Homa ya Lassa yatua Benin, yaua watu wengi

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,720
55,843
lassa-fever-benin-edo-state-559x520.jpg

Homa ya Lassa yatua Benin, yaua wawili.

Ugonjwa wa homa ya Lassa bado imeendelea kuwa tishio na kuzitesa nchi za afrika Magharibi hususan Nigeria.

Taarifa ni kwamba tayari ugonjwa huo unaoenezwa na Panya, umeingia nchini Benin baada ya kutesa watu kadhaa kwenye mpaka na Nigeria huko Edo State.

Afisa wa afya jimboni humo Heregie Aihanuwa, amesema tayari wamepata taarifa za wagonjwa wa 5 kuripotiwa nchini Benin pamoja na maiti mbili.

Idadi ya watu waliopoteza maisha nchini Nigeria kutokana na ugonjwa wa homa ya Virusi vya Lassa, imeongezeka mpaka 35 kutoka watu 2.

Mikoa iliyoathirika na kutoa wagonjwa wengi zaidi ni pamoja na Ibadan Oyo, Taraba, Kano, Edo na Niger.
 
Duh! Ebola imetulia juzi Tu sasa Ni lassa! Mungu tunusuru maana wanadamu wanafanya yao..
 
Aisee, Mungu atunusuru, huku kwetu kipindupindu kimeshindikana kutokomezwa na sababu twaambiwa ni kuacha kula kinyesi tu, sasa hii ya panya si tutaangamia kabisa?
 
Back
Top Bottom