Wengi wanaotetea mfumo huu wa utawala wanafaidika nao...
Wengi wasiofadika nao wakilalamika wanaonekana si wazalendo.
Bunge halitimizi wajibu wake wa kusimamia Serikali ( wabunge wa upinzani wanapeleka hoja binafsi zinakataliwa)
Mahakama hazipo huru kihivyo kwa kuwa tumeona mhimili wa utendaji ukisigina Katiba lakini mihimili wa Haki unaona haya kuhukumu vinginevyo.
Njia zote za kujaribu kupata haki zimebinywa ukiwamo uhuru wa kupata na kutoa Habari.
Vyama vya upinzani marufuku kufanya siasa za wazi.
Hivi Nyie mnataka watu wafanye nini? Mnataka waitishe maandamano risasi za moto zirindime?