JosephNyaga
JF-Expert Member
- Apr 28, 2014
- 291
- 232
Juzi nilikuwa nasikiliza hiyo hotuba TBC Taifa kwa kweli ni hotuba hatari sana. Hii ngoma kati ya Tanzania na Iddi Amin kumbe ilianza kutimka vumbi Dar es Salaam kuanzia siku ya kwanza kabisa ya Amin alipochukua ofisi baada ya kumpindua Apollo Milton Obote. Mzee Kawawa aliongea kwa ukali na sauti ya juu mpaka ikawa kama imeisha na inagoma kutoka aliongea vitu hatari sana kwa hisia na uzalendo mkubwa sana mpaka nikasema kwa kweli hawa wazee wetu walikuwa viongozi wa kipekee na adimu sana kuwapata.
Mwenye hii hotuba tafadhali ailete tena hapa niirudie kuisikiliza.
Mwenye hii hotuba tafadhali ailete tena hapa niirudie kuisikiliza.