Hongereni serikali sikivu ya ccm, shule zote zipo katika hali nzuri tu, hazina uchakavu hata chembe ni propaganda za upinzani kutaka kuwakosanisha na wananchi, nyie ni wapiga kazi balaa ndo maana mpo kwenye BMK mkichakalika ili kutuletea katiba iliyo bora huku mkipokea pesa kiduchu laki 3 kwa siku mkiwa mmeacha mamilioni mpokeayo kwa siku ninawapongeza sana kwa hilo, mahospitali na zahanati zetu ndo usiseme maana zimejaa madawa na vifaa tiba kedekede, wajawazito hawalali mzungu wa nne vitandani na wengine chini maana vitanda vipo vya ziada, hamna wajawazito wanaofariki kwa kukosa huduma muhimu na hilo tujipongezeni
Viongozi na familia zao huenda nje siyo kwa minajili ya kutibiwa bali kwenda kulinganisha hali za utabibu za wenzetu zilivyo chini kuliko zetu, big up kwa sana, vyuoni mikopo hutolewa kwa wingi hasa kwa watoto wa masikini na watoto wa wakubwa mara nyingi hupata asilimia 100 ili kuwafuta jasho wazee wao kwa uzalendo ulotukuka nchini, madada zetu wa chuo wanaosimama mabarabani wakati mwingine ni kwa ajili ya kutafuta tu kipato cha ziada maana boom walilopewa huishia kwenye brazilian hair na viwalo vya kukata na shoka, alama za ufaulu zimeongezwa na serikali hii sikivu kiasi kwamba mwanafunzi wa sekondari kufeli ni ndoto, hao wanaowasema ni wivu wa kike unawasumbua na mtaendelea kutawala nchi hii kwa miaka elfu na moja, hongereni sana.