kalongo kalongo
New Member
- Mar 11, 2019
- 1
- 1
Wananchi wa Tanzania tumekuwa na changamoto za kimaisha kwa muda mrefu hasa katika kupanda kwa bei za bidhaa muhimu kwa matumizi ya kila siku. Ukiangalia bei za vifurushi katika mitandao yetu ya simu inapanda kila uchwapo, mafuta ya diesel, petrol, na nishati mubadala yaani gesi bei juu. Sasa na TANESCO wanaona wasiachwe nyuma katika kupandisha bei ya unit kinyemela . Kila Mtanzania yuko kimya kama haya mambo hayatokei nchini mwetu. Nashauri kuazishwa kwa vikundi vya utetezi mfano chama cha watumiaji wa umeme, au simu, gesi na mafuta ili pale mashirika haya yakipandisha bei, wawepo kututetea na kupinga ongezeko lolote la bei ili hali kipato cha Mtanzania kinazidi kushuka kutokana na kushuka kwa sarafu yetu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app