Mkuu mantiki ipo,utakula ulichopanda,sio mambo ya mbuzi kula kutegemea urefu wa kamba yake.
Ukubwa wa serikali haulingani au haufanani na mapato ya serikali.Tuna wabunge wengi kupita kiasi,tuna mikoa na wilaya ziliongezwa kisiasa.Vile vile matumizi mabovu ya pesa za umma ndio kisiki cha maendeleo kwa muda mrefu sasa,labda Magufuri ataondoa hilo.
Kama haitoshi vipaumbele vya maendeleo havikupewa msukumo,msukumo upo kwenye chaguzi sababu kuna pesa za wafadhili.
Raisi Kenyatta anatutambia kwa sababu asili mia kubwa ya bajeti ya Kenya kwa muda mrefu haitegemei wafadhili kama Tanzania na Uganda,ni pesa ya ndani yaani kodi