Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu Majaliwa aliyoitoa leo tarehe 22.04.2016

Uliepost ungejirecord ukiwa unasoma tukakusikiliza kwenye audio ila wengine ni wavivu wakusoma vitabu mana hii hotuba kubwa sana du
 
Watanzania wengi hawana hulka ya kusoma. Ili kuchangia inabidi kusoma na kuelewa kilichoandikwa kwanza.
 
CCM MNAJITENGENEA CHUKINZAIDI KWA UBABE WENU WA KUTOONYESHA BUNGE LIVE. NAKUMBUKA MLISEMA NI GHARAMA KUONYESHA LIVE WAACHENI WENGINE WAONYESHE LIVE LAKN KAMA NI WAFANYAKAZI KUTOFANYA KAZI KWA SABABU YA BAADHI YA STAFF KUANGALIA BUNGE OFISIN KWANINI MSIPIGE MARUFUKU TV MAOFISINI?
 
Ukuaji wa Uchumi

18.Mheshimiwa Spika,malengo yetu ya kufikia Nchi ya kipato cha kati na kufanyika mapinduzi makubwa ya viwanda yanategemea sana utulivu wa uchumi. Kwa ujumla, ukuaji wa uchumi umekuwa wa kuridhisha kwani mwaka 2015, uchumi ulikua kwa asilimia 7.1 ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 7.0 mwaka 2014. Sekta zilizochangia katika ukuaji huo ni pamoja na Ujenzi, Mawasiliano, Fedha, Uchukuzi na Nishati. Pamoja na ukuaji huu mzuri wa ujumla, Sekta ya Kilimo inayoajiri zaidi ya asilimia 66.3 ya Watanzania wote wanaofanya kazi ilikua kwa asilimia 3.4 tu mwaka 2014. Ukuaji huo mdogo unamaanisha kwamba juhudi za ziada na kubwa zinahitajika ili sekta hii muhimu iweze kutoa mchango mkubwa zaidi wakati tunapotekeleza Mpango wa Pili wa Maendeleo. Historia ya maendeleo ya uchumi inatuambia kwamba, Sekta ya Kilimo ina mchango mkubwa na muhimu kwenye mapinduzi ya viwanda. Hivyo hatuna uchaguzi mwingine bali kuelekeza nguvu zaidi kwenye sekta hii ya kilimo.
Ahadi hii ilitekelezwa.
 
Back
Top Bottom