Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 10,488
- 16,646
Baada ya kuwepo kwa taarifa ya mashambuliano ya siku mbili mpakani mwa Syria na Lebanon kati ya wafuasi wa HizbuLlah na wapiganaji wa serikali mpya ya Syria,sasa tukio hilo limefuatiwa na mapatano katika ya pande hizo mbili.
Kiasili wapiganaji ya HizbuLlah ni wafuasi wa mrengo wa kishia wakati wale wa serikali mpya ya Syria ni upande wa sunni.
Mapatano hayo yanaweza yasiependezeshe serikali ya Israel ambayo katika siku za karibuni imekuwa ikitafuta nyufa kwenye serikali ya Syria ili isitawalike baada ya kuwa wameteketeza kiasi kikubwa cha silaha zilizoachwa na utawala wa Bashar al Assad
Si kutafuta nyufa pekee bali imekuwa ikiichochea seriakali hiyo mpya iingie nayo kwenye vita mapema na kuchagua makundi ya kuwaunga mkono ili waanzishe vita vya wenyewe kwa wenyewe ndani ya Syria.
Wiki iliyopita Israel ilichagua wazee wapatao 45 kwa madhehebu ya Druze waingie Israel kukutana na wenzao wa huko japo kitu kama hicho hawakukiruhusu kwa zaidi ya miaka 50.
Israel imeweka marufuku kwa serikali mpya ya Syria kuweka vikosi vyake eneo la kusini la Syria ambako watu hao wanapatikana zaidi ikisema inafanya hivyo ili kuwalinda dhidi ya ukandamizaji unaoweza kutokea kutoka kwa serikali mpya ya Syria.
Kwa ufupi makubaliano kati ya Hizbullah na serikali mpya ya Syria ni kitisho kingine kwa Israel ambayo baada ya kuondoka kwa Bashar Al Assad imejiona kama imeruka matope na kukanyaga maji ya machafu.
Mapatano kati ya makundi ya kishia na kisunni ndiyo yale yale yaliyofanya vita vya kuikamata na kuitawala Gaza kuwa vigumu katika historia yao kwani makundi hayo yamekuwa yakipigana bega kwa bega na kuwa na ushirikiano wa kila aina kwa kipindi chote kigumu cha vita.
Kiasili wapiganaji ya HizbuLlah ni wafuasi wa mrengo wa kishia wakati wale wa serikali mpya ya Syria ni upande wa sunni.
Mapatano hayo yanaweza yasiependezeshe serikali ya Israel ambayo katika siku za karibuni imekuwa ikitafuta nyufa kwenye serikali ya Syria ili isitawalike baada ya kuwa wameteketeza kiasi kikubwa cha silaha zilizoachwa na utawala wa Bashar al Assad
Si kutafuta nyufa pekee bali imekuwa ikiichochea seriakali hiyo mpya iingie nayo kwenye vita mapema na kuchagua makundi ya kuwaunga mkono ili waanzishe vita vya wenyewe kwa wenyewe ndani ya Syria.
Wiki iliyopita Israel ilichagua wazee wapatao 45 kwa madhehebu ya Druze waingie Israel kukutana na wenzao wa huko japo kitu kama hicho hawakukiruhusu kwa zaidi ya miaka 50.
Israel imeweka marufuku kwa serikali mpya ya Syria kuweka vikosi vyake eneo la kusini la Syria ambako watu hao wanapatikana zaidi ikisema inafanya hivyo ili kuwalinda dhidi ya ukandamizaji unaoweza kutokea kutoka kwa serikali mpya ya Syria.
Kwa ufupi makubaliano kati ya Hizbullah na serikali mpya ya Syria ni kitisho kingine kwa Israel ambayo baada ya kuondoka kwa Bashar Al Assad imejiona kama imeruka matope na kukanyaga maji ya machafu.
Mapatano kati ya makundi ya kishia na kisunni ndiyo yale yale yaliyofanya vita vya kuikamata na kuitawala Gaza kuwa vigumu katika historia yao kwani makundi hayo yamekuwa yakipigana bega kwa bega na kuwa na ushirikiano wa kila aina kwa kipindi chote kigumu cha vita.