Hoja ya utajiri/umaskini wa mikoa

Hoja ya utajiri/umaskini wa mikoa

mbinguni

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2013
Posts
2,767
Reaction score
1,068
Nimeshtushwa kidogo na uzi uliomo humu. Vimetumika vigezo gani kwenye tathmini husika? Inawezekanaje kwa mikoa kama Njombe na Songwe kwa upya wake na kuathiriwa zaidi na ugonjwa wa UKIMWI(NJOMBE) ikaizidi mikoa kama Mwanza na Arusha.
 
Kwa mpangilio uliowekwa wazi, inawezekana. Mikoa ya Songwe na Njombe zinapata mvua ya kutosha na kilimo cha mazao mengi hustawi kwa sana.

Mkoa was Arusha hauwezi kuufikia mkoa wa Njombe hata kidogo hasa kwa upatikanaji wa mahitaji ya msingi, Chakula na ukwasi wa wananchi hasa vijijini.

Mkoa wa Njombe pia una watu wengi waliopata elimu ya mkoloni na hivyo kujua kufanya biashara ya kisasa ya kujiletea maendeleo kuliko Mwanza na Arusha.

Mkoa Njombe pia una biashara kubwa ya miti ya mbao kwa muda mrefu. Jina la Mkoa ni changa lakini Shughuli za kiuchumi sio changa.

Kikubwa sana na tofauti kubwa iliyoonekana waziwazi ni tofauti za kina cha elimu katika maeneo.
 
Nimeshtushwa kidogo na uzi uliomo humu. Vimetumika vigezo gani kwenye tathmini husika? Inawezekanaje kwa mikoa kama Njombe na Songwe kwa upya wake na kuathiriwa zaidi na ugonjwa wa UKIMWI(NJOMBE) ikaizidi mikoa kama Mwanza na Arusha.
Wewe huijui Arusha.. Kuna wilaya za Karatu,Longido,monduli..fika ujionee acha siasa
 
Kwa mpangilio uliowekwa wazi, inawezekana. Mikoa ya Songwe na Njombe zinapata mvua ya kutosha na kilimo cha mazao mengi hustawi kwa sana. Mkoa was Arusha hauwezi kuufikia mkoa wa Njombe hata kidogo hasa kwa upatikanaji wa mahitaji ya msingi, Chakula na ukwasi wa wananchi hasa vijijini. Mkoa wa Njombe pia una watu wengi waliopata elimu ya mkoloni na hivyo kujua kufanya biashara ya kisasa ya kujiletea maendeleo kuliko Mwanza na Arusha. Mkoa Njombe pia una biashara kubwa ya miti ya mbao kwa muda mrefu. Jina la Mkoa ni changa lakini Shughuli za kiuchumi sio changa. Kikubwa sana na tofauti kubwa iliyoonekana waziwazi ni tofauti za kina cha elimu katika maeneo.
... uko sahihi sana! Pamoja na miti ya mbao, mazao mengine ya biashara yanastawi vizuri Njombe - chai, miwati, viazi mviringo, n.k. Hali ya hewa ya Njombe inachochea pia mazao ya mbogamboga za kila aina, migomba, n.k. kustawi vizuri sana. Kimisingi, Njombe kunyofolewa kutoka Iringa kumeufanya uwe vizuri zaidi kiuchumi. Pia izingatiwe Njombe ni eneo ambalo wamisionari wa Kikristo walitia kambi muda mrefu sana hivyo suala la elimu na afya ni la kipaumbele tangu enzi. Na kimisingi hivyo ndio vigezo muhimu vinavyo-determine umasikini wa mahali.
 
Mkoa mingi yenye ahaueni ni kwa sababu ya effect ya elimu ya mkoloni, hali ya hewa na shughuli za serikali. Mkoa wa DSM ni wazi una ukwasi wa kutosha.

Mkoa wa Dodoma umepanda baada ya shughuli za serikali kuongezeka lkn hali mbaya kwa wilaya za Mtera, Kongwa na Kondoa vijijini.

Mimi naona takwimu zingetolewa kwa kila wilaya. Takwimu za mikoa zinadanganya sana. Hata kwa Mkoa wa Kilimanjaro wilaya za Same na Siha zinamezwa.

Kwa Mkoa wa Arusha ni halmashauri 3 tu zenye ahaueni, Arusha jiji, Arusha DC na Meru.

Longido na Ngorongoro hali ni mbaya zaidi. Karatu na Monduli pia sio nzuri ila zina nafuu.

Bado zinahitaji mkono wa serikali kupata huduma muhimu kama maji, barabara, huduma za afya, masoko, barabara ili wananchi waweze kujikwamua na kuchangia katika pato la Taifa.
 
Mimi nimepita wilaya zote za Mkoa wa Rukwa. Hakuna wilaya ya Mkoa wa Rukwa unaolingana kwa umaskini na wilaya ya Longido au Kiteto. Nashangaa sana Mkoa wa Rukwa kuwa wa kwanza kwa umaskini.
 
Ebu nisome vizuri. Njombe kuna janga la ukimwi. Hii taarifa imeandaliwa kisiasa zaidi na sio kiuhalisia.
Wewe huijui Arusha.. Kuna wilaya za Karatu,Longido,monduli..fika ujionee acha siasa
 
Njombe kuna population ndogo Sana kulinganisha na pato la mkoa.
Hivyo ukipigwa umaskini wa kipato unaonekana chini.


