Huduma ya NBC Mobile Banking

Huduma ya NBC Mobile Banking

Pole sana mdau, mimi tokea nijaze hizo form za maombi ya hiyo huduma ya NBC-Mobile banking ni zaidi ya minne(4) bila bila mpaka sasa, kwa kweli natumia tu hii bank kwa kuwa mshahara wangu unapitia kwa hii bank, otherwise ningekuwa nimewapiga chini siku nyingi sana, bado huduma zao nyingi ni local.

Kwa kifupi nimeshakata tamaa!

Mimi sijajibiwa mwaka mmoja na karibia miezi kumi sasa. Nilijazia Muhimbili.
 
Mimi sijajibiwa mwaka mmoja na karibia miezi kumi sasa. Nilijazia Muhimbili.

Pole mkuu,mwanzo nilienda pale tawi lao la tazara haikupita wiki nikaunganishwa kweli mesej iliingia.Baada ya mwaka huduma hiyo ikawa tabu kwangu ,nikaenda pale mliman city ,nikasubir mesej ndani ya wiki mbili nilipoona kimya nikareport sasa nimeunganishwa tena,nakushauri tembelea tawi lililo karibu nawe waeleze tatizo lako tena ujaze form upya.
 
Huduma za NBC Zanzibar ziko slow sana na haziridhishi, mimi nimeshajaza hiyo form mara mbili, mwaka jana na mwaka huu, hadi leo sijapokea SMS yoyote.

Halafu mwaka huu kumekuwa na tatizo la ATM cards kumezwa bila sababu inayoeleweka, nimefuatilia nikaambiwa kadi nyingi zina matatizo hivyo zinahitaji kubadilishwa, wanajibu wateja hovyo hovyo, hawakuombi hata samahani.

Badala ya kuwataarifu wateja warejeshe kadi mbovu ili wapewe mpya wakatumia strategy ya kuzi capture kwenye ATM machine, yaani ni usumbufu mkubwa mno kwa wateja kwani unatakiwa kujaza fomu ya kuomba kadi mpya, ukawatolee copy ya kitambulisho, upigishwe foleni, uzungushwe mara kwa huyu mara kwa yule, yaani upuuzi mtupu.

Ninafahamu watu wengi zaidi wanaosema wamefunga account zao NBC kuliko wanaosema wamefungua account mpya, shame on National Bank of Commerce.
 
NBC huduma ya mobile banking mie nimeshajaza fomu Mara Tatu. Sijui tatizo ni nini nikirudi huwa wananipa fomu mpya nijaze nimeona michosho nimeamua kufungua CRDB
 
Ha hahaha..mimi wameniunganisha baadaya ya kujaza form mara 4 lakn bado ilikuwa hola,ila nilpo badili kadi nikajaza inf.upya..hapo ndpo nilpopata huduma ya sim banking hiyo ni baada ya miaka 2
 
NBC huduma ya mobile banking mie nimeshajaza fomu Mara Tatu. Sijui tatizo ni nini nikirudi huwa wananipa fomu mpya nijaze nimeona michosho nimeamua kufungua CRDB
Wadau,

Mimi ni mteja wa NBC, Jumatatu tarehe 02 June 2014 nilitembelea tawi la NBC Zanzibar kwa ajili ya kupata huduma za kibenki.

Baada ya kumaliza kilichonipeleka hapo benki nikaona ni vyema pia nijiunge na huduma ya Mobile Banking yote ni katika kurahisisha maisha.

Nikaelekezwa na kujaza fomu pamoja na kopi yangu ya kitambulisho kisha nikaambiwa nitapokea message ya kuunganishwa na huduma hiyo.

Mpaka sasa sijapokea message yoyote hivyo nikaona ni vyema nipite Benki ili kujua kinachoendelea. Majibu niliyopata ni kuwa bado sijaunganishwa kwa kuwa wanaounganisha huduma ya NBC mobile banking ni makao makuu Dar.

Tatizo ni kwamba hata huyu aliyechukua fomu yangu hajui ni lini nitaunganishwa na hiyo huduma maana anakisia tu kuwa labda nicheki leo mchana.

Niliwahi kuomba huduma kama hii kwa benki nyingine na niliunganishwa ndani ya dakika tano.

Najiuliza huu ni uzembe wa tawi la benki kwa maana ya NBC Zanzibar? Au ni uzembe wa huyu anayenihudumia au ni mifumo mibovu ya NBC Makao makuu?

Inakuwaje huduma ndogo kama hii inachukua zaidi ya siku nne kuunganishwa? Au ni kutaka tuendelee kupanga foleni benki kwa huduma ambazo zisingetupasa kwenda benki?

Kwa wanaotumia huduma hii ya NBC Mobile banking mliunganishwa baada ya siku ngapi?

Ushauri tu, Banki zetu zijifunze kutoa huduma bora na sio kubabaisha katika ulimwengu ambao makampuni mengi ya kifedha yanatoa customer care nzuri na ya kuridhisha.
Mkuu sio NBC tu mm niko benki ya posta nimeihangaikia hiyo huduma zaidi ya miez 5 nimeshajaza hizo form zaid ya mara tatu na huduma sijaipata na ukiwafuata kila mhudumu anakupa sababu yake. Mara huduma hiyo haifanyi kazi kwenye simu za lain 2, mwingine simu za android hazikubali hiyo huduma, mwingine no problem tutakuunganisha soon yan mpaka nimechoka nafikiria kuhama tu.
 
Njooni Equity Bank, kila kitu instant. •Account opening
•ATM card issuance
•Mobile banking
•Internet Banking
Sijaona bank yenye robust systems kama za hawa jamaa Tz yote. Malipo ya cheque hayachelewi, ikibounce utapigiwa simu. Aaah...keep the good work Equity Bank.
 
Mkuu sio NBC tu mm niko benki ya posta nimeihangaikia hiyo huduma zaidi ya miez 5 nimeshajaza hizo form zaid ya mara tatu na huduma sijaipata na ukiwafuata kila mhudumu anakupa sababu yake. Mara huduma hiyo haifanyi kazi kwenye simu za lain 2, mwingine simu za android hazikubali hiyo huduma, mwingine no problem tutakuunganisha soon yan mpaka nimechoka nafikiria kuhama tu.
Wafanyakazi wengine kwenye hizi taasisi ni Vimeo sana.
Yaani hawajui wanachofanya zaidi ya kukupa vijisababu visivyo na maana kabisa.
 
  • Thanks
Reactions: Mss
Mkuu inategemea na branch ulipojazia hizo form, siwatetei ila mimi nilipata huduma hiyo within one day NBC branch ya Lindi
 
Back
Top Bottom