Hoja ya CHADEMA kuhusu katiba yachakachuliwa

Hoja ya CHADEMA kuhusu katiba yachakachuliwa

Izack Mwanahapa

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2011
Posts
497
Reaction score
236
Kimsingi watu wanapounda kamati ndogo ya kushughulikia jambo fulani huwa na malengo maalum, na kamati hiyo inatakiwa kuwa huru ili kufanya kazi yake kwa ufasaha. Hatuya ya kamati kuu ya ccm kumshauri kikwete kukutana na vyama vyote vya siasa imelenga kudhoofisha hoja ya Chadema kwani kama tunavyofahamu vipo vyama vinavyounga mkono mswada wa katiba vikiwemo CUF na TLP. Kama kweli vyama vyote vya upinzani vitakutana na rais tutegemee vichwa vya habari hivi hapa:

1. "Wapinzani wakaangana wao kwa wao"
2. "Mswada wa katiba kusainiwa kama kawaida; Ni baada ya wapinzani kukinzana"
3. Wapinzani watofautiana hoja ya katiba"
 
Pendekezo la Nec litatekelezwaje wakati tayari Rweyemam alikwishawajibu CDM kuwa Rais amekubali kukutana nao? Lakini vilevile CDM wanatekeleza makubaliano ya Nec yao, je vyama vingine vimefanya lini vikao na kufikia maamuzi hayo? Je vyama vingine vimeomba kukutana na Rais au vyenyewe vinaamuliwa maamuzi yao na Nec ya CCM?

Rais hawezi kubadili uamuzi wake aliokwisha ufanya hadi sasa wa kuwaalika CDM na kukiri kuwa hilo ni jambo jema.
 
itakua ni ajabu tena ya karne kwa rais kukubaliana na NEC na pia wanaojiita wapinzanzani CUF,TLP, UDP watakua wamejidhalilisha kukubali mwaliko usiowahusu, waliunga mkono hoja leo wanaenda kufanya nn?

Maoni yangu wawaache wanaume wakaongee wao watapewa maelekezo, NCCR sina tatizo nao ni kidume kinachoibukia na kimsingi madai yao na cdm hayaachani sana wanaweza wakashiriki wakawa ndimu kwenye kachumbari ili JK ale vizuri.
 
Kama hoja inahusu katiba ya nchi sijui Chadema wanaogopa nini, kama ni upinzani bungeni hawapo peke yao.
Nashawishika kuamini kuwa Chadema wanalazimisha kuolewa mke wa pili, nyumba ndogo au kuwa "Ccm C", nashawishika...
 
Mkubwa Izack umeonambali, kama hayo yatataokea kama unavyoona basi hivyo vichwa vya habari tajwa tuvitarajie... Nec Nec Nec.. sijui wanataka nn hawa watu
 
Kama hoja inahusu katiba ya nchi sijui Chadema wanaogopa nini, kama ni upinzani bungeni hawapo peke yao.
Nashawishika kuamini kuwa Chadema wanalazimisha kuolewa mke wa pili, nyumba ndogo au kuwa "Ccm C", nashawishika...

Angalia hiyo avatar yako. Hujapata jibu bado
 
Kimsingi watu wanapounda kamati ndogo ya kushughulikia jambo fulani huwa na malengo maalum, na kamati hiyo inatakiwa kuwa huru ili kufanya kazi yake kwa ufasaha. Hatuya ya kamati kuu ya ccm kumshauri kikwete kukutana na vyama vyote vya siasa imelenga kudhoofisha hoja ya Chadema kwani kama tunavyofahamu vipo vyama vinavyounga mkono mswada wa katiba vikiwemo CUF na TLP. Kama kweli vyama vyote vya upinzani vitakutana na rais tutegemee vichwa vya habari hivi hapa:

1. "Wapinzani wakaangana wao kwa wao"
2. "Mswada wa katiba kusainiwa kama kawaida; Ni baada ya wapinzani kukinzana"
3. Wapinzani watofautiana hoja ya katiba"

tunajua mkweli ni nani na mnafiki ni yupi so tunasubiri chadema wanasema nini!tushaona cuf hakuna kitu, wanaharakati hakuna kitu, sasa ni chadema na nccr wabunge wao wawili!
 
Kimsingi watu wanapounda kamati ndogo ya kushughulikia jambo fulani huwa na malengo maalum, na kamati hiyo inatakiwa kuwa huru ili kufanya kazi yake kwa ufasaha. Hatuya ya kamati kuu ya ccm kumshauri kikwete kukutana na vyama vyote vya siasa imelenga kudhoofisha hoja ya Chadema kwani kama tunavyofahamu vipo vyama vinavyounga mkono mswada wa katiba vikiwemo CUF na TLP. Kama kweli vyama vyote vya upinzani vitakutana na rais tutegemee vichwa vya habari hivi hapa:

1. "Wapinzani wakaangana wao kwa wao"
2. "Mswada wa katiba kusainiwa kama kawaida; Ni baada ya wapinzani kukinzana"
3. Wapinzani watofautiana hoja ya katiba"
Mkuu umenena kuhusiana na hili Unajua kiufupi TLP na CUF ni CCM haohao ila wanafanya kazi kwa kivuli cha upinzani, na hili limepangwa kwasababu wanaamini kama JK hiyo siku atakuwa katika hali ya kawaida kiakiri "Sound minded" basi ataelimishwa na kuelewa hata kama anajifanya kutokuelewa kwamba mchakato wa katiba mpya unachezewa kwa kigezo cha uwingi wa wabunge wa CCM
 
Back
Top Bottom