Haijakosewa tukiangalia kwenye "Modus Operandi" yenyewe ya TRA, hilo neno "Revenge or Retaliation" lina correct linguistic meaning.
Neno "Mamlaka" yenyewe linatokana mfumo halisi wa "Kibebari" na Ukoloni, vitisho, ushirikisho, kushuritishwa bila hiyari nk. Hii imetokana na masharti ya mikopo ya IMF. Masharti ya Bwana Mkubwa.
Kaisari aliwapa watu wake kila kitu, maji safi, afya bora, elimu, ardhi nk na watu walimpa kodi Kaisari kwa mapenzi yao wakijua haki zinatendeka.
Rasilimali au maliasili tuliyokuwa nazo katika hii nchi yetu, suala la kodi au kutegemea kodi ya mapata kutoka kwa wananchi maskini ili kuendesha shughuli za serikali, ilikuwa inatakiwa iwe 2nd option.
Kodi tunazozilipa ni zetu, kwa ajili ya huduma zetu za kijamii, Serikali imechukua dhamana kufanya kazi hizo. Wananchi tunatakiwa kuiwajibisha Serikali kuwa na utawala bora ili itutendee haki, tupate yale ya muhimu kutokana na thamani ya kodi zetu. Tuiwezeshe Serikali, na Serekali ituwezeshe. We work together. Kama Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta anavyosema "Think Big"