Wanajamvi, hii gari naipenda mpaka naumwa. Maana inaitwa Honda Crossroad a.k.a SMALL HAMMER. Naombeni ushauri wakuu kabla sijaingia mkenge. Ndo nataka nimiliki gari kwa mara ya kwanza. So, naipenda sana hio gari kimuonekano. Vip kuhusu spare zake, uimara, confotability, inshort nahitaji details zake kiujumla.
Mkuu wabongo Sisi ni waoga kuanzia wauzaji spare parts na wamiliki ndiyo maana wengi wetu tumelogwa na Toyota tu.
Hii gari kila mtu ataipenda Kwa muonekano wake isipokuwa Kwenye spares, kuhusu uimara ni gari imara kama umejipanga vizuri unaweza kuagiza tu
Vuta mkoko hiyo gari ni tamu sana,acha kutishwa na wajinga ati haina spea,ni wakati sasa wa sisi wa TZ kuendesha magari mazuri,chukua mchuma huo Kenya na Uganda kila kitu unapata