Hoja ya kumpokea Lowassa CHADEMA iwekwe kando

Hoja ya kumpokea Lowassa CHADEMA iwekwe kando

Mimenusa hisia na joto la wengi kuhusu hoja ya kumkaribisha Lowasa CHADEMA - Madhara yake ni makubwa kuliko viongozi wanavyodhania. Huu ndio ukweli wenyewe:

Hata kama Lowasa angepitishwa kuwa mgombea wa CCM, bado UKAWA wangefanya vizuri maana wananchi wanakiu ya mabadiliko.

Kitendo cha Kumpitisha Magufuli kimefanya kazi ya kuichachafya CCM kuwa nyepesi zaidi maana wafuasi wa Lowasa wengine bado ungekuwa mtaji wa UKAWA hata bila kumuingiza Lowasa katika kundi la UKAWA.

Kumkaribisha Lowasa na kundi lake ni Ku-bland UKAWA, haitauwa UKAWA tena maana wanaokuja na Lowasa ni waliopitisha KATIBA mbovu, vita yetu tutakuwa tumeipoteza kwa kujisalimisha kwa adui kia aina.

Lowasa na Kundi lake ni kama mbwa mwitu. watakao baki salama ni CCM maana wao magamba yatakuwa yamevuka, yamevaliwa na CHADEMA. Chadema yenye Rostam Azizi, Karamagi, Kingunge, Lowasa, n.k siioni kama CHADEMA ya kuleta nafuu kwa walalahoi. itakuwa ni Muungano wa CCM na CHADEMA, hapo itikadi na harakati zinatakiwa zibadilike, wananchi hatukuunga nkono CHADEMA mfanye hayo.

Hii agenda ya kumpokea Lowasa mmeitoa wapi? Mbona Wabunge wa upinzani wachache waliokuwa bungeni ndio wameshawishi watu wengi kuiunga mkono kwa sababu ya hoja zao? kwani nilini Lowasa alisimama bungeni akatoa hoja ya kueleweka? Lowasa anamtazamo gani kuhusu katiba Mpya?, kuhusu ufisadi?, kuhusu muundo wa muungano? atanadi vipi ilani ya uchaguzi asiyoiamini? au kunanini hasa la ziada?

Lowasa na kundi lake wakiingia CHADEMA, wengi tutatoka CHADEMA na iko siku viongozi wote mtajikuta mnatakiwa kutoka nje ya CHAMA kwa njia ya nguvu ya vikao na katiba ya chama halafu wanabaki wao. Huu utaratibu wa mtandao hawatauacha utawatafuna nyie mnao wakaribisha watu hawa. Itakuwa kama MREMA na TLP na Ngawaiya.

Nguvu ya CHADEMA kwa sasa ni kubwa, achana na agenda ya LOWASA kuja CHADEMA, tuletee ngombea wetu asiye sehemu ya watu wa LOWASA, sisi tumeisha jiandikisha, na tunasubiri masanduku ya kupiga kura. CHADEMA bila LOWASA inawezekana. MBOWE, anayekushauri ati utapata mtaji wa watu anakuongopea. wao kama wamechukia si watupigie kura tu, unatosha. usichafue chama. Hoja yetu kwa muda mrefu ni kwamba CCM ni mafisadi, akina LOWASA, ROSTAM AZIZI, KALAMAGI, sasa wamekuwa wasafi lini? yaani kukatwa kwa LOAWASA kumewasugua na kuwasafisha??? acha mzaha, sisi tuko serious na ukombozi wa nchi hii. Bora kukosa URAIS tukawa na wabunge wengi kuliko kuwa na LOWASA kama mgombea URAIS kwa CHADEMA.

Siku moja mtakumbuka maneno yangu.

PAPA1, ni mara yangu ya kwanza kuona na kusoma mchango wako katika mtandao huu, sina maana huwa hauchangii nina maana sikuwahi kusoma ulichokiandika. Na kwa kuwa nimesoma ulichokiandika nimevutiwa sana na aina ya uchambuzi wako na uwasilishaji wako wa hoja hii. Hakuna chembe ya kashifa kwa watu na hasa Mzee wenu ( mimi ni kaka yangu) Mhe. Lowasa lakini umeonyesha kutohitajika kwake katika chama cha Democrasia na Maendeleo. Haitajiki kabisa. Aachwe akajipange upya, huko huko CCM.
 
watu wengi wanaoongelea madhara ya kumwingiza chadema lowassa wanaonekana ama ccm au wanafiki lakini ukweli utabaki ukweli chadema wakimwingiza lowassa ndio kifo chao kwani watu wengi wamesapoti chdema kwa sababu wanachukia ufisadi na lowassa bado fisadi leo chadema wakimkaribisha itaonekana wazi chadema hawapingi ufisadi bali wanapinga kukosa fursa ya kufanya ufisadi.
CHADEMA hoja yao kuu iliyowapatia umaarufu ni vita dhidi ya ufisadi. Na alama kuu ya ufisadi kwa miaka takribsn nane iliyopita amekuwa ni LOWASSA na wapambe wake wakuu. Leo wanajadiliana na alama kuu ya ufisadi kuwa mshika bendera wa UKAWA.
 
CDM haihitaji EL ili kushinda uchaguzi October 2015 Kama wanampokea awe mwanachama Wa kawaida na labda akagombee ubunge lakini sio Urais kwa tiketi ya CDM..Low as ahajawahi kemea maovu ya chama chake hadharani hata Bungeni..kama Nawaza vile.
 
Kwa mbali nakiona chama cha ACT kama chama kikuu cha upinzania in the next five years to come.
 
lowasa anaweza kwenda UKAWA na kupeperusha bendera ya urais. kazi itakayolazimika kufanya na UKAWA ni kurekebisha kauli zao za kumwita fisadi wakati hajakatwa na kamati ya maadili ya CCM.
 
Lowassa haendi upinzani,anamuona maalim seif na mrema yaliyiwakuta!
 
CCM MNA mihemko sana si mtulie!! Mmeshamaliza yenu laleni!! Acheni wengine wafanye yao!! Kuumia mtaumia tu hakuna namna nyingine sasa. Nasema mtaumia Tena sana hakuna ---- in this era. Dhambi yenu ya kuchakachua imefikia 40 zake. No way wala HAMPONI this time.
wewe inawezekana kabisa ni mwana ccm lowasa hana uwezo wa kumshinda makufuli kwa uchaguzi mkuu sana sana umoja wa chadema atautingisha na kwenye jamii imani itakuja kuwa wote ni mafisadi nguvu kubwa iliofanywa na lissu itakuwa imekufa lowasa tangia amekaa bungeni hana nguvu ya kujenga hoja kwa kipindi chote na wananchi wanaitaji mabadiliko sio kukopi na kupesti
 
Back
Top Bottom