How to go from Girlfriend to Wife

How to go from Girlfriend to Wife

Kuna wanawake kwa ajili ya kupotezea muda tu ambao hawafai kuolewa kabisa na kuna wanawake ambao wanafaa kuolewa. Sasa ukiona umekaa miaka 6 ukaachwa ujue hufai kuwa mke kabisa sema tu bahati mbaya umeumbwa mwanamke
 
Kuna mmoja anasema hata miaka 10 yupo tayari kunisubiri ili nimuoe. Namuonea  huruma she's too kind, nawaza vp ikitokea nisipomuoa🙁
Mwambie tu ukweli ili akipata wanaeendana aolewe
 
Pamoja na mambo mengi mazuri yanayopatikana katika ndoa jambo moja muhimu na kiunganishi kizuri kwa hayo mengine ni "tendo la ndoa". Hili huleta muunganiko wa kiwango cha juu sana kati ya mume na mke.

Sasa tatizo linapotokea katika hatua ya urafiki ni kuanza kujamiiana kabla ya ndoa.
-haraka za kuoana huisha kwa kuwa wanakipata kitu ambacho kilitakiwa kupatikana kwenye ndoa tu.
-Kuaminiana kunapungua kwa kuwa wameweza kushawishiana kushiriki tendo kabla.
-kama mmojawapo alikuwa bikra (sijui wanaume wanaitwaje) mwenzake humwona ni mshamba na hajui chochote ktk tendo.
-kama binti kabeba mimba na kuzaa, hutokea mabadiliko ya mwili unene, wembamba, maziwa na hata sehemu nyeti wakati mwingine na kumfanya mwanamme kuona wengine ambao bado ni vigori. Laiti wangekuwa kwenye ndoa angezidi kuvutiwa na mkewe bila kujali mabadiliko.
-heshima ya binti kwa kweli huwa ni pale tu anapokuwa hajamvulia nguo kijana. Akishavua nguo kabla ya kuoana basi tena thamani inashuka.
 
Mimi nikipata mdada anaejielewa hata kesho namuoa.
 
Nyie wanaume uwa siwaelewi. Na hakuna kesi mbaya kama hizi za watu wanaopendana alafu wakagombana. Yan unaweza kuona hapa upendo hakuna kabisa lakini after sometimes wanarudiana tena. Unajua uwa nashangaa sana.
Tatizo tuki gombana nyie huwa na kauli chafu sana
Halafu huwa mna tuchukia
 
Hainaga formula inategemea na mwanaume...
All in all ndoa isiwe the only thing u want in life, kuwa na maisha yako mwenyewe befr and after marriage
 
My singles, lets hear what these married folks have to say kwa kweli. Maana wengi wangetamani kuendeleza girfriend/boyfriend to wife/husband, lakini wengi mambo huenda ndivyo sivyo. Kuna watu unawaona wanaendana hadi raha lakini inakuwa hola! Nini kiweje? kuna formula au hakuna? Nini kinamuweka mtu 6 solid years kwenye u girlfriend/boyfriend then anakuja ingia mjengoni mtu mpya hata 6 months hajamaliza.

Yani unashuhudia mdada kaachwa solemba kwenye mataa na kipete chake kidoleni, mwingine ashafua sana majeans na kudeki kwa mkaka, amepika amepakua, mwingine kajibebesha mimba kamzalia jamaa lakini waapi! ila wanaume nyie nyie God is watching. Hivi kwani kama unamipango yako mingine why umkeep mtu kwa matumaini muda mrefu? Au wadada wengine ving'ang'anizi? Na wale wengine wasotea miaka sita ndo wanaingia huko lol!

Mnacheleweshwa na nini kwani jamani? Hayaaaa mje mshushe experience zenu na mawaidha hapa ili watu wasiimbe sana ule wimbo wa teeeenda miujiza Bwana teeendaa muuujiiizaaa usiache Mungu mwaka huu upiteee bila kuteeenda Muujizaa, it may help! Hamuwezi jua walioko kwenye hilo janga labda wakajikwamua.

Karibuni
kuna mzee (amestaafu 2017),rafiki yangu sana.eneo ambalo nafanyia kazi yeye alifanya kazi miaka 30 ilopita.kwenye utani nikamwambia kwa nn ulimwacha upendo ukamchukua bahati enzi hizo na upendo umekuwa nae mda mrefu jamii inajua upendo ndo ataolewa ukilinganisha shepu elimu mnaendana:-
akaniambia kuwa
upendo anapenda starehe na kupewa kila kitu kufanyiwa hata kazi ndogo ndogo
bahati hata nilipokuwa na matumizi mabaya alinishauri kwa upole kuhusu maisha na muda.
hata nilipomtoa out matumizi yake yalikuwa yana reflect kesho tuna amkaje lakini upendo yy haijui kesho tunaamkaje
bahati anaulizia hata mama na ndugu zangu na inapotokea kuna mgogolo haangalii haki anaangalia suluhu
upendo anapenda kuongelea matukio ila bahati anapenda kuongelea issues
upendo hajali mudi niliyokuwa nayo siku huskaila bahati amenielewa ambaye urafiki wetu ulikuwa wa muda mrefukwa uda mfupi kuliko upendo japo wote wanajali
 
Kuna mmoja anasema hata miaka 10 yupo tayari kunisubiri ili nimuoe. Namuonea  huruma she's too kind, nawaza vp ikitokea nisipomuoa🙁
Chaa hv mabinti wana shda gani..mwanaume hana mwelekeo mpe live usipooa wataoa wenzakooo,ieleweke wazii...tunayashuhudia ya Zama vs Ruge in the mean time
 
mimi nilipooa
niliangalia
upendo na kunitambua na kujitambua,uwezo wake wa kufanya maamuzi yenye hekima na busara. na nikifa anweza lea familia pekeyake?
 
Nimekupenda na weusi wako wa asili, unakuja kwangu unaanza kujichubua ili iweje? SIKUOI

nilikuwa napenda sana jinsi ulivyo na nywele asili, ama ka kichwa kako ukikata nywele unakuwa mrembo hasa, Leo upo na Mimi wewe kutoa mawigi..SIKUOI

Ulikuwa mcheshi sana kipindi cha uchumba kwa ndugu zangu, Leo hii ungekuwa wewe ndio kidume ndani kelele mtindo mmoja..SIKUOI AISEE

Nilikuwa nakupendea hicho kijungu cha wastani Leo unajiachia mwanamke unakuwa na KITAMBI.. Haki ya mungu SIKUOI

wakati tukaanza mahusiano ulikuwa una adabu sana na pesa, Leo 20000 haikutoshi..AISEE SIOI WACHA WASINIELEWE
 
Back
Top Bottom