BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Mbunge asaidia kifaa cha ultrasound
Hassan Simba, Mtwara
Daily News; Thursday,October 16, 2008 @20:20
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Anastazia Wambura, ametoa msaada wa kifaa cha kupimia magonjwa (ultrasound) kwa Hospitali ya Wilaya ya Tandahimba, mkoani humu.
Akikabidhi msaada huo uliogharimu zaidi ya Sh milioni 70 katika hafla iliyofanyika hospitalini hapo juzi, Wambura alisema lengo ni kuwawezesha wananchi kupata huduma ya vipimo vitakavyowawezesha wapate tiba sahihi.
Sasa madaktari wetu wataweza kutambua ugonjwa unaomsumbua .ile dhana ya kutumia dalili kama kielelezo cha ugonjwa sasa itakuwa haipo. Kutokana na kukosekana kwa kifaa hiki wataalamu wetu huenda walikuwa wanatoa tiba kinyume na maradhi ya mgonjwa, alisema Mbunge huyo.
Alifafanua kuwa msaada huo umetolewa na rafiki zake nchini Ujerumani na kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imegharimia kusafirisha vifaa hivyo kufanikisha lengo la kuboresha huduma hizo za afya katika hospitali hiyo.
Kifaa hiki kitatumika pia kupima maendeleo ya mtoto awapo tumboni mwa mama yake, hivyo kupunguza vito vya watoto na wajawazito wakati wa kujifungua si ultrasound pekee bali pia nimeleta kifaa cha kupimia shinikizo la damu, sukari mwilini, uzito wa mtoto na kifaa cha kupumulia alisema Wambura.
Awali akisoma taarifa, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk. James Ligwa alisema msaada huo umeondoa adha kwa wagonjwa ya kwenda Hospitali ya Mkoa Ligula kupata vipimo, jambo ambalo alisema lilikuwa kero kubwa kwa wananchi wa wilaya hiyo.
Akipokea msaada huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Ndingo aliwataka wataalamu wa kutumia kifaa hicho kukitumia kwa uangalifu ili kisiharibike katika muda mfupi.
Hassan Simba, Mtwara
Daily News; Thursday,October 16, 2008 @20:20
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Anastazia Wambura, ametoa msaada wa kifaa cha kupimia magonjwa (ultrasound) kwa Hospitali ya Wilaya ya Tandahimba, mkoani humu.
Akikabidhi msaada huo uliogharimu zaidi ya Sh milioni 70 katika hafla iliyofanyika hospitalini hapo juzi, Wambura alisema lengo ni kuwawezesha wananchi kupata huduma ya vipimo vitakavyowawezesha wapate tiba sahihi.
Sasa madaktari wetu wataweza kutambua ugonjwa unaomsumbua .ile dhana ya kutumia dalili kama kielelezo cha ugonjwa sasa itakuwa haipo. Kutokana na kukosekana kwa kifaa hiki wataalamu wetu huenda walikuwa wanatoa tiba kinyume na maradhi ya mgonjwa, alisema Mbunge huyo.
Alifafanua kuwa msaada huo umetolewa na rafiki zake nchini Ujerumani na kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imegharimia kusafirisha vifaa hivyo kufanikisha lengo la kuboresha huduma hizo za afya katika hospitali hiyo.
Kifaa hiki kitatumika pia kupima maendeleo ya mtoto awapo tumboni mwa mama yake, hivyo kupunguza vito vya watoto na wajawazito wakati wa kujifungua si ultrasound pekee bali pia nimeleta kifaa cha kupimia shinikizo la damu, sukari mwilini, uzito wa mtoto na kifaa cha kupumulia alisema Wambura.
Awali akisoma taarifa, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk. James Ligwa alisema msaada huo umeondoa adha kwa wagonjwa ya kwenda Hospitali ya Mkoa Ligula kupata vipimo, jambo ambalo alisema lilikuwa kero kubwa kwa wananchi wa wilaya hiyo.
Akipokea msaada huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Ndingo aliwataka wataalamu wa kutumia kifaa hicho kukitumia kwa uangalifu ili kisiharibike katika muda mfupi.