Hotuba ya mzee Rashidi Mfaume Kawawa kwenye maandamano ya kupinga mapinduzi ya Iddi Amin Dadaa Uganda

JosephNyaga

JF-Expert Member
Apr 28, 2014
291
232
Juzi nilikuwa nasikiliza hiyo hotuba TBC Taifa kwa kweli ni hotuba hatari sana. Hii ngoma kati ya Tanzania na Iddi Amin kumbe ilianza kutimka vumbi Dar es Salaam kuanzia siku ya kwanza kabisa ya Amin alipochukua ofisi baada ya kumpindua Apollo Milton Obote. Mzee Kawawa aliongea kwa ukali na sauti ya juu mpaka ikawa kama imeisha na inagoma kutoka aliongea vitu hatari sana kwa hisia na uzalendo mkubwa sana mpaka nikasema kwa kweli hawa wazee wetu walikuwa viongozi wa kipekee na adimu sana kuwapata.

Mwenye hii hotuba tafadhali ailete tena hapa niirudie kuisikiliza.
 
Back
Top Bottom