Hivi Ni Kweli Kabisa TABIA Haina Dawa??.....hebu tujadiliane!!

Mazingira yanachangia bana

Kama umeishi wa watu ambao ni wasafi sana, lazima watakuathiri kiaina
Hebu angalia tu hata wavulana ambao walilelewa na mama mkali, lazima watandika vitanda

Hata wakienda kujitegemea, huwa wanatandika vitanda mara nyingi


Ukarimu ni suala pana zaidi
Lakini hata ukarimu bado unafundishika

Hivi Kongosho UKARIMU unafundishika au ni TABIA ya kuzaliwa nayo??..Na inawezekana mtu akazaliwa na TABIA ya UCHAFU??....
 

Key word iwe ni "MANTIKI" ... yaani LOGIC

Mwanadamu anweza kusukumwa na misukumo miwili tu!! "Mantiki" au "Hulka"

Honestly speaking? Hulka ni kwa ajili ya wanyama na Mantiki ni kwa ajili ya wanadamu kamili!!

LAKINI mwanadamu anaweza kuamua kusukumwa na Hulka ..Hence the foundation of this discussion!!

MTU anaweza kuendeshwa na TABIA ilijengwa na MANTIKI au ilijengwa na HULKA ...!!
 
TABIA = Mazoea yanayotokana na kurudiarudia hali, mwenendo au matendo

HULKA = Tabia ya mtu, mwenendo wa mtu, maumbile. Pengine huluka.

Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili sanifu

Na vipi kuhusu SILIKA (SILKA)?
 
Mkuu Azimio Jipya naona umeamua kuingiza kitu kipya kabisa LOGIC....Na unasema ni aidha tu hiari ya mhusika kujijenga kitabia kwa kutumia hulka au mantiki!!....Hivi unaposema LOGIC sio ndo mambo ya REASONING??...Yaani pale mtu anapofanya jambo kwa kuangalia 'impact' ya jambo kwa hadhira yake au yeye mwenyewe...By the way how Logic to me is also LOGIC to you???

 
Last edited by a moderator:

Nakubaliana na hoja yako kuwa ni HIARI ya muhusika kujijenga kitabia kuotekea minisingi ya Hulka au Mantiki! Lakini nafikiri mziki unaazia hapo ... kwenye tabia za kihulka, naamini tabia zilizojengwa na mantiki hazileti contradiction ... Mfano post ya Kongosho ametoa mfano Mama mkali huwafundisha watoto wa kiume kutandika vitanda ... to me that is logic ... hivi nani haoni kuwa hiyo ni logic? ..mantiki? na it worth kujengwa kwa hao vijana kama tabia yao? Hata kama itagharimu Tough Love(Upendo wenye ukali na msisitizo) refer post ya King'asti
 
Last edited by a moderator:

Hakika kila tabia hubadilika na wa kutoa MWELEKEO ibadilike kwenda kwenye HULKA au MANTIKI ni muhusika. Ni hali ya kawaida ya mwanadamu kuwa na ustaarabu uliojengeka kutokana na thamani za uasili wa kibinaadamu unaojitofautisha na hulka za wanyama wanaojiendesha pasipo mantiki yeyote ile!
 
Hivi Kongosho UKARIMU unafundishika au ni TABIA ya kuzaliwa nayo??..Na inawezekana mtu akazaliwa na TABIA ya UCHAFU??....

inasemekana watanzania ni wakarimu kuliko wakenya

ujamaa umewapelekea wa-tz kuwa hivyo, na wakenya kuwa 'rude' u-capitalist umechangia

hospitality college course zinapelekea watu kuwa wakarimu kwenye kada zao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…