Hongera Prof. Ndalichako, pole Eliakim Maswi

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Napongeza na kutoa pole. Kwa watendaji wawili wa kiserikali. Wa kwanza, ninayempongeza, ni Waziri wa Elimu Prof. Joyce Ndalichako. Ni jana tu, Waziri Ndalichako ameagiza kufutwa kwa mfumo wa GPA kwenye kusahihisha na kutoa matokeo ya mitihani kwa kidato cha pili, cha nne na cha sita.

Mfumo wa GPA ulikuwa ukipigiwa kelele na wadau wa elimu nchini. Ulikuwa ukionesha kuwa mitihani ilikuwa ikisahihishwa kwa kuwapendelea wanafunzi. Mitihani ilikuwa ikisahihishwa kisiasa ili ionekane kuwa elimu imeimarika kwa wengi kufaulu. Elimu iliendelea kushuka na kusawajika. Hata vyuoni sasa, wanaokwenda ni kama wasiokwenda.

Kuanza kurekebisha mfumo wa elimu ni hatua njema. Waziri Ndalichako unastahili pongezi na kupewa moyo wa kufanya kazi kuirejesha elimu yetu kwenye heshima yake. Anayefaulu afaulu kweli, anayefeli afeli kweli. Si kinyume chake kama ilivyokuwa. Madaraja ya kwanza, pili,tatu,nne na sifuri ni muhimu. Hata udahili vyuoni utakuwa rahisi.

Pili, natoa pole kwa Ndugu Eliakim Maswi. Ndugu Maswi alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara. Baadaye, mwka jana mwishoni, aliteuliwa kuwa Kaimu Naibu Kamishna Mkuu wa TRA. Jana, amerejeshwa Manyara kuendelea na kazi yake ya awali-Katibu Tawala wa Mkoa kwa kile kinachosemwa kuwa 'amemaliza kazi yake aliyotumwa TRA'.

Siasa hutumia maneno ya kisiasa na kisasa. Ndiyo hayo ya kumaliza kazi aliyotumwa TRA. Kiukweli, Maswi hakuweza kuhimili manenomaneno pale TRA kuwa yeye si 'msafi' kuendesha chombo kilichosafishwa cha TRA. Alihusishwa na sakata la Esrow. Maneno hayo yalimfikia Rais Magufuli. Rais akaamua kumuondoa. Hakuwa ameteuliwa kwa 'kazi maalum pale TRA'.

Nampa pole Maswi kwakuwa kuondolewa kwake TRA na kurejeshwa Manyara ni kama kushushwa cheo. Maswi ameondolewa kistaarabu kwa maneno ya kistaarabu. Hata watanzania wengi wameamini kuwa Maswi ameondolewa kwakuwa amemaliza kazi yake TRA. Ukweli uko tofauti na hivyo.

Pole Maswi kwakuwa Escrow is still haunting you Comrade!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
maswi angekuwa haongi malaya kwa fedha za escrow angekuwa tajiri sana, tatizo lake ni Hongo nzito anazotoa vinginevyo angeshaacha kazi kwa dana dana anazopigwa kila kukicha
 
Kama ni kweli alipelekwa kufanya kazi maalum "tutasemaje"? Maswi aliwahi kufanya kazi za kawaida kabisa tena kwa vyeo vya chini kabla ya kupanda katika nafasi tumjuazo nazo leo. Hivyo kutolewa kwenye u-naibu Kamishna wa TRA kwenda RAS Manyara (ambako alikuwa) haina tofauti na alivyoondolewa u-katibu Mkuu wa Nishati na Madini na kupelekwa RAS Manyara. Kazi yake maalum ipo popote atakapoamriwa kwenda. Ndiyo nature ya kazi yake. Tusije shangaa tukamkuta siku moja ni MWEHU pale Sarender Bridge teh teh teh tukaambiwa alishakuwa mwehu ama akishinda kando ya ufukwe wa bahari kule OCEAN ROAD na kucheza na miti, nyasi na mchanga. Ni kawaida sana. Bravo Maswi kwa kuikamilisha kazi MAALUM.
 
...mbona hamzungumzii ukurupukaji wa Magufuli;kabla hajamteua Maswi alikua hafahamu record zake za nyuma? au alijaribu tu kumteua ili kupima upepo ambao umemshinda?!
 
...mbona hamzungumzii ukurupukaji wa Magufuli;kabla hajamteua Maswi alikua hafahamu record zake za nyuma? au alijaribu tu kumteua ili kupima upepo ambao umemshinda?!
Na leo kamteua mzee fastjet kuwa mkuu wa chuo kikuu cha DSM!! Madudu yote haya anayoangahika nayo (kama sio usanii) yalisababishwa na huyu huyu fj, na bado akaona ndiye anafaa kuwa sura ya chuo kikuu kikongwe nchini!! Nimeishakubali kuwa JPM ni tingatinga - ukiishaliwasha tu basi linakata mbuga hata likikuta kitoto kichanga kimelala njiani linaswaga tu.
 
unajua wako watu wanajifanya kujua sana,ilimradi mpaka wale za uso ndio wanaelewa.Kiukweli,Maswi hafai,Muhongo hafai.Maswi alikuwa anawafuatilia viongozi wenzake pale wizarani kwenye accounts zao,na maisha yao kila siku.Wakati yeye ndie alikuwa mpiga deal mkubwa.Serikali inajua haya mambo,halafu cha kushangaza mnataka kuanzisha mahakama ya rushwa.Tunawajua wala rushwa wakubwa,na wadogo,lakni watakao shitakiwa ni wale wadogo.
mfano,mwakyembe ana usafi gani? chama chote cha CCM kinanuka rushwa.Magufuli nae ana kashfa chache sio nyingi lakni moral right anayokuwapeleka mahakamani?
Mimi ushari wangu kwa raisi Magufuli,Mavi ya kal hayanuki.Kama anataka kuwafunga na kuwafukuza wafanyakzi wote serikalilni basi aanze yeye mwenyewe na chama chake kujiuzulu na waingie ndani?
Namshauri sana,ni bora awe na uhusiano mzuri sana na wafanyakazi wa serikali ndio atajenga moraly,nguvu kazi,ubunifu nk.Mambo ya kutishiana sehemu za kazi sio na yule atakayethibitika ameiba mali ya umma kipindi chako then unao wezo wa kufanya lololte.Lakni kwenda nyuma na kutafutana ni kutafuta matatizo na haujengi nchi.
 
Elimu bado haijatengamaa kabisa,hakuna sera madhubuti inayoirudisha elimu kwenye mstar.Kuna haja ya kutunga sheria kuja kulinda sera kila awamu inapoingia.Kumekuwa na kamtindo ka kila awamu ya urais,mawazir teule kujibadilishia au kutoa matamko ya kubadili mfumo wa masomo au mtihan,mfano j.mungai enz ya mkapa aliunganisha masomo ya kemia na physics kuwa moja,akafuta ek,akafuta masomo ya biashara na kilimo na michezo pia,kawamba chin ya jk,wakarudisha mfumo wa zaman,wakaanzisha mfumo wa gpa,Ndalichako chin ya jpm,wamerudisha mfumu wa zaman.Hapa jaman mfumo wa Elimu nchin bado haujatengamaa.Hakuna sera inayotekelezwa,tunaoneshana ubabe wa kutoa matamko kwa kila mawazir.
 
MTINDO WA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI KUCHAGUA MAJIBU KWA MITIHANI YOTE NAOMBA NDALICHAKO AFUTE
 
Back
Top Bottom