Nimejaribu halotel na ni kweli speed yao iko vizuri sanaaa, kwa hilo wanastahili pongezi. Ila bado sijaelewa inakuaje MB kuisha kwa kasi sana tangu nianze kutumia halotel. Natumia line ya chuo na imetokea mara 3 GB 1 kuisha ndani ya masaa 16, kitu ambacho sio cha kawaida wakati matumizi ni ya kawaida sana, yani ku-browse, whatsapp, fb, jf na instagram tu. siku ya kwanza nkachkulia poa, kesho yake ikajirudia tena na siku iliyofuata tena. Nkaona huu utoto, nkarudi tigo juzi. Waangalie hilo kiukweli