Hivi ukipigiwa simu kwa 'wrong number' lazima utukane!?

Hivi ukipigiwa simu kwa 'wrong number' lazima utukane!?

K 4 LIFE

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2015
Posts
2,567
Reaction score
419
Kuna kasumba fulani sio ya kiustaarabu, eti mtu akikosea namba ya simu akapiga kwa wrong number ni lazima umtukane?

Utasikia mshenzi mkubwa ukome kupiga namba za watu hovyo hovyo, kana kwamba amekupigia makusudi kumbe kakosea kwa bahati mbaya.

Jamani tuache huu upuuzi kwani unaweza kumtukana mkweo bila kujijua, acheni hizi tabia za kipuuzi.
 
Ha ha ha.... hii imenikumbusha kichekesho cha Anne Kansiime(U Tube), alipopigiwa... akaambiwa ni wrg#, subiria kasheshe sasa....
 
jamani kuna kasumba fulani sio ya kiustaarabu, eti mtu akikosea namba ya simu akapiga kwa yaani wrong number ni lazima umtukane? utasikia mshenzi mkubwa ukome kupiga namba za watu hovyo hovyo, kana kwamba amekupigia makusudi kumbe kakosea kwa bahati mbaya. jamani tuache huu upuuzi kwani unaweza kumtukana mkweo bila kujijua, acheni hizi tabia za kipuuzi nyambafu

Katika kitu ambacho watanzania ni Hodari ni Kupigiana simu tu, Utakuta mtu anakupigia simu saa Sita Usiku ukimuuliza vipi unama ndugu yangu Haa! nilikuwa nakusalimia.
 
Hakuna kitu kina maudhi kama vile mtu anakupigia simu ukipokea anauliza we nani? Kwani kama hakujui anakupigia wanini? Jitambulishe mimi fulani eleza shida yako kama wrong number nitakujulisha umekosea namba.
 
Mtu unamuelewesha kuwa umepiga wrong namba hakuelewi analazimisha kuwa hajakosea. Au analazimisha kujua wewe ni nani. Matusi lazima yakuhusu
 
Mimi huwa napigiwa sana wrongly ila wanaonipigia ile napokea tu wanaanza kucharanga kilugha gani sijui kama mashine huwa nabaki taaban kwa kicheko.
 
hao watu ni wapumbavu, kwa nini utukane? civilization zero
 
Kuna kasumba fulani sio ya kiustaarabu, eti mtu akikosea namba ya simu akapiga kwa wrong number ni lazima umtukane?

Utasikia mshenzi mkubwa ukome kupiga namba za watu hovyo hovyo, kana kwamba amekupigia makusudi kumbe kakosea kwa bahati mbaya.

Jamani tuache huu upuuzi kwani unaweza kumtukana mkweo bila kujijua, acheni hizi tabia za kipuuzi.
Inategemea aliyekosea kaingia kwa style gani, maana utakuta hana ustaraabu anaanza kukuuliza we nani! Unajaribu kumwelewesha hakuelewi kitakachofuata hapo malizia mwenyewe
 
Kuna kasumba fulani sio ya kiustaarabu, eti mtu akikosea namba ya simu akapiga kwa wrong number ni lazima umtukane?

Utasikia mshenzi mkubwa ukome kupiga namba za watu hovyo hovyo, kana kwamba amekupigia makusudi kumbe kakosea kwa bahati mbaya.

Jamani tuache huu upuuzi kwani unaweza kumtukana mkweo bila kujijua, acheni hizi tabia za kipuuzi.

Hapo ni sawa ila mimi napingana na wale wanaokupigia simu tena namba mpya halafu et anakuuliza wewe ni nani??? Hasira na mzuka unanipanda zaidi pale unapo muuliza ajitambulishe badala yake anakataa anang'nga'nia kuuliza wewe ni nani kwa kweli na mazito halafu namkatia simu.jumla
 
wakuu mwenye kile kichekesho cha msukuma akimtukana demu aliekosea namba "sikuwowi kago.ngwe na ppobawa" naomba antumie
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom