Hivi suala la kukagua mizigo kwa abiria wa ndege domestic arrivals Tanzania, nalo ni amri ya Magufuli?

Synthesizer

Platinum Member
Feb 15, 2010
11,208
19,001
Tanzania haiishi vioja. Kimojawapo ya kioja kinachoendelea, ambacho huenda kikatuingiza kwenye Guiness Book of World Records of Ridiculousness, ni hili linalofanyika kwenye airport za Tanzania kwa sasa, ambapo abiria wanaosafari safari za ndani ya Tanzania, wanapowasili wanapokwenda, wanatakiwa wakaguliwe mizigo waliyotoka nayo mwanzo wa safari yao ndani ya Tanzania!

Yaani mtu anasafiri kwa ndege kutoka Mwanza kwenda Dar, au Dar kwenda Arusha, Dar kwenda Mwanza, na akifika mwisho wa safari yake, anaambiwa mizigo yake lazima ikaguliwe! Na hata anaulizwa umebeba nini ndani ya begi. Kumbuka kwamba hili si kwa ajili ya usalama wa ndege, maana mtu unakuwa umewasili na kushuka toka ndani ya ndege ndio unakaguliwa mizigo!

Ukiwauliza wafanyakazi wa airport kwa nini wanakagua mizigo ya domestic flight arrivals, na ni nini wanachotafuta, wanakuambia "wanatekeleza maagizo toka juu".

Sasa ninachojiuliza ni kama haya maagizo toka juu ni kutoka kwa Raisi Magufuli katika busara zake za kuiongoza Tanzania. Je, ni katika mkakatati wa kuzuia usafirishaji wa madawa au madini? Ni kama ndivyo, je haijaingia akilini kwamba hizi ni domestic flights ambazo kama nina mali ya magendo na nikijua kuna ukaguzi airport nitatumia mabasi au usafiri mwingine? Kama wanadhani kuna umuhimu wa kukagua mizigo ya domestic flights, tufikirie kwamba kuna siku katika stand za mabasi ya mikoani tutaanza kukaguliwa mizigo tunapowasili kutoka Mbeya, Mwanza, Tabora nk?

Kwa kweli vitu vingine havihitaji uwe na elimu ya PhD kuona kwamba ni vitu vya kijima, vya kukurupuka, havina lojiki, vinaleta usumbufu usio na maana na vinaamuliwa bila kuwa na uwezo makini wa kufikiria mambo.

Nakumbuka aliporudi mara ya pili JKNIA kumtafuta yule mkaguzi mwanamke aliuliza kwa nini internal arrivals hawakaguliwi. Na akaagiza hapohapo ukaguzi uanze mara moja.
 
Sidhani jamii yoyote inayoweza kuendelea bila ya kuaminiana kwanza, sasa kama hawawaamini waliokagua wakati wa kupanda ndege, pia hawakuamini mwenye mzigo watamuamini nani sasa ...na wao ni nani mpaka wasiwaamini wenzao!?
 
Inashangaza sana yaani umetoka Dar umekaguliwa vizuri hauna shida yoyote unafika Mwanza tena unakaguliwa??? mmh

Kweli Kabisa Mkuu. Ndio maana nikasema kukaguliwa kabla ya safari ni jambo la kawaida, na kwa domestic flights ni suala la kiusalama tu. Sasa mtu umefika mwisho wa safari ya domestic flight, wanakukagua, unaulizwa umebeba nini toka Mwanza kuja Dar, au Mbeya kuja Dar, sasa hiyo ni akili kweli? Ndio maana siku zote nasema tatizo kubwa tulilonalo Tanzania ni akili ndogo kuwa na mamlaka makubwa!
 
Poor minds

Poor minds - that is normal. In any society there will always be a good percentage of poor minds. Leaders with poor minds - totally unacceptable! Sycophants even worse. Tanzania is fast becoming a country of sycophants.

So hii issue ya kukagua mizigo ya domestic flight arrivals kuna mawili - the results of a poor mind decision, or the work of a sycophant.
 
Binadamu ni kiumbe mwenye akili sana endepo wewe utaona ni kawaida. na si kila agizo mtu akisema limetoka juu basi limetoka kwa rais.
 
Kweli Kabisa Mkuu. Ndio maana nikasema kukaguliwa kabla ya safari ni jambo la kawaida, na kwa domestic flights ni suala la kiusalama tu. Sasa mtu umefika mwisho wa safari ya domestic flight, wanakukagua, unaulizwa umebeba nini toka Mwanza kuja Dar, au Mbeya kuja Dar, sasa hiyo ni akili kweli? Ndio maana siku zote nasema tatizo kubwa tulilonalo Tanzania ni akili ndogo kuwa na mamlaka makubwa!
Huo utaratibu sio mzuri na hata kama ni ishu ya usalama...Kama umetoka Dar umekaguliwa uko salama ina maanisha hujabeba mzigo au kifaa chochote ambacho ni hatarishi kupanda nacho ndege sasa iweje ufike tena Mwanza kama sio kupotezeana muda na usumbufu ni nini huko?? Mamlaka husika ziangalie hili suala kwa makini, labda kama kuna sababu nyingine ya msingi
 
