Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 414
Habari za kukamatwa na kufunguliwa mashitaka yanayodaiwa kuwa ya uchochezi. Lakini kinachonishangaza ni nguvu nyingi inayotumiwa na serikali katika suala la Ponda. Kwa mfano leo alifikishwa mahakamani morogoro na msafara wa magari 5 yaliyobeba askari wenye silaha na pia kusababisha baadhi ya barabara mjini morogoro kufungwa. Hivi kweli rasilimali zinazotumika kwa suala la huyu mtu , muda unaotumika na inconvinience wanayopata raia wengine vina tija kwa taifa hili? Nadhani kuna mambo ya maana zaidi yanayohitaji kushughulikiwa kwa nguvu na rasilimali nyingi kuliko hili...Ni mtazamo wangu tu.