rashidikurwa
Member
- Jul 16, 2017
- 34
- 26
Huyu ni mkurugenzi mtendaji wa Itv/Radio One, ni Mama shupavu, jasiri na mwenye uthubutu ambapo kwa miaka zaidi 15 amezisimamia taasisi hizi kwa kuwa na vipindi imara vyenye kuleta tija ya maendeleo katika taifa letu.
Ikumbukwe kuwa huyu ni Mama pekee anayeongoza taasisi hii ya habari ambayo imeweza kudumu katika tasnia hii kwa zaidi ya miaka 20, na kuendelea kuaminiwa na watanzania walio wengi.
Kwa taifa lolote linalohitaji kuwa na maendeleo ya kiuchumi na kisiasa linahitaji kuwa na vyombo vya habari imara kama Itv/Radio One, uwezo aliounyesha Mama huyu ni mkubwa na sitaweza kuumaliza katika ukurasa huu. Itoshe tu kusema wewe ni miongoni mwa wazalendo wa taifa letu. Hongera sana.
Sent using Jamii Forums mobile app
hahahaha wewe kila mtu na kila media na watu wake unajua hali zao hahaha.Najaribu kulinganisha hizi hongera zako ulizompa Mama Joyce Mhaville na lawama za kila siku za Wafanyakazi wa Radio One na ITV kuwa wana maisha magumu, huku kutwa wakiishia tu ' Kugongea ' Mihogo pale Kona ya ITV na kwenda kula Chakula cha ' Kushea ' pale Kambi yao Kuu ya Maryland Hotel huku ' mishahara ' yao ikicheleweshwa na kulimbikizwa.
Ama kweli leo nimeamini kwamba ' usilolijua ni sawa na usiku wa giza '.
Hongera sana Mama Joyce Mhaville kwa hizi pongezi / kongole za ' Kinafiki ' ulizopewa.
hahahaha wewe kila mtu na kila media na watu wake unajua hali zao hahaha.
Nakupa like za kutosha.... Pale Maryland wakikaaga wanaboa sana yaani.Najaribu kulinganisha hizi hongera zako ulizompa Mama Joyce Mhaville na lawama za kila siku za Wafanyakazi wa Radio One na ITV kuwa wana maisha magumu, huku kutwa wakiishia tu ' Kugongea ' Mihogo pale Kona ya ITV na kwenda kula Chakula cha ' Kushea ' pale Kambi yao Kuu ya Maryland Hotel huku ' mishahara ' yao ikicheleweshwa na kulimbikizwa.
Ama kweli leo nimeamini kwamba ' usilolijua ni sawa na usiku wa giza '.
Hongera sana Mama Joyce Mhaville kwa hizi pongezi / kongole za ' Kinafiki ' ulizopewa.
Tafakari mara mbili haya mawazo yakoI like her, she is a straight forward woman, no bling bling. She studied in Russia. Dah ila hana mtoto wala mme. Some time kutokuolewa nako ni kuzuri especially kwa career woman kuexel zaidi.