Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Kama kuna habari tunayopaswa kuisikia tena na tena ni habari ya Ujio wa Bwana Yesu Kristo. Hilo ni tukio la hakika na la kutisha kwa wasiomwamini, lakini lenye furaha kuu kwa waaminio. Maandiko yanathibitisha wazi kuwa Yesu atakuja mara ya pili kama alivyokwenda mbinguni. Malaika waliwaambia wanafunzi: "Huyu Yesu, aliyetwaliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni, atakuja vivyo hivyo kama mlivyomwona akienda mbinguni" (Matendo 1:11).
Yesu mwenyewe alisema: "Basi mimi nikienda kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi muwepo." (Yohana 14:3). Yesu alizitaja dalili za kuja kwake. Dalili hizo karibu zote zimetimia:
“Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.” (1 Wathesalonike 4:16-17)
Siku hiyo kuu, tarumbeta maalum ya Mungu italia. Ndipo makaburi ya wale waliofariki katika Kristo yatafunguka, na miili yao itafufuka kwa utukufu. Watakatifu watakaokuwa hai wakati huo, nao watabadilika upesi—kufumba na kufumbua—na kuvaa miili ya utukufu, isiyoharibika. Kisha watakatifu wote, yaani waliokuwa wamefariki na walio hai, watanyakuliwa fasta kwenda kumlaki Yesu mawinguni. (1 Wakorintho 15:51-52). Yesu hatakanyaga ardhi siku hiyo. Ataishia mawinguni na kuwanyakua wateule.
Itakuwaje kwa wasioamini?
Siku hiyo, wasiomwamini Yesu hawatanyakuliwa. Nchi ambazo siku ya tukio hilo itakuwa usiku, kama watu wawili watakuwa wamelala kitandani—mmoja anayeamini atanyakuliwa, mwingine asiyeamini ataachwa (Luka 17:34). Katika maeneo ambayo itakuwa mchana, watu wawili watakaokuwa shambani—mmoja anayeamini atanyakuliwa, mwingine asiyeamini ataachwa (Luka 17:36).
Ghafla dunia itabaki na watu waovu tu. Majengo ya makanisa ya watu wanaoishi maisha matakatifu, yatabaki matupu—hakuna tena kuhubiri, hakuna ibada, hakuna wokovu. Wale waliokuwa wanasitasita kutubu, watatambua wameachwa. Walimu wa Neno, wachungaji, walokole—wote watakuwa hawapo.
Kifuatacho?
Baada ya tukio hilo la unyakuo, ndipo dhiki kuu itaanza, ambayo haijawahi kuwapo tangu mwanzo wa ulimwengu (Mathayo 24:21). Mpinga Kristo atatokea na kujidhihirisha, na kuanza kuwatesa waliobaki. Hakutakuwa na amani. Dunia itatawaliwa na hofu, mateso na mapigo ya kutisha. Waliomkataa Yesu na kupinga kwamba sio Mungu, watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia (Ufunuo 9:6).
Nini sasa kifanyike?
Ndugu yangu, habari hiyo sio hadithi za kutungwa, ni ukweli wa maandiko. Pinga usipinge, Yesu atarudi. Hatujui siku wala saa, lakini atakuja kwa siku watu wasiyoitarajia. Je, utakuwa tayari? Utakuwa miongoni mwao watakaonyakuliwa? Kama huna uhakika, ina maana bado hujaokoka. Amua leo kuokoka, usingoje kesho. Tubu dhambi zako, amini kuwa Yesu alikufa kwa ajili yetu na umpokee sasa kwa imani, awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako. “Tazama, sasa ndiyo wakati uliokubalika; tazama, sasa ndiyo siku ya wokovu.” (2 Wakorintho 6:2)
Ukifanya hivyo, Yesu atakapokuja, utakuwa miongoni mwao watakaonyakuliwa kwenda mbinguni.
Yesu mwenyewe alisema: "Basi mimi nikienda kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi muwepo." (Yohana 14:3). Yesu alizitaja dalili za kuja kwake. Dalili hizo karibu zote zimetimia:
- Upungufu wa upendo na mmomonyoko wa maadili (Mathayo 24:12)
- Vita, njaa, matetemeko ya ardhi, magonjwa ya ajabu (Mathayo 24:6-7)
- Watu wengi kudanganywa na manabii wa uongo (Mathayo 24:11)
- Habari njema kuhubiriwa duniani kote ili iwe ushuhuda kwa mataifa yote (Mathayo 24:14), nk, nk
“Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.” (1 Wathesalonike 4:16-17)
Siku hiyo kuu, tarumbeta maalum ya Mungu italia. Ndipo makaburi ya wale waliofariki katika Kristo yatafunguka, na miili yao itafufuka kwa utukufu. Watakatifu watakaokuwa hai wakati huo, nao watabadilika upesi—kufumba na kufumbua—na kuvaa miili ya utukufu, isiyoharibika. Kisha watakatifu wote, yaani waliokuwa wamefariki na walio hai, watanyakuliwa fasta kwenda kumlaki Yesu mawinguni. (1 Wakorintho 15:51-52). Yesu hatakanyaga ardhi siku hiyo. Ataishia mawinguni na kuwanyakua wateule.
Itakuwaje kwa wasioamini?
Siku hiyo, wasiomwamini Yesu hawatanyakuliwa. Nchi ambazo siku ya tukio hilo itakuwa usiku, kama watu wawili watakuwa wamelala kitandani—mmoja anayeamini atanyakuliwa, mwingine asiyeamini ataachwa (Luka 17:34). Katika maeneo ambayo itakuwa mchana, watu wawili watakaokuwa shambani—mmoja anayeamini atanyakuliwa, mwingine asiyeamini ataachwa (Luka 17:36).
Ghafla dunia itabaki na watu waovu tu. Majengo ya makanisa ya watu wanaoishi maisha matakatifu, yatabaki matupu—hakuna tena kuhubiri, hakuna ibada, hakuna wokovu. Wale waliokuwa wanasitasita kutubu, watatambua wameachwa. Walimu wa Neno, wachungaji, walokole—wote watakuwa hawapo.
Kifuatacho?
Baada ya tukio hilo la unyakuo, ndipo dhiki kuu itaanza, ambayo haijawahi kuwapo tangu mwanzo wa ulimwengu (Mathayo 24:21). Mpinga Kristo atatokea na kujidhihirisha, na kuanza kuwatesa waliobaki. Hakutakuwa na amani. Dunia itatawaliwa na hofu, mateso na mapigo ya kutisha. Waliomkataa Yesu na kupinga kwamba sio Mungu, watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia (Ufunuo 9:6).
Nini sasa kifanyike?
Ndugu yangu, habari hiyo sio hadithi za kutungwa, ni ukweli wa maandiko. Pinga usipinge, Yesu atarudi. Hatujui siku wala saa, lakini atakuja kwa siku watu wasiyoitarajia. Je, utakuwa tayari? Utakuwa miongoni mwao watakaonyakuliwa? Kama huna uhakika, ina maana bado hujaokoka. Amua leo kuokoka, usingoje kesho. Tubu dhambi zako, amini kuwa Yesu alikufa kwa ajili yetu na umpokee sasa kwa imani, awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako. “Tazama, sasa ndiyo wakati uliokubalika; tazama, sasa ndiyo siku ya wokovu.” (2 Wakorintho 6:2)
Ukifanya hivyo, Yesu atakapokuja, utakuwa miongoni mwao watakaonyakuliwa kwenda mbinguni.