Najivunia kuwa Mtanzania
Mtu mmoja alifariki na kwenda kuzimu. Akiwa huko aligundua kwamba kuna kuzimu tofauti kwa nchi tofauti na akaamua kuchagua mojawapo yenye maumivu kidogo kwa ajili kufaidi ufalme wa kuzimu. Akaenda kuzimu ya Ujerumani na kuuliza "hapa wanafanya je?"
Akajibiwa "kwanza unakalishwa kwenye kiti cha umeme kwa muda wa saa moja.Halafu unalazwa kwenye kitanda chenye misumali kwa muda saa moja nyingine.Halafu anakuja shetani wa Kijerumani na kukucharaza bakora kutwa nzima".Hakukubaliana na hali hiyo akaondoka.
Akaenda kuzimu ya Marekani,Urusi na nyingine nyingi.Akagundua kwamba zote zinafanana na kuzimu ya Ujerumani. Baada ya hapo akaenda kuzimu ya Tanzania, huko alikuta kuna misururu mirefu ya watu wanaosubiri kuingia ndani,akashangaa,akauliza wanafanya nini humo?.
Akajibiwa, "kwanza unakalishwa kwenye kiti cha umeme kwa muda wa saa moja.Halafu unalazwa kwenye kitanda chenye misumali kwa muda saa moja nyingine.Halafu anakuja shetani wa Kitanzania na kukucharaza bakora kutwa nzima. " Akauliza,Lakini hii inafanana kweli na kuzimu za nchi nyingine mbona kuna misururu mirefu ya watu namna hii?
"Akajibiwa ,kwa sababu hakuna umeme hivyo kiti cha umeme hakifanyi kazi na misumali iliyonunuliwa haijaletwa, kwa hiyo kitanda ni kizuri kulalia.Na shetani wa kitanzania ni mtumishi wa umma,ambaye anakuja asubuhi,anasaini kwenye kitabu na kurudi nyumbani kuendelea na shughuli zake binafsi.
Wanajamii naomba tutafakari na kujadili ili tuone kama haya yanayoendelea leo nchini kuhusiana na sakata la mawaziri kama kufukuza na kujiuzulu kwa baadhi yao itakuwa suluhisho la matatizo ya Watanzania kwa sasa.
Epiphan C.P.Kasililwa
0759 440 802,0784 754 963
epiphankasililwa@gmail.com