Huduma ya NBC Mobile Banking

Huduma ya NBC Mobile Banking

jerrytz

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2012
Posts
5,980
Reaction score
4,284
Wadau,

Mimi ni mteja wa NBC, Jumatatu tarehe 02 June 2014 nilitembelea tawi la NBC Zanzibar kwa ajili ya kupata huduma za kibenki.

Baada ya kumaliza kilichonipeleka hapo benki nikaona ni vyema pia nijiunge na huduma ya Mobile Banking yote ni katika kurahisisha maisha.

Nikaelekezwa na kujaza fomu pamoja na kopi yangu ya kitambulisho kisha nikaambiwa nitapokea message ya kuunganishwa na huduma hiyo.

Mpaka sasa sijapokea message yoyote hivyo nikaona ni vyema nipite Benki ili kujua kinachoendelea. Majibu niliyopata ni kuwa bado sijaunganishwa kwa kuwa wanaounganisha huduma ya NBC mobile banking ni makao makuu Dar.

Tatizo ni kwamba hata huyu aliyechukua fomu yangu hajui ni lini nitaunganishwa na hiyo huduma maana anakisia tu kuwa labda nicheki leo mchana.

Niliwahi kuomba huduma kama hii kwa benki nyingine na niliunganishwa ndani ya dakika tano.

Najiuliza huu ni uzembe wa tawi la benki kwa maana ya NBC Zanzibar? Au ni uzembe wa huyu anayenihudumia au ni mifumo mibovu ya NBC Makao makuu?

Inakuwaje huduma ndogo kama hii inachukua zaidi ya siku nne kuunganishwa? Au ni kutaka tuendelee kupanga foleni benki kwa huduma ambazo zisingetupasa kwenda benki?

Kwa wanaotumia huduma hii ya NBC Mobile banking mliunganishwa baada ya siku ngapi?

Ushauri tu, Banki zetu zijifunze kutoa huduma bora na sio kubabaisha katika ulimwengu ambao makampuni mengi ya kifedha yanatoa customer care nzuri na ya kuridhisha.
 
Pole sana mdau, mimi tokea nijaze hizo form za maombi ya hiyo huduma ya NBC-Mobile banking ni zaidi ya minne(4) bila bila mpaka sasa, kwa kweli natumia tu hii bank kwa kuwa mshahara wangu unapitia kwa hii bank, otherwise ningekuwa nimewapiga chini siku nyingi sana, bado huduma zao nyingi ni local.

Kwa kifupi nimeshakata tamaa!
 
NBC walikula mbegu siku nyingi..., ndo maana ukiwauliza mbona mbegu hazioti wanakujibu:- subiri subiri 'leo mchana' huenda zitaota..
 
Pole sana mdau, mimi tokea nijaze hizo form za maombi ya hiyo huduma ya NBC-Mobile banking ni zaidi ya minne(4) bila bila mpaka sasa, kwa kweli natumia tu hii bank kwa kuwa mshahara wangu unapitia kwa hii bank, otherwise ningekuwa nimewapiga chini siku nyingi sana, bado huduma zao nyingi ni local.

Kwa kifupi nimeshakata tamaa!
Labda kama una mkopo nao ila mshahara unaweza hamishia benki yoyote
 
Me nna mpango jmosi nikasombe pesa zootee..ya ajabu sana hiI bank.ngoja tu zihamie nmb pamoja na folenI zote
 
mbona mimi niliunganishwa na hii huduma mara moja hata haikuchukua robo saa? ulijaza fomu zako fresh mkuu?
 
Me nna mpango jmosi nikasombe pesa zootee..ya ajabu sana hiI bank.ngoja tu zihamie nmb pamoja na folenI zote


Nmb nao ni kenge ndani ya msafara wa mamba mie nilijaza fomu Magomeni branch kuomba kubadili namba ya nmb mobile tangu 7.5.2014 hadi sasa hakuna kitu
 
mbona mimi niliunganishwa na hii huduma mara moja hata haikuchukua robo saa? ulijaza fomu zako fresh mkuu?

Mkuu, fomu nilijaza vizuri kabisa.....Jina, Namba ya akaunti, Signature..

Nina wasiwasi na huyu jamaa aliyepewa kitengo maana haeleweki kabisa. Kama tatizo halipo NBC basi waangalie watumishi wao
 
Nmb nao ni kenge ndani ya msafara wa mamba mie nilijaza fomu Magomeni branch kuomba kubadili namba ya nmb mobile tangu 7.5.2014 hadi sasa hakuna kitu

Yaani huduma ya hizi benki ni majanga kabisa. Watu wamekaa kazi ni kusikiliza muziki na kuangalia video youtube
 
Pole sana mdau, mimi tokea nijaze hizo form za maombi ya hiyo huduma ya NBC-Mobile banking ni zaidi ya minne(4) bila bila mpaka sasa, kwa kweli natumia tu hii bank kwa kuwa mshahara wangu unapitia kwa hii bank, otherwise ningekuwa nimewapiga chini siku nyingi sana, bado huduma zao nyingi ni local.

Kwa kifupi nimeshakata tamaa!

Wasiponiunganisha mpaka leo saa kumi, kesho naenda mojamoja kwa branch manager
 
mi ilinichukua siku kama 4 nkapokea meseji ya kuwa nimeunganishwa.Usajiri niliufanyia huku dar,labda form wamezituma kwa njia posta azijawafikia makao makuu wavumilie mkuu
 
Hivi hii huduma nbc mpk ujaze fomu..mbona nmb unajiunga binafsi pale kwa atms
 
Nmb nao ni kenge ndani ya msafara wa mamba mie nilijaza fomu Magomeni branch kuomba kubadili namba ya nmb mobile tangu 7.5.2014 hadi sasa hakuna kitu

Tatizo sitaki tena process ya kufungua account zingine
 
Hivi hii huduma nbc mpk ujaze fomu..mbona nmb unajiunga binafsi pale kwa atms

Yap, kuna fomu unajaza jina lako , namba ya akaunti na namba ya simu pia ina sehemu 4 za ku-tick huduma unazotaka.
.........................................................................................
You need to have an existing account with NBC first. You can register for NBC Mobile Banking Services using the following quick steps:
Visit any NBC Branch
Fill in the Mobile Banking form
Sign the form
Submit the form to the Customer Service personnel.
Your account will be created and you will receive a random generated Mobile Banking PIN
 
Me nna mpango jmosi nikasombe pesa zootee..ya ajabu sana hiI bank.ngoja tu zihamie nmb pamoja na folenI zote
tofali wee kiboko unakimbia nini na unakimbia wapi
 
Last edited by a moderator:
At last nimepokea message.Bila shaka walipita huku na kuona malalamiko.Asanteni NBC. Boresheni huduma zaidi
 
Duh, kuna benki naziogopa balaa

Nahisi nikiweka mijihela yangu itayeyuka bila maelezo
 
Back
Top Bottom