Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,145
- 162,545
- Thread starter
- #21
Ni kweli hata maandiko yanadhihirisha mtu mweusi ana tatizo la asili na ukichunguza utagundua tumeumbwa kuwa watumwa wa hawa wenzetu na ndio maana hata hizi rasilimali zetu tunazimililikisha kwa watu weupe sisi wenyewe ili waendelee kututawala.Ziko hadithi za mapokeo kuhusu early civilization, kuwa asili ya mtu mweusi ni mmoja kati ya wana watatu wa Nuhu baada ya gharika, yaani Ham, Shem na Japhet, mmoja alikuwa mweusi, baba yao alipozeeka, kuna siku alikaa vibaya, mtoto mmoja akamchungulia tuu, bila kufanya chochote, mtoto mwingine, akamwita mwenzake ili washauriane cha kufanya, yule wa tatu kuona tuu hali ile, kwanza alikwenda kumsitiri, hiyo mmoja akabarikiwa sana, ndio wazungu, wa pili akabarikiwa kidogo, ndio Asians, na watatu alilaaniwa, ndio Africans!.
Kiukweli kabisa, civilization ilianzia Africa, Egypt, hata Yesu alikulia Misri. Ukisoma historia ya zama za kale za mawe, zama za kati, zama za chuma, utakutana na dola la Axum, wakati huo ulaya ni pori tupu.
Hata sasa, barani Afrika, nchi ya kwanza kwa utajiri wa dhahabu ni Ghana, lakini leo nenda Ghana kaangalie maisha yao!.
Hapa Tanzania eneo tajiri kabisa kuliko eneo lolote jingine ni Usukumani, ndiko kwenye dhahabu yote na almasi yote, lakini leo nenda Kahama ukashuhudie maisha ya masikini Wasukuma wa pale ulinganishe na utajiri wao!. Nenda Mwadui ambako Wasukuma almasi walikuwa wanazichezea bao!.
Kiukweli kabisa ni kama tumelaaniwa vile!.
P
Utagundua pia hata elimu ya darasani tuliopata bado haifua dafu dhidi ya tatizo hili la asili (laana kama ulivyoeleza ).
