Ni mojawapo ya mashirika kongwe linaloendelea kupumua, ni shirika linalojulikana hata kwa watoto wadogo.
Lakini limekuwa kichefuchefu na headache kubwa kwa taifa na wananchi kwa ujumla, kila mahali kila kona ni malalamiko juu ya Tanesco, kama sio kwenye kununua umeme, basi ni kupoteza pesa kwenye luku, kama sio huko basi ni matatizo ya low voltage, kukatikatika kwa umeme, umeme kuongezeka na kupungua ghafla, kufungiwa umeme, kuripoti dharura, hakuna penye afadhali.
Huwezi kwenda tanesco ukatoka kwa furaha ni shirika lililojajaa madudu kwa kiwango chake, lakini hii yote inasabibishwa kwakuwa hatuna mbadala wa nishati na mbadala uliopo ni ghali umeme wa sola na jenereta.
Miaka ya nyuma tuliteseka sana na mashirika ya simu, TTCL, bima NIC, na DAWASA/DAWASCO, Hizi huduma zilikuwa kizungumkuti hasa lakini baadae kukawa na mibadala siku hizi tuna makampuni mengi tu ya bima na simu hakuna kuringa tena, upande wa maji tuna mbadala wa visima japo hili bado halijakaa sawa sana lakini kuna nafuu
Sasa ni zamu ya Tanesco, hili shirika limezidiwa linahitaji mshindani/ washindani nchi inakuwa kwa kasi kuna ongezeko kubwa sana la mahitaji ya nishati hii muhimu, na kwa hali ilivyo Tanesco hawana uwezo wa kulipa nishati ya kutosha hili taifa.
Tunahitaji mbadala/mshirika wa Tanesco sasa.