Hofu yatanda Ukerewe

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,037
Reaction score
34,741
[TABLE="width: 491"]
[TR="bgcolor: #E1E1E1"]
[TD]KUMEZUKA KUNDI Hatari linalojiita “Makhirikhiri” katika visiwa vya Ukerewe huko Ziwa Viktoria ambalo linahatarisha maisha ya watu kwa kuwachinja na kisha kuchukua viungo.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 3"]Kundi hilo linawateka watu umbali mrefu na kisha kuwachinja na hatimaye kuchukua viungo wanavyohitaji katika mwili huo

Imedaiwa kuwa, hali ni mbaya kwa kuzuka kwa watu ambapo sasa wakazi wa maeneno hayo kupatwa na hofu ya uhai wao kutokana na utekwaji hovyo wa watu kiunyama

Imedaiwa kundi hilo hutumia mbinu mbalimbali ikiwemo kuteka mabasi, pikipiki ya abiria na kisha kuamrisha vyombo hivyo kwenda wanapopahitaji na kisha kuchinja watu kinguvu na kujipatia viungo

Tayari watu kadhaa wameshatekwa na kuuawa na kundi hilo na kujipatia viungo na kudaiwa kundi hilo hata mchana wa jua kali hutembea na kuteka watu huku wakiwa na silaha

Moja ya viungo vinavyohitajika mara baada ya kuchinja mtu kikiwemo kichwa,Mikoni pamoja na sehemu za siri ndio viungo vikubwa wanavyohitaji watu hao[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Hofu yatanda Ukerewe
 
Kinachotusumbua watanzania ni ukosefu wa elimu pamoja na umaskini uliopindukia. Watu wanashindwa kuwa wabunifu wa shughuli za kiuchumi wanaishia kwenye imani hizi za kishirikina, za kuamini kwamba kichwa cha mtu kitampa utajiri nk. Viongozi wajao wajaribu sana kuona ni kwa namna gani watapunguza hali ya umasikini kwa watanzania, maana Kikwete kashindwa kabisa.
 
Mkuu Lukolo lakini

Sio hapo tu Tanzania mimi niliwahi kuwepo nchini Zambia mnamo mwaka 1980 huko Zambia kuna watu waliambia

kuwa kama unaweza kumleta Mtu mwenye kipara wataweza kunipatia pesa nyingi sana yuko mzee mmoja huko

Zambia nikamuuliza kwanini unahitaji mtu mwenye kipara akasema mtu mwenye upara kichwa chake ni dawa ya

kupata utajiri nikamuogopa huyo Mzee mmoja wa ki Zambia na ukiangalia kwa makini hakuna kitu kama hicho

kwenye kutafuta huo utajiri ni imani mbovu za watu. Ni ujinga fulani wa hao wanaotafuta Utajiri kwa njia ya

haraka haraka hakuna kabisa Eti umkate mtu albino kichwa au miguu upate utajiri kwenda zako nani

kakwambia umdhulumu mtu nafsi yake eti wewe uwe tajiri hakuna kitu kama hicho haikubaliki kabisa. Ni

Ukosefu wa elimu, Umasikini na ajira ndio unaochangia watu wachache kufanya ujinga kama huo.
 
Hiyo imani ya kipara lazima itakuwa ilianzia Mbeya. Maana Mbeya ndiyo kitovu cha uchawi africa mashariki kusini na kati. Yaani hizi habari za vipara vina utajiri mimi nimezisikia tangu nikiwa mdogo na tangu wakati huo watu wenye vipara walikuwa hawaonyeshi kabisa. Ninachodhani hapa tatizo ni elimu tu. Hakuna kingine ujinga ukishakuwa mwingi utajikuta unaamini hata vitu ambavyo havipo katika dunia hii.
 
Nchi hii haina polisi, ina sungu sungu! Period! Pole kwa victims.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…