Ila kuna umaskini Sana huko njombe na bado haujaelimika.
 
Njombe kuna population ndogo Sana kulinganisha na pato la mkoa.
Hivyo ukipigwa umaskini wa kipato unaonekana chini.
Ila kuna umaskini Sana huko njombe na bado haujaelimika.
Mkuu Njombe ni kati ya maeneo yaliyopata elimu ya mkoloni toka siku nyingi. Ni eneo lenye wasomi wengi na walioshika madaraka labda imezidiwa na Kagera + Kilimanjaro tu. Kwa elimu wako juu. Umaskini wa Njombe sio wa kukosa Chakula, malazi na mavazi.
 
Wilaya zote ulizozitaja,watu wake sio maskini hata kidogo. Wengi wao ni wafugaji/wakulima,wakulima,wafugaji,wafanya biashara,n.k
Wewe huijui Arusha.. Kuna wilaya za Karatu,Longido,monduli..fika ujionee acha siasa
 
Mh! Maradhi,umaskini,mavazi na elimu bado vipo ktk hali mbaya sana kwenye mkoa huu wa njombe na songwe. Hili ni pambio la kuwarizisha kikundi fulani.
... uko sahihi sana! Pamoja na miti ya mbao, mazao mengine ya biashara yanastawi vizuri Njombe - chai, miwati, viazi mviringo, n.k. Hali ya hewa ya Njombe inachochea pia mazao ya mbogamboga za kila aina, migomba, n.k. kustawi vizuri sana. Kimisingi, Njombe kunyofolewa kutoka Iringa kumeufanya uwe vizuri zaidi kiuchumi. Pia izingatiwe Njombe ni eneo ambalo wamisionari wa Kikristo walitia kambi muda mrefu sana hivyo suala la elimu na afya ni la kipaumbele tangu enzi. Na kimisingi hivyo ndio vigezo muhimu vinavyo-determine umasikini wa mahali.
 
Longido na kiteto kuna biashara kubwa ya kilimo na ufugaji.
Mimi nimepita wilaya zote za Mkoa wa Rukwa. Hakuna wilaya ya Mkoa wa Rukwa unaolingana kwa umaskini na wilaya ya Longido au Kiteto. Nashangaa sana Mkoa wa Rukwa kuwa wa kwanza kwa umaskini.
 
Mh! Maradhi,umaskini,mavazi na elimu bado vipo ktk hali mbaya sana kwenye mkoa huu wa njombe na songwe. Hili ni pambio la kuwarizisha kikundi fulani.
Tatizo lako unataka kuaminisha kwamba Arusha ni bora kuliko Njombe lakini hauna tafiti ulioifanya zaidi ya bla bla na maneno ya kanga moko
 
mkuu Njombe ni level nyingine haina matajiri wakubwa sanaa ila watu wa milioni milioni ni wengi sana na kama seriakali ingefanya kazi yake basi Njombe ingekuwa mbali.Standard seven wengi wana CASH mbaya mtoto wa miaka kumi tatu anamiliki ekari mbili au tatu za miti ya mbao akifika miaka ishirini tano au sita tayari msitu ushakua akiuza anapata zake more that ten milioni mtaji tayari watu wanabaki kulia lia na ushirikina lakini watu wameshatembea nenda kaone Nyumba zinazojengwa vijijin sasa hivi pamoja na soko la mabo kuvurugwa

Nimeshtushwa kidogo na uzi uliomo humu. Vimetumika vigezo gani kwenye tathmini husika? Inawezekanaje kwa mikoa kama Njombe na Songwe kwa upya wake na kuathiriwa zaidi na ugonjwa wa UKIMWI(NJOMBE) ikaizidi mikoa kama Mwanza na Arusha.
 
Hili pambio mtaliimba hadi 2025 ndio utakuwa mwisho wake. Emdeleeni kumtumikia kafiri mpate mradi wenu
Tatizo lako unataka kuaminisha kwamba Arusha ni bora kuliko Njombe lakini hauna tafiti ulioifanya zaidi ya bla bla na maneno ya kanga moko
 
Mh! Maradhi,umaskini,mavazi na elimu bado vipo ktk hali mbaya sana kwenye mkoa huu wa njombe na songwe. Hili ni pambio la kuwarizisha kikundi fulani.
Kumbuka ni miaka michache tu imepita Njombe kama wilaya iliongoza kwa usafi Tanzania Na kuwa wilaya yenye choo bora.Mwaka huu Magufuli alivyotembelea mkoa wa Njombe akasema Wana ujenzi Bora wa Nyumba ukilinganisha Na maeneo mengine,sasa unafikiri watu Hawa watakuwa maskini?
 
Kuna uwezekano mikoa kama ya Arusha utajiri ukawa unamilikiwa Na watu wachache tu Na waliobaki wakawa katika Hali mbaya
 
Kuna uwezekano mikoa kama ya Arusha utajiri ukawa unamilikiwa Na watu wachache tu Na waliobaki wakawa katika Hali mbaya
Ndivyo ilivyo kwa hali halisi katika miji an mikoa mingi nchini. Hata DSM hali iko hivyo.
 
Back
Top Bottom