Ila sio ukaguzi mkali kama wakati wa kuondoka point A...ni kupitisha mzigo wako kwenye mashine na kuendelea na utaratibu wako mwingine kitu ambacho hata kabla ya JPM ilikuwa wakati mwingine unakuta mtu amesimama anakagua kama mzigo uliokuwa nao ndo ule ambao umeainishwa kwenye boarding pass
 
Binadamu ni kiumbe mwenye akili sana endepo wewe utaona ni kawaida. na si kila agizo mtu akisema limetoka juu basi limetoka kwa rais.
Ndio maana Mkuu nimeuliza hili nalo limetoka kwa Magufuli? Kama kweli limetoka kwa Magufuli basi linanifanya nitilie shaka uwezo wa Raisi wetu wa kutafakari mambo kabla ya kuyatolea amri, na binafsi nitamuona ni rahisi ambaye sasa anazidi mipaka. Kama halijatoka kwake basi ni wazi tuna tatizo na watendaji wake wa chini ambao sasa wanaamua mambo kwa kujipendekeza na uoga badala ya busara (sycophants), na kufanya watu wazidi kumkasirikia Raisi Magufuli wakidhani yeye ndio analeta usumbufu huu usio na maana, pua wala mdomo.
 
Ila sio ukaguzi mkali kama wakati wa kuondoka point A...ni kupitisha mzigo wako kwenye mashine na kuendelea na utaratibu wako mwingine kitu ambacho hata kabla ya JPM ilikuwa wakati mwingine unakuta mtu amesimama anakagua kama mzigo uliokuwa nao ndo ule ambao umeainishwa kwenye boarding pass
Uwe mkali au usiwe mkali, ni usumbufu ambao hauna maana wala hausaidii chochote. Umeona foleni inavyokuwa ndege mbili au tatu za domestic zinapoingia pamoja? Na kwa nini kama una akili timamu uweke vitu ambavyo havina ulazima wa kufanya na ukiona wazi vinaleta usumbufu?
 
Ndio maana Mkuu nimeuliza hili nalo limetoka kwa Magufuli? Kama kweli limetoka kwa Magufuli basi linanifanya nitilie shaka uwezo wa Raisi wetu wa kutafakari mambo kabla ya kuyatolea amri, na binafsi nitamuona ni rahisi ambaye sasa anazidi mipaka. Kama halijatoka kwake basi ni wazi tuna tatizo na watendaji wake wa chini ambao sasa wanaamua mambo kwa kujipendekeza na uoga badala ya busara (sycophants), na kufanya watu wazidi kumkasirikia Raisi Magufuli wakidhani yeye ndio analeta usumbufu huu usio na maana, pua wala mdomo.
ye anaweza kusema ongezeni ulinzi/ukaguzi,hayo mengine wenye kamati ndo wanaongeza ili kutekeleza.
Kumbuka tofauti kubwa iliyopo kati ya binadamu na wanyama ni akili
 
ye anaweza kusema ongezeni ulinzi/ukaguzi,hayo mengine wenye kamati ndo wanaongeza ili kutekeleza.
Kumbuka tofauti kubwa iliyopo kati ya binadamu na wanyama ni akili

Nami nahisi hivyo. Na kama ni hivyo basi ujumbe huu na umfikie Raisi Magufuli na tutafurahia kusikia tena neno "Wapumbavu" katika hotuba zake.

"Mimi natoa amri kwamba ulinzi katika airports zetu uongezeke na "wa..vu" wanaenda kusumbua abiria wa ndani ya Tanzania kwa ukaguzi ambao ni usumbufu na hauna tija"

Ila Mkuu, kama suala la ukaguzi wa mizigo ya domestic flight arrivals ni amri ya Raisi, then quote yangu hapo juu, mmmh.
 
Kwa safari za ndani siwezi panda ndege hata niwe na haraka kiasi gani
Heee! Kwa nini mkuu? Siku hizi watu tunakula uroda na Bombardier tumeshasahau mambo ya kupanda mabasi na tochi za trafiki tuki-drive kwenda mikoani!
 
trna ni nzuri sn walichelewa mno kuanzisha huu mfumo sio kila kitu mzungu aanzishe vingine na wao waje wajifunze kwetu
 
Nakumbuka mkuu aliwapiga biti siku Ile pale terminal 1na akasema watu wanakuja Na private jet toka mikoani bila kukaguliwa sasa Nafikir Hawa wamejiongeza wanakagua abiria wote wanaoingia bila kuzingatia kuwa Hawa walikotoka wamekaguliwa kiukweli Ni usumbufu Na nidhamu za uoga zinatumaliza
 
Heee! Kwa nini mkuu? Siku hizi watu tunakula uroda na Bombardier tumeshasahau mambo ya kupanda mabasi na tochi za trafiki tuki-drive kwenda mikoani!
Maamuzi tu na furahi kuona vijiji vya watu na kukutana na watu watofauti na inanisaidia kujua nchi yetu
 
Maamuzi tu na furahi kuona vijiji vya watu na kukutana na watu watofauti na inanisaidia kujua nchi yetu

Mkuu, nimeendesha gari kwenda kwetu zaidi ya mara 20. Sasa kwangu hilo halina maana tena. Na tochi na kusimamishwa na trafiki kila baada ya dakika ishirini vimekuwa kero sasa.
 
Back
Top Bottom