kwisha
JF-Expert Member
- Sep 9, 2021
- 1,666
- 4,365
Mimi mwenzenu sijui nimeumbwa na moyo wa namna gani, yaani kuna muda najilaumu kwanini nipo hivi! Mimi huwa sina muda wa kupenda wanawake wengi na siweza kutoka na wanawake wawili kwa kipindi kimoja. Nikipenda ujue nimependa kweli.
Lakini nimejikuta nimekuwa mtu wa kuumizwa na mapenzi sana, tofauti na wale ambao wanakula na kuondoka! Leo nilikuwa na ongea na mpenzi wangu kwenye simu, kwa bahati nzuri tulivyokuwa tunaongea hakukata simu, alifikiri mimi nimekata simu.
Nikaanza kusikia sauti ya kunitukana, alikuwa anaongea na rafiki yake. Eti amenichoka, mimi ni mwanaume gani ambaye sina vituko, muda wote nipo kimya sana kama mtu ambaye anatoa mzigo chooni. Amechoka na hali yangu, sijui anapenda mwanaume ambaye kidogo ana changamsha akili yake.
Mara anasikia yupo na huyu, sijui yupo na yule, ndiyo raha; mimi na yeye kuwa na ugomvi tuna fanya wiki hatuongei sijui. Aliongea mengi sana, hakika nimeumia sana. Nimejikuta dhaifu sana! Kumbe nilivyo na mahaba kwake yeye hapendi.
Naombeni mbinu za kuwa "Bad boy"!
Lakini nimejikuta nimekuwa mtu wa kuumizwa na mapenzi sana, tofauti na wale ambao wanakula na kuondoka! Leo nilikuwa na ongea na mpenzi wangu kwenye simu, kwa bahati nzuri tulivyokuwa tunaongea hakukata simu, alifikiri mimi nimekata simu.
Nikaanza kusikia sauti ya kunitukana, alikuwa anaongea na rafiki yake. Eti amenichoka, mimi ni mwanaume gani ambaye sina vituko, muda wote nipo kimya sana kama mtu ambaye anatoa mzigo chooni. Amechoka na hali yangu, sijui anapenda mwanaume ambaye kidogo ana changamsha akili yake.
Mara anasikia yupo na huyu, sijui yupo na yule, ndiyo raha; mimi na yeye kuwa na ugomvi tuna fanya wiki hatuongei sijui. Aliongea mengi sana, hakika nimeumia sana. Nimejikuta dhaifu sana! Kumbe nilivyo na mahaba kwake yeye hapendi.
Naombeni mbinu za kuwa "Bad boy"!