Hivi TRC kweli wataweza kuendesha Treni za kisasa?

Kwa kumbukumbu zangu ilishawahi binafsi shwa hii TRC kwa wahind walifel wapi,tuanze hapo.
 
Ngoja tujifunze kwa ATCL kwanza. Wakiweza basi na TRC wataweza tena kwa kishindo.
 
TRL
TBC
TTCL
ATCL
TANESCO

Hawa watoto wa baba mmoja na ndugu zao ambao sijawataja ni matatizo matupu
 
Naafikiana na wazo la kuwapa wanaoijenga kuiendesha,
Hivi reli ya zamani itaondolewa au wanaiacha kama historia
reli ya zamani itabaki na itakuwa inatumika, kwa mfano, stesheni ya dar itajengwa kwa mfumo wa ghorofa, treni ya sgr, itafika stesheni upande wa juu ghorofani, hivyo abiria watapanda na kushuka treni mpya wakiwa ghorofani na ile treni ya zamani itabaki upande wa chini, kuserve wale ndugu zetu wanaoendelea kwenda ubungo na pugu, itaserve maneo madogomadogo ya wakazi (commuters)
 

Nashukuru Mkuu, je vipi kuhusu reli hiyo kongwe kuanzia Pugu na kuendelea hadi Kigoma, Mpanda, Mwanza nk
 
Nashukuru Mkuu, je vipi kuhusu reli hiyo kongwe kuanzia Pugu na kuendelea hadi Kigoma, Mpanda, Mwanza nk
wa mikoani nao watapambanua waitumie vipi huko kote, naamini sehemu kama morogoro ama dodoma nao wataanzisha safari za ndani kwa ndani kutumia reli hiyo, naamini
 
Kama mtanzania anaweza kurusha ndege ndio hiyo treni?
Nyinyi mibavicha ni mivivu ya kufikiri na kila kitu walahi
Pathetic DNA
 
Kama mtanzania anaweza kurusha ndege ndio hiyo treni?
Nyinyi mibavicha ni mivivu ya kufikiri na kila kitu walahi
Pathetic DNA


Kwenye ndege kuna nidhamu kwasababu ya kanuni na sheria za kimataifa za usalama, lakini kwenye nchi kavu kwakuwa ni usafiri wa ndani basi kunakuwa na elements nyingi za uzembe mwingi
 
Ndio maana Wanatakiwa kunyooshwa

Hizi slogan za kuwanyoosha ni slogan za watu walewale wasiojua cha kufanya.

Huwezi kuniambia Vodacom, Airtel, Tigo yanafanya vizuri kuliko TTCL kwa sababu haya makampuni yanawanyoosha watumishi wao na TTCL haiwanyooshi.

Ki msingi mfumo mzima wa umma umeshakuwa corrupted ni vigumu kuunyoosha na ndio maana wanashauri serikali kujitoa kwenye shughuli za kiuchumi. jenga sekita binafsi wakopeshe mitaji wafanye wakurudishie mitaji yako kwa riba, wakulipe kodi na watengeneze ajira kwa watu wengine.
 
Huko Voda,Tigo na airtel unadhani wafanyakazi wakikosa tija au kuleta hasara unadhani wanaachwa kazini?
 
We jamaa njoo huku uchukue malalmiko ukaywasilishe Kwa Kadogosa
Tanzania Railways Co.
 
Kama mtanzania anaweza kurusha ndege ndio hiyo treni?
Nyinyi mibavicha ni mivivu ya kufikiri na kila kitu walahi
Pathetic DNA

Tatizo la nchi yetu ni vyama vya siasa kutengeneza wahuni wa propaganda ambao hawajui chochote kinavyoendelea bali kazi zao ni kukaa kwenye mitandao kutengeneza propaganda kwa maana ya kupinga au kusapoti.

ungekuwa ni mtanzania unayefanya kazi na umeona utendaji wa hizi taasisi, hata angalau umetumia mabasi ya watu binafsi kama abudi ukaona jinsi unavyokwenda kukata tiketi unavyopokelewa, unapewa tiketi kwa kutajiwa mda kamili na jinsi mtu anavyosafiri confortable. Sio swala la ugumu au technolojia ya hali ya juu bali commitment na nidhamu ambayo mtu binafsi mmoja amefanikiwa kuijenga kwenye biashara lakini

Lakini je hawa wahuni wametumia usafiri kama wa treni huu wanaoendesha TRC?

hapa tunachokizungumza ni kumpa mtu nafasi alafu anatangaza nafasi za ajira lakini wanaoajiriwa ni wenye "god father" na sio waliotoka kwenye usaili. Mtu anaanza kazi akijua mimi nimeletwa na mtu fulani basi anawadharau wote hasikilizi.

