguliwe kesi ya uhaini na ya uchochszi ,Lema pia anapaswa afunguliwe kesi ya uhaini na uchochezi kamati kuu yote iliyopita wanapaswa kufunguliws kesi ya uhaini na uchochezi ,sasa kwNini wabague.Anaye shirikiana na mwizi na yeye ni mwizi ,wanaoshirikiana na Lisu nao ni wahaini.
 
Back
Top Bottom