Lakini kitu kingine kilichowastua kupita kiasi hao Sisiem, ni mwamko wa hali ya juu waliouonyesha vihana wa 'kinyalukolo' kule Makambako, mkoani Njombe, ambako hilo zoezi la uandikishaji ndiko lilikoanzia, ambako vijana wengi walikuwa 'wakijihimu' kuamka saa 8 usiku ili kuwahi foleni ya uandikishaji wa kesho yake.
Baada ya hao Sisiem kufanya 'ushushushu' wao wenyewe wakagundua kuwa zaidi ya asilimia 80 ya waliojiandikisha huko wameonyesha dhamira ya kuwapigia kura Ukawa.
Baada ya hao maccm kuligundua hilo, wanaona sasa safari yao 'imeiva' ya kuvifuata vyama vingine viasisi vya nchi jirani, kama vile KANU ya Kenya, UPC ya Uganda na UNIP ya Zambia kuvifuata kule vilikokwenda.