Hata sekita binafsi wana manapeana ajira kwa kujuana lakini kule wana machungu na mitaji hivyo wanasimiana ili wapate tija, mali za serikali huwa ni kama mali zisizo na mwenyewe hivyo watu hawana machungu.

Hebu tazama jengo la machinga complex limetumia shilingi ngapi? lakini kama hizo fedha angekuwa amekopa mtu binafsi kwanza kuzikopa angetakiwa kuweka mali zake rehani. hiyo tu ingemfanya kuwa makini tangu hatua ya mwanzo katika kupendekeza mradi kutazama mradi ambao una tija na angeusimamia uzalishe na sio kutumia mabilioni na kutengeneza kitu kisicho na tija.
 
Kwa kumbukumbu zangu ilishawahi binafsi shwa hii TRC kwa wahind walifel wapi,tuanze hapo.

Nadhani tatizo kubwa tulilo nalo sisi ni jamii yetu imekwisha jengeka vipi?

Sio kwamba "Serikali" haiwezi kuendesha vitu hivi kwa ufanisi bali tunapozungumza nchi yetu hapa tulipo hoja ni yeyote utakayempa kazi ya kuendesha shirika hili yale majukumu ya msingi anayaweka pembeni anabeba mengine.

mfumo wetu wa recruitment haulengi katika kutafuta yule ambaye ni bora vilevile hata katika kutafuta private operator tunafanya vimbwanga vilevile. Wahuni wasiojua kitu wanaojua kuhonga ndio wanaoshinda zabuni.

Wataalamu wanaokaa kuandaa proposal zao kitaalamu wanaishia kuzungushwa tu. Hivyo tusichukulie kuwa shirika hili lilikwisha binafsishwa na wahindi wakashindwa bali tutazame kutafuta au kutengeneza shirika la binafsi liendeshe.

Wauzieni tuwakusanye wanaoendesha mabasi yao kwa ufanisi hapa kwetu tuwauzie shea hata kwa kuwakopesha na wao ndio wawe operator.

Tuachane na upuuzi wa kumpa operator masharti eti ya kuchukua wafanyakazi wote wa mashirika haya ambayo wao wamekwisha zoea kuiba mafuta ya kuendeshea ndiyo njia baadhi wanajua inawatoa kimaisha sio mishahara, wamezoea kufanya ujanja kwenye mifumo ya tiketi.

ukifika kituoa cha treni unapima mzigo unawakabidhi lakini sasa wanakwambia eti mzigo ulio mikononi mwao wao hawapakii hivyo utafute wabebaji upatane nao ili hao wabebaji ndio wapakie na usipopatana nao mzigo wako hauji. Gharama ya kusafirisha mzigo kwa treni ukipiga mahesabu ya gharama za treni ziko chini kulinganisha na mabasi au magari lakini ukiweka gharama hizi za wapakiaji ambao ni binafsi gharama zinakuwa juu kuliko kutuma mzigo mdogo kwa magari.

Vipo vikorokoro vingi ambavyo ukimleta private operator unatakiwa umwachie huru ili akabiliane navyo na kubwa ni kuvunja mitandao iliyokuwa ndani ili atengeneze mifumo yake lakini serikali imekuwa "blind" kugangania kuwalazimisha waendeshaji kuchukua wafanyakazi wote wa zamani katika mashirika haya na ndiyo kimekuwa chanzo kikubwa cha kushindwa kuwadhibiti.

ATCL walileta mwekezaji kutoka afrika kusini wakampa masharti yale akashindwa

TRL walileta mwekezaji kutoka india matokeo yaleyale.

Yaani ni sawa na mtu amekuwa na shamba ana watumishi na kila akiingiza mtaji watumishi wanakula hapati mavuno alafu anatafuta mtu wa kuendesha shamba eti anampa masharti ya kuwabakiza watumishi wake hawa wote????? unategemea nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…